MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,171
Lengo la kuomba kazi ktk chama tawala ni baada ya kuona kwamba, chama hiki kikongwe hakijui tatizo lake. CCM hawajui matatizo yao kwa kukosa watu wenye ufahamu au kwa kukosa watu wenye kusema ukweli. Hebu angalia maamuzi ya hivi karibuni na tutafute sababu zake;
CCM walisema na wanasema walishinda kwa asilimia 60 na zaidi kidogo. Je, hilo ni tatizo kiasi cha kuanza kuvuruga vyombo vyao vya utawala? Au tuamini maneno ya CHADEMA, kwamba CCM hawakushinda kwa kura? Yaonekana wanajua kilichotokea na wanaanza kutafuta mbinu za kurudisha imani ili washinde kihalali.
CCM wamejivua gamba au niseme ndo wameanza kujivua gamba maana hawajafika kwenye tatizo, ingawa pia sijui kama wanafahamu maana ya hayo maneno. Lakini;
1. Je, tatizo wanalijua?
2. Je, nini lengo la hayo manjonjo wanayoyaonyesha na kujidai eti kujivua gamba?
Majibu ya maswali hayo ni kwamba;
1. Naamini CCM hawalijui tatizo lao, hivyo hawawezi kujivua.
2. Ktk kujivua wana lengo baya, ovu na la kinafiki.
Hapo ndo naanza kuomba kazi ili niwasaidie kutatua yanayowasibu, kama watapenda.
CCM hawajui ni kwa nini wa-Tz wamewaacha. Naomba niwambie CCM kwamba wa-Tz wamewaacha kwa sababu siyo chama chao. CCM kimekuwa chama cha koo fulani-fulani. Milango ya kuingia ktk chama ilishafungwa kwa wasiyokuwa na majina ya koo hizo.
Vijana kwa kufahamu hilo na kwa kupenda kuchangia ktk siasa za nchi yetu, wameamua kujiunga na vyama vyenye milango iliyo wazi, kuingia na kutoka! Bahati nzuri vyama kama hivyo ni vingi.
Kwa kutojua tatizo lao, bado CCM wanaunda upya uongozi wao kwa kuingiza majina yaleyale ya koo hizo-hizo. Akina Makamba akina Nape, akina Mukama na wengine wanatakaokuja. Naamini hata akina Kikwete mdogo wako njiani kuingia. Wao wanasema wanajivua gamba.
Lakini hebu angalia nyuma kidogo uone sababu ya kufanya hivyo.
Mpaka mwisho wa kampeni za uchaguzi wa 2010, CCM walijinadi na kusema wako imara na hawana tatizo. Wakituambia wote tunaowakosoa ni kwa kukosa ufahamu. Wakaendesha uongo wakidhani ndo propaganda mpaka ndani ya JF wakazuka wachangiaji wa kila siku ambao leo hii hawaonekani. Ninachokiona ktk maamuzi yote wanayotuonyesha sasa hivi ni unafiki kwamba eti wamegundua makosa yao. Eti ghafla wamechukia ufisadi. Miezi 6 iliyopita hata Kikwete alionywa juu ya tabia ya kuwatetea mafisadi ktk majukwaa ya kampeni lakini masikio yalikuwa yameziba. Iweje leo hii masikio yake yazibuke wakati kelele zimekwisha pita?
CCM bado hawachukii mafisadi. Wanajidai kuchukia ufisadi ili tuwafurahie. Mbona hawafungui milango yao? Mbona wanarudisha watoto wao na babu zao ktk utawala?
Kama CCM hawataki kutuajili ili chama kifufuke, basi hata CCM ya Mukama itakufa tu!