Jazmine
Member
- Oct 29, 2011
- 25
- 8
Umri wangu ni miaka ishirini na mmoja. Wazazi wangu hawakuwahi kuoana wala kuishi pamoja kwani nilipokuwa conceived (wazazi) wangu walikuwa bado kwenye late teens, wakati huo wanafunzi. Katika mazingira hayo, umri wangu wote nimelelewa na familia ya mama yangu kisiwani zanzibar katika maadili ya kiislamu.
Kwa ung'ang'anizi wangu, Mwaka jana nimefanikiwa kumshawishi mama yangu mpaka akanikutanisha na baba yangu.
Yeye Mkristo na maisha yake yote ni Tanzania Bara, sababu familia ya mama'ngu hawakutaka aibu ya familia wala mahusiano na mawasiliano yeyote na baba'ngu. Nililelewa nao na kusomeshwa mpaka umri huu, ingawa mama'ngu amekiri mbele ya baba'ngu kwamba kwa takriban miaka kumi na moja wamekuwa wanawasiliana (kwa siri) na baba'ngu iwapo palikuwapo na mapungufu ya pesa na ambazo mama alishindwa jazilia.
Hivi sasa na mawasiliano ya mara na baba'ngu na kiukweli ananipenda sana, nami nampenda sana. Tatizo ni kwamba
limepitishwa azimio la kwenda kupima DNA kutokana na shinikizo la ndugu wa baba, japo mwenyewe baba ananambia kiukweli naye hajiskii kufanya hilo.
Woga wangu ni kwamba majibu yakiwa ni kinyume na ninavyoyatarajia, nami sitaki kumpoteza huyu baba ambaye kwa miaka mingi nimekuwa natamani nifahamiane nae, leo hii mwenyezi mungu katukutanisha halafu majibu yawe negative, kwamba sio baba yangu? Nisaidieni wanajamii forums, nijiandae vipi kulipokea hili. Natauficha wapi uso wangu majibu yakiwa kinyume na ninavyoyatarajia, kwa maana tayari tushazoeana sana na baba'ngu.
Kwa ung'ang'anizi wangu, Mwaka jana nimefanikiwa kumshawishi mama yangu mpaka akanikutanisha na baba yangu.
Yeye Mkristo na maisha yake yote ni Tanzania Bara, sababu familia ya mama'ngu hawakutaka aibu ya familia wala mahusiano na mawasiliano yeyote na baba'ngu. Nililelewa nao na kusomeshwa mpaka umri huu, ingawa mama'ngu amekiri mbele ya baba'ngu kwamba kwa takriban miaka kumi na moja wamekuwa wanawasiliana (kwa siri) na baba'ngu iwapo palikuwapo na mapungufu ya pesa na ambazo mama alishindwa jazilia.
Hivi sasa na mawasiliano ya mara na baba'ngu na kiukweli ananipenda sana, nami nampenda sana. Tatizo ni kwamba
limepitishwa azimio la kwenda kupima DNA kutokana na shinikizo la ndugu wa baba, japo mwenyewe baba ananambia kiukweli naye hajiskii kufanya hilo.
Woga wangu ni kwamba majibu yakiwa ni kinyume na ninavyoyatarajia, nami sitaki kumpoteza huyu baba ambaye kwa miaka mingi nimekuwa natamani nifahamiane nae, leo hii mwenyezi mungu katukutanisha halafu majibu yawe negative, kwamba sio baba yangu? Nisaidieni wanajamii forums, nijiandae vipi kulipokea hili. Natauficha wapi uso wangu majibu yakiwa kinyume na ninavyoyatarajia, kwa maana tayari tushazoeana sana na baba'ngu.