Nani mwenye akili kuliko Mwl Nyerere?

Nani mwenye akili kuliko Mwl Nyerere?

huku ni kumuenzi au kumuabudu? mambo kibao alikuwa ana copy na ku paste, vitu kama katiba za taa, tanu, azimio la arusha, ujamaa wa china,muungano wenye nyufa, udini na upendeleo kwa wakatoliki, watu wanamuona wa maana sana wakati alishindwa kila kitu,mambo yote yanayotusumbua sasa chanzo ni yeye.
 
Nilitaka kukupa Like ila nikaona Haikutoshi!Katika siku zoote, Leo Naomba Kukupongeza na Kukubaliana na wewe.Kila Binadamu ana Akili, mazingira na hali za kiuchumi na kijamii ndizo hupelekea baadhi ya watu kujiona wao si kama wengine.Watu ambao bado wanaamini kuwa ni Nyerere peke yake ndo alikuwa na Akili hapa Tanganyika, wanasumbuliwa na Infiriority Complex ambayo watadumu nayo hadi kufa kwao.Ninaamini kuwa nina Akili ya kuweza Kumkosoa Binadamu awaye yeyote kama hakuwa au hayupo Sahihi.Muungano wenyewe nimejaribu kutafuta taarifa kama ulikuwa na Backup ya Wananchi Husika, kumbe hauna Backup yeyote zaidi ya Usanii wa Nyerere na Karume (though the main purpose was for Security issues).
Nadhani sasa tuungane na Malawi na Rwanda (red bolded), sijui kwa nini Uganda ilitushinda kuungana nayo? Au ni kwa ukubwa wake?
 
Alikuwa 'GENIUS' na bingwa wa kululunganya!
Kila alipolulunganya hapana dawa ila kululunganya!
Na 'watu' wakiombwa rai zao hubaki wakilulunganya zaidi!
Jamani wabongo tutumieni 'daftari la mahesabu' na hizi lulungalulunga nyingine zibaki hivyo hivyo lulungalulunga!


tumblr_m0qda9g54e1rqq7lro1_1280.jpg
 
Simba wa Afrika
attachment.php

Kapiga ki kamanda. Jamaa alikuwa great thinker. Sema tu sisi tunaojidai kumuenzi hatuchukui yale mazuri tunachukua hata Yale ya kijinga. "Kizazi chat 10 hakitapata la kujifunza kutoka Kwetu"
 
Nyerere alijitahidi sana alikua best leader kwa kizazi chake, kuhusu muungano namlahumu kushindwa kuseti uwe wa serikali moja. leo tungekuwa tunazungumza mengine kabisa
 
Hivi nyie maGreat thinkers iweje mumtegee mwanadamu mwenzenu tena marehemu awaendeshee maisha yenu?? Are you serious???

ah! kumbe na wew hamnazo!? ni kweli kila mtu ana akili lakin tunatofautiana hasa kulingana na vipawa tulivyojaliwa na Mungu lakin pia mazingira tunayokulia! Kama hutaki kuongozwa na fikra za waliomarehemu sidhan kama ungeenda shule kujifunza hata namna ya kusoma na kuandika achilia mbali kuwasoma kina PRATO, KARL MAX,n.k kwani wote hao ni MAREHEMU
 
Ningemuunga mkono mleta mada kama angesema hakuna kiongozi mwenye akili safi kama Nyerere tangu aachie uongozi hadi umauti wake.Hawa akina FAIZA FOX wanaoshinda hapa kwenye mitandao kujaribu ignore mafanikio ya Nyerere wanajisumbua bure tu ukweli utabakia pale pale siku zote kuwa hakuna kama Nyerere.At least Nyerere alikuwa na vision ya kuijenga Nchi inayojitegemea tofauti na hawa tulio nao leo ambao wameigeuza nchi yetu kuwa kama mwanamke anayejiuza kwa wanaume ili apate pesa za kuendesha maisha yake ya kila siku.Tanzania leo inadaiwa deni kubwa ambalo kulilipa kwake ni kuwauzia Wadeni wetu rasilimali za Taifa kwa bei ya kutupa na kwa masharti nafuu.Haya ndiyo mafanikio wanayojivunia akina FAIZA FOXY?Hii hoja ya kwamba kwasababu sera za kiuchumi za kijamaa zilishindwa kuleta mafanikio yaliyotarajiwa ni dhaifu kwasababu hata Wachina wenyewe waasisi wa ujamaa walishindwa na ujamaa wao.Ujamaa na biashara/uchumi ni sawa na mafuta na maji,havipatani hata kidogo.Wakati ujamaa unatilia mkazo zaidi kwenye usawa,ubepari unatilia mkazo kwenye ku-reward individuals kulingana na elimu yao,utaalamu wao na zaidi kulingana na michango yao.Sasa hiyo equality utopia ya ujamaa hivi kweli kwa mfano wewe una maarifa mazuri na ya kina juu ya fani flani kisha ulipwe mshahara sawa na yule mwenye maarifa kidogo au asiyekuwa nayo kabisa sidhani kama ideas za namna zilikubaliwa kwa moyo mmoja na wananchi wa kawaida na hii ndiyo sababu commitment katika uwajibikaji miongoni mwa wananchi haikuwa juu sana.Faida kubwa ya ujamaa wa Nyerere ni kwamba una-promote sana utu na una-discourage sana pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho yaani HAVES & HAVE NOTS.Hasara yake ni kwamba Ujamaa unazuia ushindani kwenye soko and subsequently cripple innovation & creativity as socialism encourages collectivism among the societal members which result in philosophical & ideological dogma(unchallenged thinking).Unchallenged thinking inazuia free and independent thinking hivyo kuwanyima wananchi mmoja mmoja fursa ya ku-make use of their untapped potentials they possess within hence discouraging innovation and creativity=social & economic development.
 
MI MPAKA LEO SIAMINI KAMA KUNA MWENYE AKILI NA BUSARA KAMA NYERERE
sasa busara zake zinasema hivi ......................
"Huwezi kuniua kwa nia njema, halafu useme kwamba haujaniua. Utakuwa umeniua tu. Na ukifufua serikali ya Tanganyika ni sawa na kuua Muungano, kama hamlijui hilo.
Hivyo, huwezi ukavunja Muungano halafu ukasema kwamba haukujua kama utauvunja MUUNGANO, Utakuwa umeshauvunja, na hautaweza kuurudisha tena. Msidhani mimi (Nyerere) na Karume hatukuziona serikali tatu" - Mwl. Nyerere 1993, Dodoma.

Nashangaa mbowe na magwanda ya chadema yanampinga Mwalimu nyerere kama sio laana kumpinga mzee nyerere ni nini

Miungano ya kisiasa ilishia miaka ya 1970 ulimwengu wa leo ni miungano ya kiuchumi, kwa wakati huo ilikuwa ni sahihi kabisa na hata watu wa kuhoji hawakuwepo wengi kama sasa. Ulimwengu wasasa vijana hawataki historia au mambo yafunikwefunikwe!
 
Nyerere alijitahidi sana alikua best leader kwa kizazi chake, kuhusu muungano namlahumu kushindwa kuseti uwe wa serikali moja. leo tungekuwa tunazungumza mengine kabisa

well said!..sidhan kama huu muungano ungekua wa serikal moja kungekua na maneno haya yote, nyerere alikosea sana ktk muundo wa serikal ya muungano hilo halina ubishi...
 
Wote mpo sawa maana serikali ya mtu ni kichwa chake mwenyewe ila Julius.k. Nyerere amejitahidi ila msiofikiria kwa undani ndivyo mzaniavyo kama mngekuwa nyinyi cjui mngekuwa mmetufanyia nini ?Hongera j.k.Nyerere wajukuu baadhi tunakukumbuka 1396787312511.jpg
 
Back
Top Bottom