Deejay nasmile
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 5,822
- 5,415
sasa hapo inamaana enzi hizo wapo Nyani walikuwa wanajua hesabu? si walikuwa hawana akili bado, sasa naona walivyokuwa wanabadilika wanakuwa binadamu sasa akili zikaanza kuja, walipokuwa binadamu kabisa nadhani wakagundua na Kalenda sasa...Sina hakika kama wakati mwenyezi mungu alipoumba dunia aliweka hz nchi km tanzania,malawi,kenya,marekani nk.(naamini hvo sababu hata kwenye biblia hakuna neno marekani wala tanzania)
1.swali langu je ni na aliyekuwa/waliokuwa wanagawa mipaka ya dunia mfano bara hili na lile,au nchi hii na ile?
yeye alikuwa na nguvu gani
2.kabla haijawa tanganyika eneo hili ambalo tanzania ipo lilikuwaje.waliishi nani? walitumia jina gani
3.kuanzia mwaka gani binadamu waliacha kuwa nyani(maana wanasema binadamu walikuwa manyani)
Sina hakika kama wakati mwenyezi mungu alipoumba dunia aliweka hz nchi km tanzania,malawi,kenya,marekani nk.(naamini hvo sababu hata kwenye biblia hakuna neno marekani wala tanzania)
1.swali langu je ni na aliyekuwa/waliokuwa wanagawa mipaka ya dunia mfano bara hili na lile,au nchi hii na ile?
yeye alikuwa na nguvu gani
2.kabla haijawa tanganyika eneo hili ambalo tanzania ipo lilikuwaje.waliishi nani? walitumia jina gani
3.kuanzia mwaka gani binadamu waliacha kuwa nyani(maana wanasema binadamu walikuwa manyani)
1. Dunia hii inamilikiwa na yule aliyeiumba kulingana na imani yako.
2. Kuhusu kugawa dunia, hii ilikuwa ni kazi ya Watawala waliokuwepo enzi hizo ili waweze kutawala kwa urahisi bila kuingiliana na kusababisha vita; rejea falsafa ya "Gawa Utawale" au kwa lugha ya Kiingereza "Divide and Rule" Rejea kilichofanyaka katika mkutano wa Berlin mwaka 1884 na matokeo yake
3. Kabla ya Tanganyika, eneo hili lilikuwa German Osta Afrika ikiwa na rasilimali nyingi, misitu, wanyamapori ila watu walikuwa wachache sana ambao waliishi kwa misingi ya kikabila na walikuwa tayari kupinga uvamizi kutoka mataifa mengine rejea Mkwawa, Kimweri, Mirambo, Mangi Sina na wengine wengi
4. Binadamu hajawahi kuwa nyani, binadamu ni binadamu na nyani ni nyani. Kinachotokea ni mabadilko (evolution) yanayosababishwa na harakati za binadamu katika kupambana na mazingira yake. Mabadliko haya yanatokea katika mwonekano wake na uwezo wa kufikiri na kutenda; na bado yanaendelea (angalia mwonekano wa watoto wanaozaliwa sasa hivi au linganisha picha za miaka hata ya 60 na za watu wa miaka hii). Binadamu wa zamani walikuwa na miili mikubwa kwa sababu ya aina ya kazi walizofanya, kwa sasa milili ni midogo lakini akili nyingi. Katika Tanzania, tafiti zinaonyesha kuwa binadamu walikuwepo tangu miaka milioni 3.6 iliyopita, ushahidi huo unapatikana katika Bonde la Olduvai kule Ngorongoroa ambako mnmo mwaka 1959 kuligunduliwa fuvu la binadamu aliyetwa Zinjanthropus boisei. Kabla ya ugunduzi wa moto, binadamu waliishi porini kama wanyama wakila matunda, mayai ya ndege, mizizi na nyama mbichi; wakinyweshewa na mvua na kupigwa na baridi kwa maana hiyo hata miili yao ilikuwa na manyoya kwa ajili ya kuukinga mwili na baridi. Baada ya ugunduzi wa moto, binadamu walianza kuishi pamoja kwenye mapango (mwanzo wa vijiji?) na kutokana na kuota moto, manyoya yalianza kupungua miilini mwao. Aidha, walianza kutumia moto kuchoma chakula chao. Kwa hiyo jinsi ambavyo binadamu amekuwa akijitahidi kupambana na kuboresha maisha yake amekuwa akibadilika na kuwa na sura kama hiyo yako. Ila kama ungezwaliwa miaka milini 3.6 iliyopita, hakika ungekuwa na sura mbaya ukilinganishwa na binadamu wa sasa.
Angalia aina hii ya maisha: Kuishi porini na kula chakula kibichi - kutumia zana za mawe - ugunduzi wa mto - kuishi katika mapango na kuota moto - ugunduzi wa zana za chuma - kuishi kwenye nyumba za nyasi - kuishi kwenye - nyumba za bati/ghorofa - matumizi ya teknlojia kukabili maisha; badala ya kutembea mwendo mrefu binadamua anatumia magari, ndege, simu na vingine vingi ambavyo vimefanya dunia kuwa kijiji. SASA FIKIRIA MARA MBILI KABLA HUJAANZA KUKUFURU KUWA BINADAMU ALIKUWA NYANI, HEBU JIULIZE NI KWA NINI NYANI WA SASA HAWABADILIKI KUWA BINADAMU.
Well said sawabho... Yeke waraye!
Refer kwa Wegner na Theory ya Continental Drift.
1. Dunia hii inamilikiwa na
yule aliyeiumba kulingana na imani yako.
2. Kuhusu kugawa dunia, hii ilikuwa ni kazi ya Watawala waliokuwepo enzi
hizo ili waweze kutawala kwa urahisi bila kuingiliana na kusababisha
vita; rejea falsafa ya "Gawa Utawale" au kwa lugha ya Kiingereza "Divide
and Rule" Rejea kilichofanyaka katika mkutano wa Berlin mwaka 1884 na
matokeo yake
3. Kabla ya Tanganyika, eneo hili lilikuwa German Osta Afrika ikiwa na
rasilimali nyingi, misitu, wanyamapori ila watu walikuwa wachache sana
ambao waliishi kwa misingi ya kikabila na walikuwa tayari kupinga
uvamizi kutoka mataifa mengine rejea Mkwawa, Kimweri, Mirambo, Mangi
Sina na wengine wengi
4. Binadamu hajawahi kuwa nyani, binadamu ni binadamu na nyani ni nyani.
Kinachotokea ni mabadilko (evolution) yanayosababishwa na
harakati za binadamu katika kupambana na mazingira yake. Mabadliko haya
yanatokea katika mwonekano wake na uwezo wa kufikiri na kutenda; na bado
yanaendelea (angalia mwonekano wa watoto wanaozaliwa sasa hivi au
linganisha picha za miaka hata ya 60 na za watu wa miaka hii). Binadamu
wa zamani walikuwa na miili mikubwa kwa sababu ya aina ya kazi
walizofanya, kwa sasa milili ni midogo lakini akili nyingi. Katika
Tanzania, tafiti zinaonyesha kuwa binadamu walikuwepo tangu miaka
milioni 3.6 iliyopita, ushahidi huo unapatikana katika Bonde la Olduvai
kule Ngorongoroa ambako mnmo mwaka 1959 kuligunduliwa fuvu la binadamu
aliyetwa Zinjanthropus boisei. Kabla ya ugunduzi wa moto, binadamu
waliishi porini kama wanyama wakila matunda, mayai ya ndege, mizizi na
nyama mbichi; wakinyweshewa na mvua na kupigwa na baridi kwa maana hiyo
hata miili yao ilikuwa na manyoya kwa ajili ya kuukinga mwili na baridi.
Baada ya ugunduzi wa moto, binadamu walianza kuishi pamoja kwenye
mapango (mwanzo wa vijiji?) na kutokana na kuota moto, manyoya
yalianza kupungua miilini mwao. Aidha, walianza kutumia moto kuchoma
chakula chao. Kwa hiyo jinsi ambavyo binadamu amekuwa akijitahidi
kupambana na kuboresha maisha yake amekuwa akibadilika na kuwa na sura
kama hiyo yako. Ila kama ungezwaliwa miaka milini 3.6 iliyopita, hakika
ungekuwa na sura mbaya ukilinganishwa na binadamu wa sasa.
Angalia aina hii ya maisha: Kuishi porini na kula chakula kibichi -
kutumia zana za mawe - ugunduzi wa mto - kuishi katika mapango na kuota
moto - ugunduzi wa zana za chuma - kuishi kwenye nyumba za nyasi -
kuishi kwenye - nyumba za bati/ghorofa - matumizi ya teknlojia kukabili
maisha; badala ya kutembea mwendo mrefu binadamua anatumia magari,
ndege, simu na vingine vingi ambavyo vimefanya dunia kuwa kijiji.
SASA FIKIRIA MARA MBILI KABLA HUJAANZA KUKUFURU KUWA BINADAMU ALIKUWA
NYANI, HEBU JIULIZE NI KWA NINI NYANI WA SASA HAWABADILIKI KUWA
BINADAMU.
Afu unajua watu kumbe Darwin's theory of evolution hamuielewi, maana kila siku watu wanachanganya kua Darwin alisema tulitoka kwenye nyani.. hako na kale ka-kipengele unapewa juu juu hata ukweli hujausoma.. Real theory inachosema sio kwamba tulikua nyani, inasema sisi pamoja na nyani tulitoka kwa ancestor sawa, sio kwamba ancestor wetu alikua nyani... Na hiyo sense wanayotumia scientists ni kwamba miili yetu na yani tunafanana kwa 94% kumfanya yeye kua mnyama ambaye tuko nae karibu sana kuliko wanyama wengine..
Tutatukana bure weye dada/mdogo wangu, lugha za watu hizo. Tusalimiane tu kwa lugha ya Taifa, habari za asubuhi Mrembo. Kama nawe ni wa huko, karibu chemba -pm.
Afu unajua watu kumbe Darwin's theory of evolution hamuielewi, maana kila siku watu wanachanganya kua Darwin alisema tulitoka kwenye nyani.. hako na kale ka-kipengele unapewa juu juu hata ukweli hujausoma.. Real theory inachosema sio kwamba tulikua nyani, inasema sisi pamoja na nyani tulitoka kwa ancestor sawa, sio kwamba ancestor wetu alikua nyani... Na hiyo sense wanayotumia scientists ni kwamba miili yetu na yani tunafanana kwa 94% kumfanya yeye kua mnyama ambaye tuko nae karibu sana kuliko wanyama wengine..
nakubaliana na maelezo yako kwa maana hiyo miaka ijayo dunia inaweza kuja kuishi binadamu wa aina nyingine tofauti siyo
Mkuu hilo jina linatoka kuleeee......... Ndio maana nikakusalimia hivo! Samahani kama sio wa kuleeeee!!!!!!
Binfsi siamini,na sito kaa niamini binadamu alikuwa nyani huyo nyani akajabadilka kuwa binadamu kulingana na vipindi,kwangu big NO.
Mungu alimwumba,Binadamu,kisha viumbe ili binadamu avitawale vyoote vilivyomo.
Hiyo historia waliyoiandika wazungu,ni kutaka kutuchafua na kutudhalilisha watu weusi,ili ionekane ss tulikuwa manyani,washenzi sana watu hawa.
Kwaku walieza kuona nyani waa Afrika ni weusi basi ikawa ndo chimbko la mwafrika kuwa alitokana na nyani,
Katika historia mabara (continent)yalikuwa yameunga kabisa kama kijiji lkn kutokana na climatical change mf.Tetemeko la ardh ndipo iliweza kuyagawa mabara,Hata ukiangalia vizuri atlasi unaweza ukaifanya kama mchezo wa puzzle na ukaiunga ki akili tuu bila ubishi.
Baada ya mabala kugawanyika ndipo wengne tukawa katika Kanda(tropical) tofauti tofauti,Ikiwepo yenye baridi,Joto,mvua,ukame,jangwa na Kadhalika.Hio ikapelekea kuwa ngozi na nywele tofauti tofauti kulingana na Kanda.
Kuhusu kugawa nchi,hizi mipaka na majina ni sisi tu binadamu ndo tulifanza hivyo.
Pia naona kuna haja ya historia kuandikwa upya kabisa na wanafunzi wafundishwe iliyo andikwa na waafrika wenyewe.
Haina shida Mkuu, lakini mimi sio wa huko nilifanya kazi North Mara, ndo nikapata jina hilo baada ya kuckia linatajwa tajwa.