kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,745
Tamko la kamanda wa Polisi
Askari hawa walikuwa katika doria ya kawaida, walimkamata mwenye bodaboda na alikuwa anagoma kutii amri na wakati wanabishana alitoa kisu ndipo askari huyo akampiga risasi, alisema kamanda huyo.
Hata hivyo, alisema kituo hakikuteketea chote, na kwamba hata nyaraka zilizoungua ni chache.
Tamko la Mashuhuda Wananchi
Awali, ilielezwa na mashuhuda kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni kuwa polisi walifika katika Kijiji cha Mugoma kwa lengo la kukagua pikipiki mbovu na zisizokuwa na usajili na walifika katika gereji moja na kukuta mmiliki wa gereji hiyo akitengeneza pikipiki, kumtaka aipeleke kituoni kwa maelezo kuwa ilikuwa mbovu.
Baada ya hapo, fundi aligoma kutekeleza agizo hilo na polisi mmoja alimpiga risasi, kitendo ambacho kiliamsha hasira kwa wananchi waliokuwa jirani na eneo hilo.
Ilielezwa na mashuhuda kuwa baada ya tukio polisi aliyefyatua risasi alikimbilia kujificha katika nyumba iliyopo jirani na gereji hiyo, huku akimuacha mwenzake.
Wananchi walimvamia yule askari aliyebaki pale gereji na kuanza kumcharanga kwa mapanga na kumpiga mawe hadi akafa, alisema mmoja wa mashuhuda.
Alifafanua kwamba baada ya kuhakikisha kuwa wamemuua, wananchi hao walikwenda katika nyumba aliyojificha askari aliyekimbia, kutaka kuichoma moto iwapo angegoma kutoka.
Mmiliki wa nyumba ile baada ya kuona wananchi hao wanataka kuichoma moto nyumba yake alimtaka askari huyo kutoka nje, alipotoka tu wananchi walimvamia na kuanza kumpiga mawe na kumuua, alisema.
Kituo cha polisi kilichoteketezwa kwa moto, kipo karibu na mpaka wa Tanzania na Burundi.
My Take!
Hivi inapoteza heshima ipi iwapo hawa viongozi wetu wa Polisi watakuwa wakweli? Kauli yake hii inataka kuaminisha umma kwamba huyu raia aliyeuawa alitaka kuwadhuru Polisi ndo wakachukua hatua ya Kumuua
CHANZO GAZETI LA MWANANCHI
Askari hawa walikuwa katika doria ya kawaida, walimkamata mwenye bodaboda na alikuwa anagoma kutii amri na wakati wanabishana alitoa kisu ndipo askari huyo akampiga risasi, alisema kamanda huyo.
Hata hivyo, alisema kituo hakikuteketea chote, na kwamba hata nyaraka zilizoungua ni chache.
Tamko la Mashuhuda Wananchi
Awali, ilielezwa na mashuhuda kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni kuwa polisi walifika katika Kijiji cha Mugoma kwa lengo la kukagua pikipiki mbovu na zisizokuwa na usajili na walifika katika gereji moja na kukuta mmiliki wa gereji hiyo akitengeneza pikipiki, kumtaka aipeleke kituoni kwa maelezo kuwa ilikuwa mbovu.
Baada ya hapo, fundi aligoma kutekeleza agizo hilo na polisi mmoja alimpiga risasi, kitendo ambacho kiliamsha hasira kwa wananchi waliokuwa jirani na eneo hilo.
Ilielezwa na mashuhuda kuwa baada ya tukio polisi aliyefyatua risasi alikimbilia kujificha katika nyumba iliyopo jirani na gereji hiyo, huku akimuacha mwenzake.
Wananchi walimvamia yule askari aliyebaki pale gereji na kuanza kumcharanga kwa mapanga na kumpiga mawe hadi akafa, alisema mmoja wa mashuhuda.
Alifafanua kwamba baada ya kuhakikisha kuwa wamemuua, wananchi hao walikwenda katika nyumba aliyojificha askari aliyekimbia, kutaka kuichoma moto iwapo angegoma kutoka.
Mmiliki wa nyumba ile baada ya kuona wananchi hao wanataka kuichoma moto nyumba yake alimtaka askari huyo kutoka nje, alipotoka tu wananchi walimvamia na kuanza kumpiga mawe na kumuua, alisema.
Kituo cha polisi kilichoteketezwa kwa moto, kipo karibu na mpaka wa Tanzania na Burundi.
My Take!
Hivi inapoteza heshima ipi iwapo hawa viongozi wetu wa Polisi watakuwa wakweli? Kauli yake hii inataka kuaminisha umma kwamba huyu raia aliyeuawa alitaka kuwadhuru Polisi ndo wakachukua hatua ya Kumuua
CHANZO GAZETI LA MWANANCHI