Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,355
- 2,739
Tayari kitu chenye ncha kali kimefanya kazi
Hatuwezi kuupata ukweli kama kila mtu atakuja na uchunguzi kama wa kwako: Polisi maelezo yao mistari miwili na ya wananchi mengi kama ulivyofanya. Unatoa hoja na mwisho una conlude - polisi ni waongo..! Nadhani tutaupata ukweli pakiwepo na kitu huru cha kuchunguza na kuelezea tukio hili bila ya kuegemea upande wowote.
Serikali hii haiwezi kuwa upande wa Raia. Je gereji hupelekwa kitu kizima au kibovu?
Hiki ni nini?Mkuu Police ni kiboko kwa ku{c}ingizia.. Mie nina mfano hai kabisa.. Walikamatwa jirani zangu wawili ndani kwao katika operation ya kumtafuta mwizi.. Walitonywa kuwa huyo wanaemtafuta analala humo.. Walipoenda hawakumkuta mtu wao wakaamua kuwakamata hao jirani wawili.. Baadae katika kuwapiga na kuwalazimisha kusema wakamvunja mmoja mguu kwenye goti.. Ndugu zake huyo alievunjwa goti wakaja juu.. Kilichotokea ni kupewa ke{c}i ya uvunjaji wa kutumia nguvu na kwamba walikamatwa kwenye eneo la tukio la ujambazi..! Huwezi kuamini walikaa ndani miezi sita na ke{c}i ikaisha kwa gharama kubwa sana..! Hiyo ilitosha kunipa sababu ya kutowaamini Police maisha yangu yote..
Niki{c}ikia jambazi au majambazi yameuawa katika "majibishano" ya risasi na Police nina{c}ikitika kwa kuwa ninaamini hao waliouawa {c}iyo majambazi.. Ila wameuawa na majambazi walio na magwanda..
hakuna ubishi askari wameuwawa kinyama na askari wameua raia,cha msingi ni kusubiri tume ije ichunguze na kutoa mapendekezo na maoni kuhusiana na jinsi ya kushughulikia matukio ya aina hiyo yasitokee tena.pia katika matukio ya namna hiyo wapo baadhi ya watu wameona tukio zima na wapo tayari kutoa ushahidi.swala la nani anauwezo wa kuwasiliana na marehemu siyo issue,mbona usia wa marehemu unakubalika akisha kufa kama ushahidi sembuse madai ya mtu kutolewa kisu?.kama tunaweza kukubali usiwa wa marehemu kwanini tusikubali mambo mengine?.kama unaushahidi peleka ktk tume iliyoundwa usaidie,kama huwezi kufikisha ujumbe/ushahidi wako basi ukubaliane na majibu ya tume.
POlis wanaingia ktk mtihani mwingine, mwema asipotumia akili na kujiandaa fidia wafiwa ,huku akitakiwa wapa memo polisi upesi wajifunze kuwa na adabu na wasitegemee tena ulinzi wa kijinga wa jeshi la polisi kwa uongo, atapelekea polisi wengi zaidi kuuwawa, na hao watu wa huo ukanda bado wana kumbukumbu za vita.Ujinga wa polisi unaweza kuw ani mwanzo wa vita full ambayo polisi hawata iweza. Mbaya hii habari imeshafungua vichwa vya raia, polisi watapigia simu ili wakauwawe, watauwawa uraiani.Watauwawa ktk guest house, watauwawa ktk pombe na madisco.Mwema aache usanii kwa issue very serious kama hii, ni matukio amabyo jeshi la polisi walipaswa omba yasitokee.Kwani majibu yoyote yatakayotoka bado raia wameshajifunza kitu, hakuta tofauti na kumwonyesha mtoto picture ya ngono, hatoacha itafuta kuitazama hata kama utamwambia ni mbaya.Huyu RPC ni kiboko, amejuaje hayo ya kutoleana visu na kupigana risasi wakati wahusika wote wawili wamefariki? Au yeye ni kigagula na anaweza kuwasiliana na marehemu? mwaka huu tu unakwisha huku tukiendelea kushuhudia killa aina ya sinema kutoka policcm.
Tamko la kamanda wa
Polisi
Askari hawa walikuwa katika doria ya kawaida, walimkamata mwenye
bodaboda na alikuwa anagoma kutii amri na wakati wanabishana
alitoa kisu ndipo askari huyo akampiga
risasi, alisema kamanda huyo.
Hata hivyo, alisema kituo hakikuteketea chote, na kwamba hata nyaraka
zilizoungua ni chache.
Tamko la Mashuhuda Wananchi
Awali, ilielezwa na mashuhuda kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni kuwa
polisi walifika katika Kijiji cha Mugoma kwa lengo la kukagua pikipiki
mbovu na zisizokuwa na usajili na walifika katika gereji moja na kukuta
mmiliki wa gereji hiyo akitengeneza pikipiki, kumtaka aipeleke kituoni
kwa maelezo kuwa ilikuwa mbovu.
Baada ya hapo, fundi aligoma kutekeleza agizo hilo na polisi mmoja
alimpiga risasi, kitendo ambacho kiliamsha hasira kwa wananchi waliokuwa
jirani na eneo hilo.
Ilielezwa na mashuhuda kuwa baada ya tukio polisi aliyefyatua risasi
alikimbilia kujificha katika nyumba iliyopo jirani na gereji hiyo, huku
akimuacha mwenzake.
Wananchi walimvamia yule askari aliyebaki pale gereji na kuanza
kumcharanga kwa mapanga na kumpiga mawe hadi akafa, alisema mmoja wa
mashuhuda.
Alifafanua kwamba baada ya kuhakikisha kuwa wamemuua, wananchi hao
walikwenda katika nyumba aliyojificha askari aliyekimbia, kutaka
kuichoma moto iwapo angegoma kutoka.
Mmiliki wa nyumba ile baada ya kuona wananchi hao wanataka kuichoma
moto nyumba yake alimtaka askari huyo kutoka nje, alipotoka tu wananchi
walimvamia na kuanza kumpiga mawe na kumuua, alisema.
Kituo cha polisi kilichoteketezwa kwa moto, kipo karibu na mpaka wa
Tanzania na Burundi.
My Take!
Hivi inapoteza heshima ipi iwapo hawa viongozi wetu wa Polisi watakuwa
wakweli? Kauli yake hii inataka kuaminisha umma kwamba huyu raia
aliyeuawa alitaka kuwadhuru Polisi ndo wakachukua hatua ya Kumuua
CHANZO GAZETI LA MWANANCHI
kwa hiyo unataka kuniambia kwamba tanzania hamna uwezekano wa kupata taarifa sahihi juu ya mambo?Taarifa zipi ambazo utazipata katika nchi hii zilizotafitiwa kitaalam ndugu? Ya Ulimboka, Ally Zona(Moro) Mwangosi, Taarifa zake unazo? na umeziamini? je kama uziamini unategemea taarifa za kitaalam zitoke wapi.
Hiki ni nini?
Je c ni sawa na s, naogopa kukwambia urudi darasa la kwanza.
Tamko la kamanda wa Polisi
Askari hawa walikuwa katika doria ya kawaida, walimkamata mwenye bodaboda na alikuwa anagoma kutii amri na wakati wanabishana alitoa kisu ndipo askari huyo akampiga risasi, alisema kamanda huyo.
Hata hivyo, alisema kituo hakikuteketea chote, na kwamba hata nyaraka zilizoungua ni chache.
Tamko la Mashuhuda Wananchi
Awali, ilielezwa na mashuhuda kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni kuwa polisi walifika katika Kijiji cha Mugoma kwa lengo la kukagua pikipiki mbovu na zisizokuwa na usajili na walifika katika gereji moja na kukuta mmiliki wa gereji hiyo akitengeneza pikipiki, kumtaka aipeleke kituoni kwa maelezo kuwa ilikuwa mbovu.
Baada ya hapo, fundi aligoma kutekeleza agizo hilo na polisi mmoja alimpiga risasi, kitendo ambacho kiliamsha hasira kwa wananchi waliokuwa jirani na eneo hilo.
Ilielezwa na mashuhuda kuwa baada ya tukio polisi aliyefyatua risasi alikimbilia kujificha katika nyumba iliyopo jirani na gereji hiyo, huku akimuacha mwenzake.
Wananchi walimvamia yule askari aliyebaki pale gereji na kuanza kumcharanga kwa mapanga na kumpiga mawe hadi akafa, alisema mmoja wa mashuhuda.
Alifafanua kwamba baada ya kuhakikisha kuwa wamemuua, wananchi hao walikwenda katika nyumba aliyojificha askari aliyekimbia, kutaka kuichoma moto iwapo angegoma kutoka.
Mmiliki wa nyumba ile baada ya kuona wananchi hao wanataka kuichoma moto nyumba yake alimtaka askari huyo kutoka nje, alipotoka tu wananchi walimvamia na kuanza kumpiga mawe na kumuua, alisema.
Kituo cha polisi kilichoteketezwa kwa moto, kipo karibu na mpaka wa Tanzania na Burundi.
My Take!
Hivi inapoteza heshima ipi iwapo hawa viongozi wetu wa Polisi watakuwa wakweli? Kauli yake hii inataka kuaminisha umma kwamba huyu raia aliyeuawa alitaka kuwadhuru Polisi ndo wakachukua hatua ya Kumuua
CHANZO GAZETI LA MWANANCHI