Fred Mwakitundu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 227
- 383
Askofu Gwajima na Usukuma
Askofu Shoo na Uchagga
Tarehe 3.3.2020 Viongozi wa dini wawili hapa nchini wamekata mawimbi ya anga kwa jambo linalofanana.
Askofu Gwajima wa Kanisa la ufufuo na uzima lililopo Dar es salaam, alihojiwa na polisi kwa kusambaza vipeperushi vyenye lugha ya kisukuma akiwahamasisha wajitambue na kusaidiana, alitumia picha ya Mhe.Rais ili kuwahamasisha waungane na kuunda chombo madhubuti.
Huko Moshi Mkoani Kilimanjaro tarehe 3.3.2020 Askofu Shoo wa KKKT alikutana na wachungaji wake wapatao 200 na kuwaambia serikali ya awamu ya tano na baadhi ya maaskofu wanawaonea wivu wachagga .
Akasema wachagga wamefanikiwa sana kusababisha waonewe wivu au kuonewa na akawataka waungane na kusaidiana na kulinda Dayosisi yao, bahati mbaya Askofu Shoo hajahojiwa na polisi kama Gwajima.
Kuwabagua wachagga au wasukuma ni kosa kubwa, lakini na wao kujibagua na kujiona bora kuliko makabila mengine ni kosa kubwa zaidi.
Watanzania tujiulize nani kafufua ukabila tena nchini mwetu?
Askofu Shoo na Uchagga
Tarehe 3.3.2020 Viongozi wa dini wawili hapa nchini wamekata mawimbi ya anga kwa jambo linalofanana.
Askofu Gwajima wa Kanisa la ufufuo na uzima lililopo Dar es salaam, alihojiwa na polisi kwa kusambaza vipeperushi vyenye lugha ya kisukuma akiwahamasisha wajitambue na kusaidiana, alitumia picha ya Mhe.Rais ili kuwahamasisha waungane na kuunda chombo madhubuti.
Huko Moshi Mkoani Kilimanjaro tarehe 3.3.2020 Askofu Shoo wa KKKT alikutana na wachungaji wake wapatao 200 na kuwaambia serikali ya awamu ya tano na baadhi ya maaskofu wanawaonea wivu wachagga .
Akasema wachagga wamefanikiwa sana kusababisha waonewe wivu au kuonewa na akawataka waungane na kusaidiana na kulinda Dayosisi yao, bahati mbaya Askofu Shoo hajahojiwa na polisi kama Gwajima.
Kuwabagua wachagga au wasukuma ni kosa kubwa, lakini na wao kujibagua na kujiona bora kuliko makabila mengine ni kosa kubwa zaidi.
Watanzania tujiulize nani kafufua ukabila tena nchini mwetu?