Mtende
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 6,385
- 7,335
Uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliotangazwa leo na Waziri Mkuu Pinda kwa mara nyingine unaturejesha kwenye swali ambalo huulizwa na watu wengi,kwamba ni NANI HAO WALIO WASHAURI WA RAIS KIKWETE?
Inawezekanaje Rais wa nchi akose umakini mkubwa kiasi hiki hata amteue Paul Makonda kuwa Mkuu wa Wilaya?Kwa kauli na mwenendo,Paul Makonda anakosa sifa na uadilifu wa kuwa mteule wa Rais;hana uadilifu wa kukalia ofisi yoyote ya umma aghalabu ofisi ya DC. Hana tofauti na Mrisho Gambo aliyeondolewa,hawa ni vijana wenye majivuno na walevi wa madaraka.Ndivyo alivyo pia Nape Nnauye...lakini hawa eti ndo JK anaona ni watu wenye sifa za kuwa wateule wa Rais?hakika hawa wana sifa za kuwa wateule wa Kikwete,hawana sifa za kuwa wateule wa Rais wa nchi.
Mungu atusaidie hii miezi 7 iliyobaki iishe haraka.
si mwingine bali ni yule mwalimu wa upe mama salma kikwete