Salaam kwenu wana JF. Kuna hili shirikisho la michezo la wizara kwa kifupi SHIMIWI ambayo mashindano ya michezo kutoka katika wizara mbalimbali za serikali yanategemea kufunguliwa rasmi hapo kesho mjini Morogoro mgeni rasmi akiwa Waziri wa habari utamaduni na michezo. Chakushangaza sana, 98% ya washiriki wa mashindano hayo ni watumishi wakada ya chini wakiwemo wahudumu wa ofisi, messengers, madreva, walinzi na vibarua wa muda mfupi. Nijuavyo mimi, kushiriki michezo ni moja wapo ya kuuweka mwili wako fit na kukwepa matatizo mbali mbali hasa ya kiafya. Sasa kwa nini washiriki wa kada ya juu wakiwemo mawaziri, wakurugenzi na makamishina wasishiriki hata kama ni michezo michache tu? Ingekuwa ni USA tungetegemea watu wazito kama hao angalau wachache wao wakishiriki. Nasikia hata hao 2% ya washiriki waliokanyaga vidato baadhi ya Wizara kama vile mambo ya ndani na nyinginezo wanawalipa posho ya chini yaani 45,000/= sawa na ya hilo kundi la kwanza kama vile wasomi hawatakiwi kushiriki na wakishiriki wajishushe vidato. Sababu waliyopewa na viongozi ni eti pesa hazitoshi na wanaweka akiba kwa ajili ya michezo ya Mei Mosi. Kwangu mimi hii haiingii akilini kabisa. Kama kuna kuna mwana JF mwenye uelewa wa SHIMIWI please, nieleweshe!!