Salam wanajukwaa!
Sisi wengine tuko vijijini, hivyo, tunaishia kusikia sikia tu kutoka kwenu 'maborn town'.
Tunasikia kuwa eti wao ndio waliomtoa shujaa na kumuweka Masiah wa Fey toto.
Kwamba wao ndio wanateua kuanzia Cabinet members hadi maCEO.
Kwamba wao ndio wako nyuma ya mikataba yote mikubwa.
Kwa ufupi wao ndio huassamble parts zote za chapa hii ya TV, na hata zipatapo hitilafu, ni kiwanda cha pale pale msoga ndio huweka spare parts zingine. Inadaiwa remote wao ndio hubaki nayo, na hupendelea TV ikae Dar kwani ni karibu zaidi kwa remote kufanya kazi na haihitaji dish bali Antena tu kuliko Dodoma.
Shida haya yamekaa kizushi tu. Ushahidi uko wapi? Msoga wanasemwa lakini ushahidi sifuri! Hebu nyie 'maborn town' mtusaidie sisi 'mabush star' ili tupate elewa ukweli wa haya maneno..