Ndugu Watanzania wenzangu, kwa takribani miaka kumi sasa tumeshuhudia vyama vya upinzani hususani CHADEMA wakitumia muda wao mwingi na rasilimali nyingi kupambana na ufisadi hapa nchini Tanzania.
Wamezunguka nchi nzima wakiwahubiri watu juu ya adhma yao hiyo nzuri ya kupambana na mafisadi.
Wametumia kila aina ya operation na mikutano kuwaaminisha Watanzania kuwa wao na ufisadi ni sawa na paka na panya. Bungeni wamekuwa vinara wakufichua mafisadi na hata kushinikiza wawajibishwe.
Wamekuwa na ujasiri mpaka wakuwataja baadhi ya mafisadi papa hapa nchini (rejea list of shame2007 by Dr. Slaa).
Edward Ngoyaye Lowassa ni miongoni mwa Watanzania waliokuwa wakitajwa kwa kina na upana sana na upinzani kama nguli wa ufisadi nchini Tanzania (rejea mikutano mbalimbali ya chadema). Wakathubutu kusema kuwa hakupaswa kuwa uraiani saizi bali jela au amenyongwa kabsa. Wakailaumu serikali kuwa inalinda wezi na mafisadi.
Watanzania tukawaamini Chadema, tukaamini kuwa Chadema wana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi, tukawashangilia kila kona, tukaamini kuwa watatuletea mabadiliko, mabadiliko yaliyoshindwa kuletwa na CCM.
Katika harakati zote hizi, Chadema walikuwa pamoja, viongozi wote mpaka na wanachama, wakipinga ufisadi na udhalimu wa CCM.
Leo wamebadilika, yule mtu waliyekuwa wakimsema na kumtaja kwa kina na upana kabsa kuwa fisadi nguli na hatari Tanzania wamemkarbisha kwenye chama chao, tena akiwa na siku mbili tu wakampa nafasi ya kugombea urais, tena bila kupingwa, pasipo hata kumchunguza. "Samaki na ndege leo wameoana sijui wataishi wapi". Sasa nauliza swali...
NANI ANAFAA KUSHIKA DODOKI KUMSAFISHA LOWASSA CHADEMA WATANZANIA WAELEWE?
BY
SOLOMON
Wamezunguka nchi nzima wakiwahubiri watu juu ya adhma yao hiyo nzuri ya kupambana na mafisadi.
Wametumia kila aina ya operation na mikutano kuwaaminisha Watanzania kuwa wao na ufisadi ni sawa na paka na panya. Bungeni wamekuwa vinara wakufichua mafisadi na hata kushinikiza wawajibishwe.
Wamekuwa na ujasiri mpaka wakuwataja baadhi ya mafisadi papa hapa nchini (rejea list of shame2007 by Dr. Slaa).
Edward Ngoyaye Lowassa ni miongoni mwa Watanzania waliokuwa wakitajwa kwa kina na upana sana na upinzani kama nguli wa ufisadi nchini Tanzania (rejea mikutano mbalimbali ya chadema). Wakathubutu kusema kuwa hakupaswa kuwa uraiani saizi bali jela au amenyongwa kabsa. Wakailaumu serikali kuwa inalinda wezi na mafisadi.
Watanzania tukawaamini Chadema, tukaamini kuwa Chadema wana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi, tukawashangilia kila kona, tukaamini kuwa watatuletea mabadiliko, mabadiliko yaliyoshindwa kuletwa na CCM.
Katika harakati zote hizi, Chadema walikuwa pamoja, viongozi wote mpaka na wanachama, wakipinga ufisadi na udhalimu wa CCM.
Leo wamebadilika, yule mtu waliyekuwa wakimsema na kumtaja kwa kina na upana kabsa kuwa fisadi nguli na hatari Tanzania wamemkarbisha kwenye chama chao, tena akiwa na siku mbili tu wakampa nafasi ya kugombea urais, tena bila kupingwa, pasipo hata kumchunguza. "Samaki na ndege leo wameoana sijui wataishi wapi". Sasa nauliza swali...
NANI ANAFAA KUSHIKA DODOKI KUMSAFISHA LOWASSA CHADEMA WATANZANIA WAELEWE?
BY
SOLOMON