Nani ana afadhali?

Nani ana afadhali?

kakuruvi

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2009
Posts
770
Reaction score
259
Mwisho wa wiki iliyopita nilisafiri nje ya Dar na kwenda vijijini huko Korogwe, kuna mahali tulifika nikajisikia kula muwa. Basi tulisimama barabarani karibu na daraja moja la mto Rwengela kwenye mashamba ya mkonge Magoma Estate.

Wakaja vijana tukawaagiza miwa kwani hapo ndio mashambani kwao, waliporudi walionekana kwenye malumbano fulani, hatukujua mpaka tulipowauliza kulikoni? Kumbe walipoondoka walijihisi haja kubwa wote kwa pamoja, mmoja akajisaidia mtoni, mwengine pembeni ya mto.

Ubishi ulikuwa, mmoja anamlaumu mwenzake kwa kujisaidia pembeni ya mto kwani atawatesa wote watakaopita pale kwa harufu ya kinyesi, mwingine anamlaumu mwenzake kwa kujisaidia mtoni kwa kuwa atawalisha uchafu wote wanaotegemea maji ya mto huo huko kote utakakopita.

Wana JF tuambie madhara yatakayosababishwa na mazingira ya uchafu wa kila mmoja, nani ana afadhali kati ya hawa wawili?
 
MMMH na hiyo miwa mkala kweli?

Kama ulikuwepo aliyekula ni mimi tu kwa kutegemea kisu kikali si unajua tena ganda la muwa. ila hatukuendelea kusimama tena hapo tuliendelea na safari.
 
Mwisho wa wiki iliyopita nilisafiri nje ya Dar na kwenda vijijini huko Korogwe, kuna mahali tulifika nikajisikia kula muwa. Basi tulisimama barabarani karibu na daraja moja la mto Rwengela kwenye mashamba ya mkonge Magoma Estate.

Wakaja vijana tukawaagiza miwa kwani hapo ndio mashambani kwao, waliporudi walionekana kwenye malumbano fulani, hatukujua mpaka tulipowauliza kulikoni? Kumbe walipoondoka walijihisi haja kubwa wote kwa pamoja, mmoja akajisaidia mtoni, mwengine pembeni ya mto.

Ubishi ulikuwa, mmoja anamlaumu mwenzake kwa kujisaidia pembeni ya mto kwani atawatesa wote watakaopita pale kwa harufu ya kinyesi, mwingine anamlaumu mwenzake kwa kujisaidia mtoni kwa kuwa atawalisha uchafu wote wanaotegemea maji ya mto huo huko kote utakakopita.

Wana JF tuambie madhara yatakayosababishwa na mazingira ya uchafu wa kila mmoja, nani ana afadhali kati ya hawa wawili?


Hapo hakuna mwenye afadhali... ila hicho sio kinachoniogopesha .... NINACHOKUWA NA WASIWASI NACHO ni JE na nyie mlikula hiyo MIWA?..... maana naona hapo na wewe inabidi ujiweke kundi moja la wasioajali afya kama ulikuwa hiyo miwa
 
Waliojisaidia hovyo na wewe uliyekula miwa ya waliojisaidia hovyo wote hali moja kanuni za kiafya zinasemaje yaani kisa mlimmenya kwa kisu kikali tu ndo mjustify violation yenu ya kanuni za afya. Hapo ngoma droo wote sawa tu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom