Rose Mayemba
JF-Expert Member
- May 7, 2012
- 721
- 1,017
Tangu Tanzania iingie kwenye ushindani mkubwa katika siasa hasa kwa vyama hivi viwili( CHADEMA & CCM), watanzania wengi wasio na hatia wamepoteza uhai wao na wengine kupoteza viungo vyao( tukiacha wakati wa CUF na NCCR mageuzi).
Nawakumbuka akina Dr ulimboka, Daudi Mwangosi, Said kubenea, mauaji ya Arusha( tarehe 5/01/2011 na yale yaliyotokea hivi karibuni). Serikali yetu tukufu iliunda tume kufuatilia vitendo hivyo vya kinyama na kikatili ili baadae ije na majibu ya kuwaridhisha watanzania, si hivyo tu bali tujue muafaka wa wahusika wa vitendo hivyo viovu(nasikitika mpaka leo hakuna kunachoendelea)
Kinachonishangaza ni kwamba serikali yetu kupitia chama chake imesema inawafahamu wahusika wa matukio hayo yote na imewatangaza hadharani wahujumu hao wa maisha ya watu lakini hakuna hatua zozote za makusudi zinazochukuliwa juu yao. CHADEMA ni watuhumiwa namba moja wa mauaji na ukatili huu unaoendelea dhidi ya watu hawa.
Kwanini inatumia pesa nyingi kuunda tume kuchunguza matukio haya ilihali wahusika wanawafahamu? . Ama kwanini haijawakamata wanaodai CDM ndo wahusika ili wakasaidie kutoa ushahidi mahakamani? Je huku si kushindwa kuongoza kwa watawala?. Na mbona haijawahi kuleta majibu ya tume hizo tangu zimeanza kuundwa zaidi ya kuwahadaa watanzania?
Kwanini tusiamini kama matukio haya yanafanywa na wao wenyewe huku wakiisingizia chadema?. tumechoka kufungwa macho huku watanzania tuwekwe wazi tujue.
Kama serikali yetu ambayo ndiyo yenye dhamana ya kulinda haki za binadamu imekalia kimya unyama huu nani alaumiwe?.Ni waliofanya vitendo hivyo au wale waliowaacha huru ili waendelee kuyafanya haya?
TUMECHOKA KUONA DAMU ZA NDUGU ZETU ZIKIMWAGIKA...WATANZANIA TUNATAKA AMANI
Nawakumbuka akina Dr ulimboka, Daudi Mwangosi, Said kubenea, mauaji ya Arusha( tarehe 5/01/2011 na yale yaliyotokea hivi karibuni). Serikali yetu tukufu iliunda tume kufuatilia vitendo hivyo vya kinyama na kikatili ili baadae ije na majibu ya kuwaridhisha watanzania, si hivyo tu bali tujue muafaka wa wahusika wa vitendo hivyo viovu(nasikitika mpaka leo hakuna kunachoendelea)
Kinachonishangaza ni kwamba serikali yetu kupitia chama chake imesema inawafahamu wahusika wa matukio hayo yote na imewatangaza hadharani wahujumu hao wa maisha ya watu lakini hakuna hatua zozote za makusudi zinazochukuliwa juu yao. CHADEMA ni watuhumiwa namba moja wa mauaji na ukatili huu unaoendelea dhidi ya watu hawa.
Kwanini inatumia pesa nyingi kuunda tume kuchunguza matukio haya ilihali wahusika wanawafahamu? . Ama kwanini haijawakamata wanaodai CDM ndo wahusika ili wakasaidie kutoa ushahidi mahakamani? Je huku si kushindwa kuongoza kwa watawala?. Na mbona haijawahi kuleta majibu ya tume hizo tangu zimeanza kuundwa zaidi ya kuwahadaa watanzania?
Kwanini tusiamini kama matukio haya yanafanywa na wao wenyewe huku wakiisingizia chadema?. tumechoka kufungwa macho huku watanzania tuwekwe wazi tujue.
Kama serikali yetu ambayo ndiyo yenye dhamana ya kulinda haki za binadamu imekalia kimya unyama huu nani alaumiwe?.Ni waliofanya vitendo hivyo au wale waliowaacha huru ili waendelee kuyafanya haya?
TUMECHOKA KUONA DAMU ZA NDUGU ZETU ZIKIMWAGIKA...WATANZANIA TUNATAKA AMANI