Nanenane 2016.

Nanenane 2016.

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,650
Reaction score
21,007
Nilikuwa kwenye maonyesho ya nanenane hapa Mbeya. Nimejifunza mambo mengi kwenye vitalu vya Jkt nimejifunza kuhusu kilimo cha mboga mbalimbali exotic kama Kandoro, lettuce, turnip na nyingine inaitwa beet roots. Pia wanafundisha ufugaji wa nyuki, samaki, kuku, ng'ombe na sungura.

kwenye banda la TANAPA nimejifunza mambo mengi ya kuvutia.
kwenye banda la Yara nimejifunza mambo mengi kuhusu matumizi sahihi ya mbolea
kwenye wizara ya maji na umwagiliajji nimejifunza kwa uzuri sana kuhusu schemes za umwagiliaji. wanafundisha vizuri sana.

pia nimekula chips, nyama choma, fanta passion, juisi ya ukwaju na sambusa. pia kuna burudani mbalimbali za mziki.

wewe umejifunza nini nanenane ya mwaka huu?
 
Mkuu mi naenda leo...ila ninavyopenda kilimo hakyanan ntatamani niibe trekta moja
 
Nitaenda jumamosi.

Nataka nijifunze zaidi kwenye ufugaji hasa wa kuku, ng'ombe wa maziwa na nyama, mbuzi na nguruwe.

Kidogo nitajifunza kuhusu ufugaji wa nyuki na kilimo cha mpunga na migomba.

Mwaka jana nilijifunza zaidi kwenye kilimo cha mazao ya msimu, mbogamboga na matunda. Nikipata muda mwaka huu nitafanya recap kidogo.
 
Naomba unieleze zaidi kuhusu beetroots inaweza kuota sehemu za joto? Napenda sana hilo tunda
 
Nitaenda jumamosi.

Nataka nijifunze zaidi kwenye ufugaji hasa wa kuku, ng'ombe wa maziwa na nyama, mbuzi na nguruwe.

Kidogo nitajifunza kuhusu ufugaji wa nyuki na kilimo cha mpunga na migomba.

Mwaka jana nilijifunza zaidi kwenye kilimo cha mazao ya msimu, mbogamboga na matunda. Nikipata muda mwaka huu nitafanya recap kidogo.

Hapo kwenye Nguruwe ndio mpango mzima.
 
Yara ndo nahitaji kuwaona ili wanipe maelekezo sahihi ya mbolea zao
 
Back
Top Bottom