Namuona Alikiba akiachwa na Harmonize

Namuona Alikiba akiachwa na Harmonize

sangujoseph

Senior Member
Joined
Nov 30, 2015
Posts
164
Reaction score
184
By Sangu Joseph

Miezi kadhaa iliyopita niliandika mawazo yangu (Tathmini yangu kwa Harmonize nje ya WCB - JamiiForums moja ambao), mwisho nilijiuliza Harmonize atachukua nafasi ya nani kati ya Alikiba au DiamondPlatnumz, mwisho nikasema labda tuone historia mpya ikiandikwa kuwa mafahari watatu wakikaa kwenye zizi moja la BongoFleva.

Leo niendelee kutokea hapa, tumeona Album ya Konde Boy, na sasa #Dodo ya KingKiba, kila mmoja ni ametisha kwa upande wake, Kiba audio kali sana video ndiyo usiseme tumempata Alikiba tunayemjua kiufupi Ngoma imekamilika kila idara changamoto zilizopo ni za kawaida sana (Nitaeleza siku nyingine), kuhusu bwana Rajab KondeBoy niliasheleza kitambo sana kupitia ( Tathmini ya Sangu J kuhusu uzinduzi wa albamu ya #AFROEAST ya Harmonize - JamiiForums ) na ( PART 2 : Tathmini ya SanguJ uzinduzi wa albamu ya #Afroeast ya Harmonize - JamiiForums ) hayo ndiyo majibu.

Kwa nilichokiona kati ya hao wawili, Kiba na Konde Boy ndiyo battle kubwa iliyopo sasa, kwa sababu asilimia kubwa ya wanaomsapoti Konde ndiyo hao wanaomsapoti Kiba, sasa kinachokuja ni kugawana tu.

Sasa kwenye battle ya kugombea kugawana wadau wanaowasapoti mara nyingi anayeshinda ni yule mwenye Project nyingi sana, na hapo unamuona Konde Boy akiwachukua wadau wengi sana, Ila kazi ya Alikiba moja inaweza kuwa kali kuliko kazi zote za KondeBoy ila tatizo la Bwana King, anakaa muda mrefu kutoa ngoma, plus na wasanii wake, huku ndugu Konde akiwa One-man Army.

Kwa Diamond ni tofauti kwa sababu yeye kitambo inajulikana haungwi mkono na wengi wanaowaunga mkono King na Konde Boy hivyo kwake anafurahia na kunywa kahawa pale Kijiweni Madale, akiwa ameweka miguu juu.

Kwa sasa game Battle ya Alikiba, Konde na Chibu imefikia patamu sana kwa sababu wanaojudge ni mashabiki Ila itakua tamu zaidi.

Insta: FB: Twit: SanguJoseph

#KijanaMzalendo #IloveTZ

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana alikiba anawanyima usingizi sana..kama alikiba ni mbovu mbona mnawapambanisha na hao wasanii wenu.si mpambanishe na wakina juxna wengine wapo wengi tu. Jibu ni kiba ndio king wao usipo mshinda nisha na kiba basi ujue huyo ni utipolo.wamekuja wataondoka watamuacha . Kale DODO upoze moyo wako maana ni tiba tosha.
 
Ali Kiba mzembe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu binadamu hatufanani hata ufanyeje kiba awezi kuwa mondi na mondi awezi kuwa kiba..kama mpenzi wa mpira sawa Ronaldo na Messi. Ronaldo anatimia nguvu sana kwakufanya mazoezi illikufanika malengo yake na amefanikiwa na Messi anafanya mzoezi yakawaida ila hutumia kipaji chake sana ili kufanikisha malengo yake nae pia amefanikiwa. Muache mtu apende akitakacho.
 
Hizo battle mnaleta nyinyi wenyew wanakula bata hawana habari nyinyi mnawapambanisha duuu fanyeni yenu banaa
 
Mbona unajikanganya kijana?mara hujui anachoimba mara unafahamu uwepo wa jeje..lol..hueleweki mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Moja kati ya utumbo alio umwaga.kwahyo kama nafahamu ndio anajua..unamsifia mtu wakati nyimbo yake unasikiliza mdundo tu.hamna cha ziada aeleweki anaimba nini
 
NI kama vile wanafunzi wakishindwa kuelewa mathematics utasikia mwalimu fulani haeleweki mara hivi mara vile
Ni mfano halisi kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe unaelewa kitu gani zaidi yakutikisa kichwa unasikiliza mdundo tu.yeye mwenyewe haelewi kaimba nini sembuse wewe.
 
Back
Top Bottom