Namtafuta baba yangu na ukoo wake

Namtafuta baba yangu na ukoo wake

Pole sana wewe nenda hapo ulipozaliwa pia ktk kituo hicho cha kazi ulizia hapo hata marafiki zake mama yako, lazima utapata hata mmoja wapo anaweza kukupa mwanga wowote, ili upate pakuanzia
 
Nilichogundua hii familia Ina pepo la utengano. Huyo alijetokeza Kama anamjua huyu dogo nae anashangaa kwanini hawawasiliani kwa miaka 13.... Funny enough mnakuja kutajana majina yenu halisi humu ukutani. Wachaga wakikutana kila mwezi wa 12 mnawatukana, ni mpaka watoto wenu watakapopeana mimba ndo mtajua umuhimu wa family reunion.

My word:
Wewe uliyejitokeza hapa Kama unamjua huyu mleta mada na wengine, fanyeni grand family reunion moja tu itawasaidia. Acheni upuuzi. Hata huyo mnaemtafuta anaweza asiwe msaada Kama nyie wenyewe hamna umoja. Gadem.
Tatizo ume coment kishabiki sana ..wee ujui kitu ni bora ukauliza kuliko kuja na mambo ya pepo
 
Nimeupenda huu mtiririko wa hii mada, hongera Geofrey Maseta kwa kujitokeza kumsaidia ndugu yako ni wachache sana wenye moyo huo mwingine angeona post akapotezea

Pia nakushauri yamadongo ukishindwa kupata majibu kwa maseta nakushauri rudi kule Tabora ulikozaliwa hata kama ulienda ukakuta wengi ni wageni/wapya nachoona mimi hukufanya tracing nzuri kama mama alikuwa askari magereza huo ni mwanzo mzuri ebu jaribu kuulizia wakuu wake wa kazi na co-workers enzi hizo (wakitumia rosters, jinsi alivyokuwa anapangiwa kazi lazima kuna wale ambao mara nyingi alikuwa anapangwa nao, na mara nyingi story za wapenzi kutendwa na kadhalika tunawapa sana marafiki zetu kuliko ndugu.) nadhani hata kama walihamishwa hawawezi kuwa wote lazima wengine washajenga maeno yale yale.
 
Baba asiye mtafuta mtoto, amepoteza sifa ya ubaba. Kumtafuta mtu asiye na sifa unayomtafutia ni kupoteza muda. Maisha bila baba yanawezekana. Tumia muda wako kufanya ya maana.
 
Mimi nakupa pole. Ila ilikuwa vyema kama ungeweka mawasiliano yako. Fikiria mtu anapeleka taarifa zako kwenye magroup, je wawasiliane na nani sasa?
 
Baba asiye mtafuta mtoto, amepoteza sifa ya ubaba. Kumtafuta mtu asiye na sifa unayomtafutia ni kupoteza muda. Maisha bila baba yanawezekana. Tumia muda wako kufanya ya maana.
Mkuu kuna wengine wanaweza ku fanya ngono ya siku moja, wakaachana na mama akashika ujauzito na hata asiweze kum-trace ni nani kampa ujauzito.
 
Mkuu kuna wengine wanaweza ku fanya ngono ya siku moja, wakaachana na mama akashika ujauzito na hata asiweze kum-trace ni nani kampa ujauzito.

Huyo ni baba kweli? Nway, kila mmoja na anavyoguswa. Binafsi, ni heri niitwe sina baba kuliko baba wa aina hii hata akipatikana. Kwa umri wa mpaka unaandika Jf, inafaa kuhangaika kufa na kupona kwaajili yako na wale atakaokupa Mungu.
 
Huyo ni baba kweli? Nway, kila mmoja na anavyoguswa. Binafsi, ni heri niitwe sina baba kuliko baba wa aina hii hata akipatikana. Kwa umri wa mpaka unaandika Jf, inafaa kuhangaika kufa na kupona kwaajili yako na wale atakaokupa Mungu.
Mkuu lakini kuna situation nyingine ambazo baba anaweza asiwe na makosa, hasa mwanamke anapokuwa anatembea na wanaume wengi kwa wakati mmoja. Kuna dada mmoja alikuwa ''mwingi'' akapata ujauzito akashindwa kujua kwa hakika ni nani alimpa ujauzito. Akaamua kufa na mwanamme mmoja (ambaye nadhani alimchagua kwa sababu alikuwa na fedha kuliko wale wengine). Mtoto alipokuwa ikajajulikana sio wa yule mwanamme aliyesakiziwa. Na kuwapata tena wale wengine ilikuwa shida kwani siku zilishaenda. Matukio kama haya ni common sana kwenye ngono za chap chap!
 
Back
Top Bottom