Pierina Vicka
JF-Expert Member
- Mar 18, 2017
- 223
- 488
Pole sana,umejaribu kwenda huko kahama?Habari za wakati huu wapendwa, mimi naitwa PENDO GERVAS KALILO. Nilizaliwa mwezi Septemba mwaka 1993, Kahama. Kwa sasa ninamtafuta baba yangu mzazi ambaye anaitwa GERVAS KALILO. Sijawahi kumuona baba yangu, na jina lake nililiona kwenye kadi yangu ya kliniki likiwa na majina hayo mawili tu.
Mama yangu aliitwa KHADIJA OMARY KABONA, mwenyeji wa Masumbwe. Kwa maelezo niliyopewa na bibi yangu, mama alitoka Masumbwe na kwenda Kahama kufanya kazi za ndani. Akiwa huko alipata ujauzito. Inasemekana baba yangu alikuwa mfanyakazi wa dukani, wakati mama yangu alikuwa akifanya kazi za ndani.
Mama alipofikia kipindi cha kujifungua, alishindwa kujifungua kawaida na alifanikiwa kujifungua kwa njia ya upasuaji. Bibi yangu hakuwa na taarifa kuhusu hali hiyo. Boss wa mama yangu alisafiri hadi Masumbwe kwa teksi kumjulisha bibi kwamba mwanawe amejifungua mtoto wa kike, lakini amejifungua kwa upasuaji, hivyo alihitaji kwenda kumuuguza.
Bibi yangu, pamoja na mtoto wa kaka yake aitwaye ELIZA, walipanda teksi pamoja na huyo boss wa mama na kwenda Kahama. Walipofika Kahama, bibi alikaa kwa muda, kisha akarudi Masumbwe. Mimi na mama yangu tuliendelea kubaki kwa boss wake mama, ambaye inasemekana aliishi katika eneo la Uhindini.
Baadaye, mama yangu aliwahi kusafiri kwenda Singida kwa kaka yake na alikaa huko kwa miaka kadhaa. Aliporudi Kahama, alifika tena kwa yuleyule boss wake wa zamani. Mama yangu alifariki mwaka 1999.
Kwa sasa nimeamua kumtafuta baba yangu. Bibi yangu ana umri mkubwa na kuna mambo mengi hayakumbuki vizuri, hivyo ninapojaribu kumuuliza siwezi kupata maelezo ya kutosha kuhusu baba yangu.
Baba, kama bado uko hai, natamani sana siku moja nikuone. Natamani pia kukufahamu wewe ni nani, maisha yako yalikuwaje, na kama una familia nyingine ningependa pia kuwafahamu.
Sina nia nyingine yoyote zaidi ya kutafuta ukweli wa nilikotoka na kumfahamu baba yangu mzazi. Kama kuna mtu yeyote anayemfahamu GERVAS KALILO, aliyewahi kuishi au kufanya kazi Kahama, hasa katika eneo la Uhindini, au ana taarifa yoyote inayoweza kunisaidia kumpata, naomba anisaidie kwa kunipa taarifa.
Asanteni sana kwa msaada wenu. Mungu awabariki. 🙏
kwa yeyote mwenye taarifa za uhakika ani PM au apige namba hii+255 689 848 090🙏
Mbona kama ukienda alipokua anafanyia kazi mama yako utampata huyu baba kirahisi sana kuliko mtandaoni?Pole sana,umejaribu kwenda huko kahama?
Sahihi mkuu!Mbona kama ukienda alipokua anafanyia kazi mama yako utampata huyu baba kirahisi sana kuliko mtandaoni?
Kama alikuwa muuza duka siyo rahisi kumpata. Pia unaweza kumpata na ukawa disappointed vibaya sana. All in all jaribu ila usipompta usisikitike kwa kuwa bibi yako amekupa maisha, anzia hapo.Habari za wakati huu wapendwa, mimi naitwa PENDO GERVAS KALILO. Nilizaliwa mwezi Septemba mwaka 1993, Kahama. Kwa sasa ninamtafuta baba yangu mzazi ambaye anaitwa GERVAS KALILO. Sijawahi kumuona baba yangu, na jina lake nililiona kwenye kadi yangu ya kliniki likiwa na majina hayo mawili tu.
Mama yangu aliitwa KHADIJA OMARY KABONA, mwenyeji wa Masumbwe. Kwa maelezo niliyopewa na bibi yangu, mama alitoka Masumbwe na kwenda Kahama kufanya kazi za ndani. Akiwa huko alipata ujauzito. Inasemekana baba yangu alikuwa mfanyakazi wa dukani, wakati mama yangu alikuwa akifanya kazi za ndani.
Mama alipofikia kipindi cha kujifungua, alishindwa kujifungua kawaida na alifanikiwa kujifungua kwa njia ya upasuaji. Bibi yangu hakuwa na taarifa kuhusu hali hiyo. Boss wa mama yangu alisafiri hadi Masumbwe kwa teksi kumjulisha bibi kwamba mwanawe amejifungua mtoto wa kike, lakini amejifungua kwa upasuaji, hivyo alihitaji kwenda kumuuguza.
Bibi yangu, pamoja na mtoto wa kaka yake aitwaye ELIZA, walipanda teksi pamoja na huyo boss wa mama na kwenda Kahama. Walipofika Kahama, bibi alikaa kwa muda, kisha akarudi Masumbwe. Mimi na mama yangu tuliendelea kubaki kwa boss wake mama, ambaye inasemekana aliishi katika eneo la Uhindini.
Baadaye, mama yangu aliwahi kusafiri kwenda Singida kwa kaka yake na alikaa huko kwa miaka kadhaa. Aliporudi Kahama, alifika tena kwa yuleyule boss wake wa zamani. Mama yangu alifariki mwaka 1999.
Kwa sasa nimeamua kumtafuta baba yangu. Bibi yangu ana umri mkubwa na kuna mambo mengi hayakumbuki vizuri, hivyo ninapojaribu kumuuliza siwezi kupata maelezo ya kutosha kuhusu baba yangu.
Baba, kama bado uko hai, natamani sana siku moja nikuone. Natamani pia kukufahamu wewe ni nani, maisha yako yalikuwaje, na kama una familia nyingine ningependa pia kuwafahamu.
Sina nia nyingine yoyote zaidi ya kutafuta ukweli wa nilikotoka na kumfahamu baba yangu mzazi. Kama kuna mtu yeyote anayemfahamu GERVAS KALILO, aliyewahi kuishi au kufanya kazi Kahama, hasa katika eneo la Uhindini, au ana taarifa yoyote inayoweza kunisaidia kumpata, naomba anisaidie kwa kunipa taarifa.
Asanteni sana kwa msaada wenu. Mungu awabariki. 🙏
kwa yeyote mwenye taarifa za uhakika ani PM au apige namba hii+255 689 848 090🙏
🙏Kama alikuwa muuza duka siyo rahisi kumpata. Pia unaweza kumpata na ukawa disappointed vibaya sana. All in all jaribu ila usipompta usisikitike kwa kuwa bibi yako amekupa maisha, anzia hapo.
🙏Kazi ipo mzee alikuwa mfanyakazi pengine alikuwa ni mwenyeji wa eneo hilo au nje ya hapo....
Jitahid Utampata
SawaMtoto sio mali ya mzazi ila amepitia tu kwa mzazi
Sipajui kuna nyumba nyingi pale at least ningejua jina la boss wake mamaMbona kama ukienda alipokua anafanyia kazi mama yako utampata huyu baba kirahisi sana kuliko mtandaoni?
AmenMungu akusaidie umpate baba yako
AmenMungu akufanyie wepesi na akukutanishe na mzee wako
Nitashukru sanaSawa Sawa Utampata Hata Huo Ukoo Tu
Amen 🥹🙏No matter what happened miaka ya nyuma, wewe huna hatia, nakuombea kwa Mungu huyu mzee apatikane akiwa mzima wa afya.
Me nakushauri achana nae kwanini yeye hakutafutii wewe ni mkubwa Sasa unapaswa kutulia na mume wako.Sawa