Namshangaa Mh. Mbowe....!!

Namshangaa Mh. Mbowe....!!

UKIWA mtwambie watanzania kuwa mnajiandaa kukataa matokeo...kwa visingizio vya kijinga...kuwa tume wamepelekwa maafisa wapya...mbona hamkugoma kuingia kwenye uchaguzi kama mlijua tume sio huru?

Lubuva kaishatwambia tutapiga kura wenyewe na tutazihesabu wenyewe vituoni na kubandika....sasa hao makamishna wanatuhusu nini na watatuibia vipi kura...

Akili za mbowe zinaendana na kiwango cha elimu yake tumhurumie...
 
Akihutubia wananchi wa Vunjo amesema Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC haiko huru kuanzia leo,baada ya baadhi ya watendaji kubadilishwa hivyo kuanzia sasa wananchi watambue Tume yao haiko huru.

Hivi kabla ya baadhi ya watendaji kubadilishwa Tume ilikuwa huru?

Ina maana miaka yote Tume ilikuwa huru Hadi leo watendaji walipobadilishwa ndio imekosa uhuru.?

Mh.Mbowe uache kutulaghai wananchi na kutuona hatuna uwezo wa kufikiri wala kuona kinachoendelea ndani ya siasa zetu.!

Wengi tunaelewa Tume haiko huru miaka yote , hivyo unaposema kuanzia leo, unawafanya wenye uelewa wazidi kukushangaa kwa misimamo na kauli zako zenye ukigeugeu.!
Wewe ulitaka asemeje? Andika hapa maelezo unayo ona ni sahihi ili tukosoe alichosema.
 
Dah ushabiki mbaya mbowe alichosema kipi cha uwongo na ni lini mbowe aliwahi kusema tume ya uchaguzi ii huru???
Siku zoooote tumeshihudia wakilalamika tume haiko huru
Na Hii leo imejidhirisha baada ya baadhi ya ma officer kuondolewa nyakati izi??
 
Wewe ulitaka asemeje? Andika hapa maelezo unayo ona ni sahihi ili tukosoe alichosema.

Kinachohojiwa ni kusema kuanzia leo kana kwamba huko nyuma Tume ilikuwa huru, halafu hana mamlaka ya kumpangia Rais muda wala mtumishi wa kumteua pale NEC.!

Ni vema Mbowe angesema sheria iliyovunjwa kuliko kuwajaza ujinga watanzania, kila alichokifanya Rais kipo ndani ya mamlaka yake, hata leo anaweza kumtoa Lubuva sheria inamlinda.
 
"Kila mtanzania" ina maana ya "unanimous"

Kwa hiyo basi hakuna haja ya kulalamika, kupiga kampeini na kufanya uchaguzi. Kufanya kampenini ni kuwaomba watanzania wasiotaka kukupa kura ili wakufikirie kukupa kura zao. Kabla ya kupiga kura, hakuna ajuaye mshindi ni yupi. Tuliofuatlia chaguzi hizi kwa muda mrefu tunajua kuwa wingi wa watu mkutanoni siyo reflection ya kura kabisa. Wengine huuhudhuria ili kuptisha muda tu kwa vile wanakuwa hawana la kufanya wakati huo.
Usihangaike sana na hawa vijana ambao wamejaza ushabiki kwenye fikra zao.

Mbowe kwa kutambua fikra zao fupi, kwa sasa anawatumia kama anavyopenda.

Mbowe ni kati ya wanasiasa wasio na aibu katika ulaghai hata mbele ya watu wenye fikra pana.
 
Dah ushabiki mbaya mbowe alichosema kipi cha uwongo na ni lini mbowe aliwahi kusema tume ya uchaguzi ii huru???
Siku zoooote tumeshihudia wakilalamika tume haiko huru
Na Hii leo imejidhirisha baada ya baadhi ya ma officer kuondolewa nyakati izi??
Ushabiki unakufanya usione udhaifu kwenye kauli ya Mbowe.
 
UKIWA mtwambie watanzania kuwa mnajiandaa kukataa matokeo...kwa visingizio vya kijinga...kuwa tume wamepelekwa maafisa wapya...mbona hamkugoma kuingia kwenye uchaguzi kama mlijua tume sio huru?

Lubuva kaishatwambia tutapiga kura wenyewe na tutazihesabu wenyewe vituoni na kubandika....sasa hao makamishna wanatuhusu nini na watatuibia vipi kura...

Akili za mbowe zinaendana na kiwango cha elimu yake tumhurumie...
Nahisi Mbowe anawaandaa wafuasi wake baada ya kuhisi gia ya Angani kubuma.
 
Siku za hivi karibuni alisema watagomea uchaguzi kutokana na kutokuwa na haki akaja na agenda ingine hyoo kwa wananchi kuwa tume kwanzia leo haiko huru hyoo yote inaokana na ku paniki na kukosa hoja pole sana ukawa
 
Watafute viongozi wako wa ukawa na uwaeleze kuwa waache kutudaha kutokana na kupaniki na kile kinacho endelea ndani ya umoja huo
 
Akihutubia wananchi wa Vunjo amesema Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC haiko huru kuanzia leo,baada ya baadhi ya watendaji kubadilishwa hivyo kuanzia sasa wananchi watambue Tume yao haiko huru.

Hivi kabla ya baadhi ya watendaji kubadilishwa Tume ilikuwa huru?

Ina maana miaka yote Tume ilikuwa huru Hadi leo watendaji walipobadilishwa ndio imekosa uhuru.?

Mh.Mbowe uache kutulaghai wananchi na kutuona hatuna uwezo wa kufikiri wala kuona kinachoendelea ndani ya siasa zetu.!

Wengi tunaelewa Tume haiko huru miaka yote , hivyo unaposema kuanzia leo, unawafanya wenye uelewa wazidi kukushangaa kwa misimamo na kauli zako zenye ukigeugeu.!

Mbowe na wafuasi wa UKAWA sasa hivi UKIWA umewatawala!!! Wamepagawa baada ya kushtuka wanapigwa mbele na nyuma
Wakishngaa tena....wanapigwa Juu na Chini..... Chezea Jembe Magufuli..... Team Magufuli Imetanda nchi nzima kwa ghafla.... Kuna vikosi vya anga! vikosi lukuki vya ncha kavu... vikosi lukuki vya invisible teams..... vikosi maalumu vya kwenye midahalo.....UKIWA walidhani kununua Wenye Magazeti, Wauza Magazeti, viongozi wa Boda Boda, Nyumba za Dini za Misukule na wachovu wengine, Makonda na wapiga debe wa dala dala nk KUMBE Tanzania ina wigo mkubwa!!! WACHA WAENDELEE KULALAMIKA...... Magufuli Ikulu yako baba.... zimebaki wiki mbili kwa UKAWA kuwa UKIWA RASMI...
 
Kimsingi Mbowe anapenda sana kulalamika, lakini akumbuke kwamba alisema wamemchukua Lowasa kwani ndo anajua wizi wa ccm, mbona tena anatapatapa?

Na wao wataangaika sana, kwani Mwl.Nyerere aliwahi kuwambia kwamba ni vema wakatafuta nafasi za kutumikia wananchi kwa maana ya serikali/mitaa, udiwani na ubunge alafu wakishaaminiwa wapewe nchi, walipuuza ushauri wa baba wa taifa, huwezi kuwa na wabunge 27 kati ya majimbo 266, alafu unataka Urais, ni aibu sana, wangetumia nguvu nyingi kwenye ubunge na udiwani maana yake tungepata hiyo tume huru na sheria nyingi zingekaa vizuri na ndo shida ya watz, wao wamekomaa na Urais wakati wagombea wao tena walio wengi hawana fedha za kufanyia kampeni, kila siku wimbo wao ni tume ya uchaguzi.

Kweli katika hali ya kawaida utawapatia nchi watu ambao kila kukicha ugombana kwenye nafasi za majimbo? hii nafasi ya Urais bado haiwafai kabisa.

Nadhani wanachama, wafuasi na mashabiki wa UKAWA, umoja usio chama cha siasa, wamekuelewa. Lakini, tunavyowajua humu jamvini utapata matusi kibao. Ukweli utabaki ukweli kwamba zamu hii watapata wabunge wachache. Nabashiri, Mnyika, Lissu, na Mdee, vijana machachari kisiasa na waliokuwa na mtazamo chanya wa mabadiliko, watakosa ubunge kwa kuwa vigeugeu.
 
Anachokifanya Chairman Mbowe ni 1. KUWAAMINISHA WATANZANIA KUWA CCM IMESHASHINDWA INATAFTA NJIA MBADALA HIVYO ANAWAHIMIZA NA KUWATIA MOLARI YA KUENDELEA KUSAPOTI UKAWA 2.AMESHAONA UPEPO SIO MZURI KWA UKAWA HIVYO ANATAFTA SABABU ASIJE ANGUSHIWA JUMBA BOVU KUWA YEYE NDO CHANZO CHA KUSHINDWA, faida yake ni kwamba anaweza akawin huruma ya raia kwani always mtu anayeonekana keonewa huwa anapata sapoti kubwa hivo raia wanaweza vutika kuipgia kula UKAWA kwa wingi, hasara yake ni kwamba anaweza akawakatisha watu tamaa wasiende kupiga kura wakiamini hata wakipiga wanayempigia hawezi shinda kwakuwa ataibiwa kura, na hii ni mbaya zaidi, mfano nina ndugu yangu tangu 2000 anawapigia wapinzani bt mwaka huu anasema ataipigia CCM pamoja na sababu nyingine anasema anawapigia kila mara ila hawashindi, sasa naye anatamni ushindi, sasa watu kama hawa wanaokata tamaa wapo, so Mbowe must be careful na nanma anavyolipresent otherwise kama walishashitukia dili kwanini na wao wasijipange kimya kimya kuangalia namna ya kudeal nalo kuliko kukurupusha ndege.
 
Kwa mtazamo wake yeye kutokana na vitendo vya Rais kubadirisha watendani wa Tume wakati zimebakia siku chache ndio umempa msukumo wa kusema maneno hayo. Jirani yako akienda kuiba kuku halafu manyoya akaja kumwagia nyumbani kwako kisha ukaja kukamatwa wewe kutokana na ushahidi wa manyoya ungekubaliana nalo hilo?
 
Mkuu huyu Mbowe ameshagundua wafuasi wake wengi hawana uwezo wa kuhoji kauli zake.

Ndio maana inafika wakati anatoa kauli zinazopingana na misimamo yake ya awali.

Kama Taifa hatuitaji viongozi vigeugeu na wasiosimamia misimamo yao, Mbowe amedhihirishi hilo na kuwa hapaswi kuaminiwa Maana kauli zake zinategemea zaidi upepo wa kisiasa kwa muda huo.

Nadhani umechanganya mambo hapo mkuu. Kwamujibu wa Twaweza wafuasi wengi wa Chadema niwale wanaojua nini kinaendelea ndani yanchi na Duniani kwaujumla. Yaani watu walioelimika (wasomi)

Bali Ccm ndoinaungwa mkono nawatu wasiojua A wala B. Wao wakiambiwa tu kidumu wanaitika kidumu. Hao ndowaliowengi nchi hii ila kdri sikuzinavozidi kusonga mbele wanatoweka maana waliowengi umri umewatupa mkono.
 
Nadhani umechanganya mambo hapo mkuu. Kwamujibu wa Twaweza wafuasi wengi wa Chadema niwale wanaojua nini kinaendelea ndani yanchi na Duniani kwaujumla. Yaani watu walioelimika (wasomi)

Bali Ccm ndoinaungwa mkono nawatu wasiojua A wala B. Wao wakiambiwa tu kidumu wanaitika kidumu. Hao ndowaliowengi nchi hii ila kdri sikuzinavozidi kusonga mbele wanatoweka maana waliowengi umri umewatupa mkono.
Hao wasomi wengi wamechangia nini kuhusu Demokrasia ndani ya Chadema Zaid ya kuburuzwa na maamuzi ya Mbowe.?

Kama wasomi wenyewe ndio wale wanaokubali demokrasia kuminywa ndani ya chama, wasio na uwezo wa kumkosoa mwenyekiti wao, basi afadhali mambumbu wa ccm wanaoruhusu Demokrasia ndani ya chama Chao hata kama inamashaka.
 
Back
Top Bottom