Katika watu nisiotaka hata kukutana nao ni pamoja huyu jamaa eti mwakilishi wa watu jimbo la Sikonge, hata sijui kazi zake kila siku ni nini?
wasting time to discuss about this eti member of parliament!!! -- watu wa sikonge hawana mwakilishi serikalini, kama unabisha fanya utafiti.
Hakuna kinachoendelea wilayani sikonge si kilimo cha tumbaku, uvuvi, uvunaji asali nk - vijana, kina mama, wazee wote wa wilaya hii wamechoka vibaya mno; mbunge hana mkakati wowote kunyenyua uchumi wa watu wa wake, yaani hata kuishawishi serikali kuwekeza hata viwanda vidogo vidogo hakuna, bulding capacity kwa vijana kujikwamua ki-uchumi hakuna aisee!!
Kama kweli tunataka kuendelea lazima 2015 tuchague mwakilishi atayetufikishia matatizo yetu, as of now Sikonge ipo nje ya ramani ya tanzania. Anayebisha atembelee vijiji hivi Sikonge yenyewe, Chabutwa, ipole, usunga, imalampaka, mibono na viunga vyake akajionee mwenyewe ninachokisema.