masanzu ngoja nikupe story niliyoisoma zamani kidogo.
Juma alikuwa kijana mtanashati sana. Mabinti wengi wa kijiji cha Chekereni walimpenda, lakini Juma hakujua ni jinsi gani aseme. Kati ya mabinti hao alikuwepo msichana mrembo sana Juliet. Juma alimpenda sana Juliet ila kama kawaida hakuwa na ujasiri wa kumwambia.
Siku moja akaenda kwa mganga kijijini kwao ili ampe dawa ya kumfanya apate ujasiri wa kuongea na Juliet. Mganga akampa dawa, akamwambia ipake mkononi kisha nenda kaongee naye. Juma alichukua dawa na kwenda kuongea na Juliet. Walikubaliana na harusi kubwa ikafanyika kijijini kwao. Baada ya harus Juma akaenda kwa mganga kumshukuru. Mganga akamwambia.."mwanangu, sikukupa dawa yoyote yale yalikuwa ni majivu tu, nilichofanya ni kukupa ujasiri.". **story imeishia hapo**.