Nampenda sana yeye na wanae lakini sasa..

Nampenda sana yeye na wanae lakini sasa..

RingaRinga

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2015
Posts
1,052
Reaction score
529
Ana watoto wake wawili ambao alitoka nao kwa mmewe wa awali, sikufahamu maisha yake baada ya kupotezana naye kwa takribani miaka 9 wakati huo sikuwa na ukaribu naye mkubwa, ni ile kufahamiana tu.

Nilikuja kuonana naye akiwa ameshazaa hao watoto na akiwa ameshatoka kwa mmewe huyo. Nilikuja kufaham kweli alitoka mwenyewe kwa mmewe, maelezo yake ni kuwa mmewe alikuwa kiwembe.

Nilianza kuwa na ukaribu naye tulipoonana naye mwaka jana January nikiwa ktk harakati zangu za kibiashara, (nafanya biashara ya simu na vifaa vyake, nikamsaidia kumpelekea simu yake kwa fundi, na hivyo nikamsaidia simu kwa ajili ya mawasiliano wakati yake naishughulikia kwa fundi. So through that nikawa na mawasiliano naye.

Siku moja nilimtoa out ktk moja ya fukwe za ndani hapa jijini kwa ajili ya maongezi. Niliongea naye kwa kirefu, kwa kuwa tayari nilifaham kiasi kuhusu maisha yake nilishawishika kumsaidia kuendesha maisha yake. Tukawa marafiki, marafiki kweli....!!

Mambo mengi yalipita katikati hapo mwisho tuliangukia ktk mahusiano ya mke na mme, tulikubaliana hivyo baada ya urafiki wa karibu sana na kumjali sana bila chembe ya masharti au matarajio ya kumfanya kuwa mpenzi au mke wangu, yeye ndiye aliyepropose hivyo.

Watoto alikuwa amewapeleka kwa bibi yao, taarifa zikawa zinakuja kuwa watoto wanauguaugua tukashauriana akawachukue.

Watoto walikuja lkn hakuwatambulisha moja kwa moja km mm ni baba yao, kwa kuwa sikuwepo wakati wanakuja (nafanyia shughuli zangu nje ya mji anapoishi), nikawa naongea nao ktk sim walikuwa wananiita uncle, nilipokuwa nakuja mjini nikawa silali pale lakini nilikuwa nashinda pale, natoka nao, tunafanya manunuzi na muda wote walijua mm ndo nawahudumia.


Ilikuwa vigumu kidogo kuwaingizia pin kuwa mm ni baba yao, tulishauriana yy awaambie lakini hakuweza nikamwambia aniachie kazi hiyo mm.
Nikawa naongea sana na watoto kwa simu, siku moja nikawatega nikawauliza tu; " napenda sana kuja kuishi na nyinyi, mtapenda?" wakasema wanapenda tena sana, nikawauliza "sasa mi nikianza kuishi na nyinyi mtapenda niendelee kuwa uncle yenu au baba?" wakasema kwa pamoja uwe baba (kumbuka yote haya niliyaratibu mm bila mama yao kujua kuwa lini nimepanga kuongea nao nn, kwa hiyo walijibu wenyewe bila msaada wa mama yao, wala hakuwa karibu wakati naongea nao)

NTAENDELEA kwnye comments punde..
 
So nikaongea na mama yao pale pale wakiskia, nikafanya km kumwuliza km na yeye anakubali niwe baba yao mlezi na yeye awe mke wangu akakubali.

Hilo soo tukawa tumemaliza,
tukakubaliana kufanya uzinduzi wa familia. Tukapanga kuifanya weekend moja ktk hotel moja ya maana kiasi hapa jijini, tukafanya na kulala hapohapo. Ilikuwa nzuri sana. Baada ya hapo maisha ya kifamilia yakaendelea.

Nilimuahidi mke wangu huyu kuwa lazima siku moja tifunge nae ndoa kwa kuwa spendi kuishi naye easy'easy, nikaendelea kumhudumia yeye na watoto kwa kila kitu kuanzia pango chakula na mambo mengine, nikamsaidia kumuingiza mtoto mkubwa shule stdI kwa kumkamilishia mahitaji na michango yote, mdogo chekechea.
Shida ikaja sasa (kiini cha topic), amekuwa akinidanganya sana kwa minajili ya kutaka nimpe pesa kwa ajili ya mambo ambayo sio ya kweli, km kusingizia ugonjwa, na mabo mengine ya kwao ambayo nilithibitisha baadae kuwa si kweli, lkn pamoja na kuumbuka nilikuwa namsamehe na kuendelea naye vizuri. Nikampa mpango mkakati wa kumtengenezea mtaji ili angalau afanye shughuli ztakazomwezesha kukidhi mahtaji yake mengine, lkn tulikosana baada ya yeye kuzidi kufanya vitu ambavyo slijua si level yangu kwa kipindi hicho, kuniomba mara kwa mara kusaidia ndugu zake hata kwa matatizo ambayo ni ya kijinga km kuendekeza mapenzi na wasichana wa shule(kuwatoa lockup).

NITAENDELEA punde....
sim yag inareboot kila baada ya muda
 
We endelea ....tu na ushika pembe...huyo mwanamke afai ndio maana kashindwana na mmewe mkuu
 
Halaf wakati flani nimekuwa naona km anafanya vitu pasipo na chembe ya woga kwamba naweza nikaondoa shilling yangu ktk mahusiano haya kwa kuwa sina mtoto hapo wala hana ujauzito wangu, so sina cha kupoteza wala kulaumiwa uzuri ndugu zake wanajua ukorofi wake na wema wangu.

Wakati fulani alinifanyia ujinga kwa kumshirikisha ndugu yake, akasingizia sim imeharibika hivyo nimnunulie nyingine, akawa hayupo hewani kumbe kamuuzia sim kaka yake akamwambia asiniambie, halafu akasajili namba mpya na kuitumia hiyo kwa watu wengine na ndugu zake.

Kaka yake hakupenda akaniambia na kunielrza kila kitu na kunipa namba mpya aliyosajili.

Nikaamua kumpiga ban, ili nione kinachomfanya ajiamini kias hicho,
sikuona lolote zaidi ya kupata shida kupita kias hadi akarudisha watoto kwa baba yao na yeye kuendelea kubahatisha maisha,
Aliharibikiwa akachuja, nikawa napata habari zake, kodi ya nyumba anadaiwa hajalipa mwezi wa 2, hela nilizomwekea hisa akazikopea, akala, wenyewe wakaja kuchukua vitu ndani.

Ndugu zake wakanisihi, nikamhurumia nikamlipia pango mwaka mzima, watoto wake walipelekwa kwa mke mwenzie mji tofauti na anapoishi baba yao, sakawa wanaugua bila huduma nikaambiwa nikamshauri awafate, akawachukua wakiwa wagonjwa, nikamsaidia kuwatibu na mambo ya lishe, maisha yakaendelea.
NNITAENDELEA...
 
Mkuu wewe simu ina reboot kila mda. Ina mana hata powerbank huna na licha ni mtu wa ma simu simu na accessories zake.

Sio case ya charge, ni window 535, sjui km ndivyo zilivyo au ni kitu gani
 
Sio case ya charge, ni window 535, sjui km ndivyo zilivyo au ni kitu gani
Hiyo unaitwa microsoft lumia. Ni mid range phones.... ni nzuri. Na kuji reboot huenda betri imeisha. Au inatingishika... ila ukweli unaujua mwenyewe na simu yako.
 
Msomaji naomba uelewe kuwa mdada huyu ni beutiful aina ya JLo hivi, siamini km uzuri wake unatawala akili zake.

Lakini mm nimeamua kumwonesha true Love ingawa siwasliani naye sana, wala hatu'do', na hakuna anayehoji kati yetu, naendelea kumhudumia yeye na wanae, nafanya hivi kwa ajili ya watoto wake tu,

Sasa najiuliza hivi mdada una watoto wawili umepata mtu anakupenda wewe na wanao, anakuhudumia vizuri tu pia umeahidiwa ndoa km hakutakuwa na kikwazo toka kwa X', unapata wapi muda wa kucheza na nafas km hii? (ingawa si kitu ninachokitaja kwake, naangalia na kujiuliza moyoni tu)
Why mtu awe na akili ya dizain hii?
Ni kitu nilichojiwekea nadhiri kuwa ntapenda kuoa mwanamke mwenye mtoto 1 au 2 aliyetendwa na x' nikiamini nitamsuprise kwa upendo wa aina yake, maana hata nisipokuwa karibu naye yeye, ni rahisi kuwa karibu na watoto, na ni rahisi kuonyesha upendo kupitia kwa watoto, ingawa haimaanishi kuwa sikuwa pationate kwake, nilikuwa pationate sana tu & she didn't regrate when it came to 6x6 issues.
 
Back
Top Bottom