Nampenda sana, jamani naomba ushauri

Nampenda sana, jamani naomba ushauri

Joined
Jun 24, 2013
Posts
6
Reaction score
0
umri wangu ni miaka zaidi ya 25 ni mkaz wa mby city. knamsichana nampenda sana kiasi kwamba sitamani msichana yeyote mwingine ktk dunia hii, lakin kinachoniumiza tangu nimekua naye hamna kipindi ambacho tumewahi kukaa kwa amani angalau wiki 2, ni malumbano wakat wote tena yasiyo na sababu ya msingi lakin anaonesha ananipenda sana tatizo cjui ni nini, hali ambayo imepelekea mimi kupata maradhi ya moyo na vidonda vya tumbo , kinachonishangaza tunashirikiana kwa kila hali na tuna kipindi kirefu sasa(miaka 6) nashindwa namna ya kutafuta amani kati yangu mimi na yeye, nampenda sana.
 
Tatizo ni hiyo miaka 6 bila mavuno yoyote...
Ugomvi wenu mara nyingi huwa juu ya mambo gani?
 
ulivyotaja mbeya umenikumbusha kichuna changu chitoto cheupe. hapo inaonekana kuna mmoja ana wivu wa kupindukia kwa mwenzake, ila mpaka unapata maradhi hamna upendo hapo. kwa umri wako bado mdogo sana jijenge kimaisha utapata anayekupenda zaidi.
 
Pole sana.......
Wapo baadhi ya watu wanapenda kubembelezwa,wanalianzisha vagi makusudi baada ya hapo umbembeleze.
 
Too much disagreement is a sign of incompatibility.....mkuina hamuelewani mara nyingi zaidi kuliko kuelewana, mnaspend muda mwingi kulumbana bila sababu kuliko kuagree pamoja, ni ishara damu zenu hazigandani. Achaneni,japo kwa muda uone kama utakufa.
 
Unapata vidonda vya tumbo, unapata ugonjwa wa moyo na wewe bado umeng'ang'ania tu! Unataka tukushauri nini ndugu yetu!?
Watu wanasema mapenzi mtu hushauriwi ni maamuzi yako mwenyewe, wee hujaona au kusikia watu wanakufa kwa mapenzi? Ndio mfano wako.

Mtu tatizo unaliona, tena unalo muda mrefu, acha likuue au achana naye upone.
 
Mwanzo wenu ulikuwaje? Sasa kama mnagombana hivyo bado hamjaoana what do u expect? Tena hadi maradhi umepata loh! Kisa? Utakufa cku si zako umuache mwenzio akiendelea na maisha! Fikiri nini chanzo cha migogoro yenu isiyokoma jadilianeni mmeshndwana kila mtu afate yake kwanini uteseke pengine c huyo mungu aliyekuchagulia that y hamuendani kimtazamo .tafakari!
 
my God,yaani huo umri wako mdogo jamani!
..mpaka unaumwa!!?aah,kweli bora utumie akili sio moyo lol!
...ww ni bora uachane nae, utakufa hapo!
..ss nawaza ht kumuacha utaweza kweli?
 
umri wangu ni miaka zaidi ya 25 ni mkaz wa mby city. knamsichana nampenda sana kiasi kwamba sitamani msichana yeyote mwingine ktk dunia hii, lakin kinachoniumiza tangu nimekua naye hamna kipindi ambacho tumewahi kukaa kwa amani angalau wiki 2, ni malumbano wakat wote tena yasiyo na sababu ya msingi lakin anaonesha ananipenda sana tatizo cjui ni nini, hali ambayo imepelekea mimi kupata maradhi ya moyo na vidonda vya tumbo , kinachonishangaza tunashirikiana kwa kila hali na tuna kipindi kirefu sasa(miaka 6) nashindwa namna ya kutafuta amani kati yangu mimi na yeye, nampenda sana.
Watu wasipoendana kitabia ndio inavyokuwa hivyo...mmoja akiwa moto mwengine lazima awe maji kupooza moto sio mafuta kuongeza moto...kwahio lazima mmoja wenu apoe kikiwaka au utakufa kwa presha...
 
my God,yaani huo umri wako mdogo jamani!
..mpaka unaumwa!!?aah,kweli bora utumie akili sio moyo lol!
...ww ni bora uachane nae, utakufa hapo!
..ss nawaza ht kumuacha utaweza kweli?
mkuu akimuacha akimuona anatoka na mwengine sio ndo moyo utasimama kabisa..LOL!!!!
 
umri wangu ni miaka zaidi ya 25 ni mkaz wa mby city. knamsichana nampenda sana kiasi kwamba sitamani msichana yeyote mwingine ktk dunia hii, lakin kinachoniumiza tangu nimekua naye hamna kipindi ambacho tumewahi kukaa kwa amani angalau wiki 2, ni malumbano wakat wote tena yasiyo na sababu ya msingi lakin anaonesha ananipenda sana tatizo cjui ni nini, hali ambayo imepelekea mimi kupata maradhi ya moyo na vidonda vya tumbo , kinachonishangaza tunashirikiana kwa kila hali na tuna kipindi kirefu sasa(miaka 6) nashindwa namna ya kutafuta amani kati yangu mimi na yeye, nampenda sana.
Pole sana ndugu yangu! lakini mbona mmekaa mda mrefu hivyo kwenye uchumba, jee mna lengo la kuoana, jee mna watoto?? Mimi nahusisha ugomvi wenu huo na wivu alionao mwenza wako!! kama utafuatilia kwa makini utagundua hilo! jaribu kumsikiliza vile anavyokwambia, labda hapendi uwe karibu na wanawake wengine, hasa wale anaowatilia mashaka!!
 
Aisee pole sana,ilishanitokea hiyo wakati nipo form six ila nikachukua maamuzi magumu kama El..
 
Muda mliokaa pamoja ni mrefu sana! Na inakera zaid muwe hamjafanya vitu vya maana na vya maendeleo, na labda haon future on you thats why
 
umri wangu ni miaka zaidi ya 25 ni mkaz wa mby city. knamsichana nampenda sana kiasi kwamba sitamani msichana yeyote mwingine ktk dunia hii, lakin kinachoniumiza tangu nimekua naye hamna kipindi ambacho tumewahi kukaa kwa amani angalau wiki 2, ni malumbano wakat wote tena yasiyo na sababu ya msingi lakin anaonesha ananipenda sana tatizo cjui ni nini, hali ambayo imepelekea mimi kupata maradhi ya moyo na vidonda vya tumbo , kinachonishangaza tunashirikiana kwa kila hali na tuna kipindi kirefu sasa(miaka 6) nashindwa namna ya kutafuta amani kati yangu mimi na yeye, nampenda sana.

hiyo ni kwaajili ya utoto tu kaka,mnapozidi kuwa watu wazima mtakaa sawa tu.hata mimi na wafu tulikuwa hivyo hivyo,tangu tunatongozana mpaka tunafunga ndoa ilikuwa ni baada ya miaka 9,tulikuwa tukikorofishana sana,yaani mpaka marafiki walikuwa wametuchoka mpaka wakatushauri tuachane.lakini kila nikianza kutafuta dem mpya mawazo yanarudi kwa mwenzangu au utakuta wakati wewe unahaha kutafuta mwingine yeye anakuwa mpole yaani unakata tamaa mwenyewe kuendelea na michakato.(sio kwamba anajua unatafuta,hapana.inatokea tu anakuwa kama ndo mwanamke aliyetulia sana)mpaka siku tunafunga ndoa kila mtu alikuwa anaamini hatuta maliza hata miezi sita,lazima makesi yetu na usuluhisho uwe wa mara kwa mara.YAANI NAKUHAKIKISHIA,TULIPOTOKA TU KANISANI KUFUNGA NDOA SIJUI NA MAUGOMVI YALIISHIA WAPI.TUNAELEKEA KUUMALIZA MWAKA WA NNE SASA,HAKUNA CHA UGOMVI WALA NINI.YAANI HATA SISI HUWA TUNAJISHANGAA ILIKUWAJE,SANA SANA TUNABAKIA KUTANIANA TU.HUWA NAMWAMBIA SIKU NIKILIANZISHA NITAMBEBA NIKAMTUPIE PADRI ALIYETUFUNGISHA NDOA ILI AMPELEKE KWAO,SI ANAJUA JINSI AMBAVYO HUWA NIKILIANZISHA HALI INAVYOKUWA...TUNABAKIA KUCHEKA NA KUFURAHI TU.YATAKWISHA TU
 
uchumba ukishakua sugu...malumbano hayaishi kwenye mahusiano...
pengine haoni kama una uelekeo wa kusettle nae
 
Acha uoga wa kuanza upya. Ukiwa na kitu halafu kikaharibika ukakipeleka kwa fundi kikaharibika tena, halafu kila wakati kinaharibika tu, basi itakuwa hunabudi kukiuza na kuongezea hela ili ununue kipya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom