Nikifanya reference na ule uzi wako mwingine..Za asubuhi ndugu zangu..
Natumaini mmeamka salama.
Ndugu zangu, dhumuni la kuleta uzi huu hapa jamvini ni kuomba msaada
hali ya mahusiano yangu imefikia pabaya.
Na sijui nafanyaje mpenzi wangu huyu amekuwa ni mtu wa visirani visivyo isha na majibu machafu hata kwa kosa dogo nilijaribu kumuonya kwa miaka miwili sasa tuliyokuwa kwenye mahusiano lakini hajirekebishi.
Kama binadamu wengine kuna makosa madogo madogo kama kuchelewa kufika eneo fulanu kutokana na kubanwa na shughuli na vingine vingi. Ila ninachoshindwa kumwelewa huwa ananijibu hovyo alafu anakimbilia kuachana kuliko kawaida kosa dogo amekimbilia kuachana sio mtu wa kusamehe anabeba visasi mno ukumkosea leo anakumbushia na ya zamani nimemvumilia lakini sasa nachoka nimesha jaribu kuongea na mzazi wake dada zake waongee nae.
Ata pretend wiki moja yuko sawa lakini baada ya hapo anarudia tabia zake nikijichunguza mimi sina kosa sijawahi hata kumsaliti nimekuwa mwanifu kwake lakini yeye hataki kuelewa kiburu kimemjaa nimemsaidia mambo mengi kwenye maisha yake, haswa kutokana na hana kazi ya kueleweka lakini naona juhudi zangu hatambui.
Akitishia kuachana nikikubali kukaa kimya baada ya wiki ananitafuta anaomba msamaha ("huwa anadai kuwa anachanganyikiwa mpaka kufikia hiyo hali ya kuniacha alafu baadae ndio anashtukia kuwa amenikosea, anadai kuwa ananipenda").
Naombeni ushauri ndugu zangu, nifanyaje?