Namna ya kumkamata mwanaume!!

Mada hii ya ukweli sana, ngoja nielezee masahibu niliyowahi kupitia:
1.Pekua pekua. Mpenzi tuliyekuwa tukiishi mikoa tofauti alikuja kunitembelea mahali ninapoishi. Nilipigwa search kuanzia picha mpaka salary slips. Nilipigwa search kama napekuliwa na wanausalama! Siipendi hii tabia, maana inaonyesha mtu hakuamini bila sababu ya msingi. Kwangu mimi, Love=trust.

2. High expectations. Hili nalo limekuwa ni tatizo kwangu kiasi kwamba kuna mpenzi wangu alishindwa kujizuia, akamwaga chozi akilalamika ati kitanda changu ni kidogo na matawi ya chini kuliko anacholalia home kwao. Hii sio nzuri, maana mimi naamini maisha yanajengwa mkiwa pamoja. Dada zetu wanapenda wakute kila kitu kimeota kama uyoga-kuanzia magari, nyumba, fedha zimetuna kwenye akaunti benki, nk.

3.Annoyingly pushy. Mpo kwenye gemu ndani ya 6x6, huku chura amemeza nyoka, akiona unaanza kukolea anaanza kukuuliza "..sasa mpenzi unakuja lini nyumbani?", "..utanioa?", "..sasa mpenzi ile hela niliyokuomba vipi?", "..mpenzi una mpango gani na mimi?". Huwa napata kichefuchefu sana. Sipendi mpenzi wangu awe na tabia za makahaba!

4. Mizinga ya mbagala na Gongo la mboto! I sympasize with the victims of the two calamities... wapenzi wetu wakati mwingine wanakuwa na too demanding as if umeshamuoa. Kuna mmoja aliniambia, "..mbona mama huwa ananiambia ukipata mchumba (mpenzi) ndo kila kitu anatakiwa akuhudumie?". Anaendelea: "..mama anasema wakati wa usichana wao, mchumba (mpenzi) alikuwa anahudumia kila kitu". Hapa watu wanashindwa kutofautisha mapenzi ya zamani na siku hizi. Zamani mtu anakuwa na mpenzi 1, toka usichana hadi uzeeni; leo jambo la kuachana baada ya mwaka au mwezi ni kawaida. Why would I want to invest so much in a potentially short term relationship?
Hapa sina maana wapenzi wasisaidiane. Ila inakuwa tatizo mpenzi (wala hata sio mchumba) anapoombwa ada ya shule wakati msichana ana familia inayomsomesha. Tusaidiane vitu vidogo vidogo ili hata mambo yakitushinda tunaachana bila hiyana. Sio kwenda mahakamani kudai magari na miradi mliyoanzisha pamoja kama wapenzi.

Angalizo: Hapa naongelea wapenzi. Sio wachumba wala wanandoa.
 

.....kwangu mie, wangu kafaulu yote na sasa yumo katika 'final exam' ya haya mawili....

Labda niongezee neno la akiba.....mara nyingi kwenye hatua hizi za mwisho kuna kina dada/mama ambao huamua "kuubeba" ujauzito kama '-guarantee-' ya kumkamata vizuri (assurance) huyo mwanaume (asijemkimbia) ambayo kwa tafsiri yangu hilo pia linaangukia kwenye category ya kumkamata 'pembe' huyo mwanaume.

Mnalizungumziaje hili? (....Kumradhi wazee wa 'msiikurubie zinaa,' na wahamasishaji wa nyota ya kijani)
 


Ahsante sana Kaka Mbu,

Hata mie michango yangu umesimama katika hizo nguzo. Labda ni kutojua kujieleza vizuri.

Sijui King'asti, BAK et al wanastumia nguzo zipi?

Mie sifanyi kazi ya kuuza data pasipo sababu ya msingi!!

Babu DC!!
 
Reactions: Mbu
Ahsante sana Kaka Mbu,

Hata mie michango yangu umesimama katika hizo nguzo. Labda ni kutojua kujieleza vizuri.

Sijui King'asti, BAK et al wanastumia nguzo zipi?

Mie sifanyi kazi ya kuuza data pasipo sababu ya msingi!!

Babu DC!!

........Si lazima ugonjwa Babu, hata kukinga ni sababu ya msingi pia!

Hahhahaahha nimedandia tren kwa mbele hata sijui mwaongeleani hapa...ngoja nisome
 

Mpendwa King'asti,

Hivi unaweza kuwa na uhakika kuwa ukimwambia hayo yote unafanya uhusiano wenu uwe imara?



Where do you draw the line? Kwamba hiki nimueleze na hiki nife nacho?

Kuna mshikaji wangu mama yake alikuwa kahaba wa kijiuza mitaa fulani ya Dar. Jambo hili lilimuumiza sana tena sana. Ila baada ya kijana wake kuwa mkubwa (nadhani wakati yuko college), mama aliacha kabisa na kurudi kijijini kulima. Hili ungefurahi kuambiwa na BF wako?

Babu DC!!
 

Soulmate hili la kina mama 'kuamua' kubeba mimba ndipo hasa wengi wetu tunapokosea. Wanawake wengi huwa tunaitumia hii silaha kama silaha ya kukumaliza kabisa kumbe ndo tunajimaliza. Kubeba mimba si 'uamuzi' wa mmoja, tena mwanamke pekee ni maamuzi ya pamoja na ambayo hujenga zaidi kuliko yakiamuliwa na mmoja. Ingawa pia sometimes kuna kujisahau kati ya wapenzi ambao sasa wameshaanza kujifeel 'confortable' to each other, ambapo utakuta hata kama walikuwa wanatumia kinga basi zinawekwa kando na hakuna wa kumwuliza mwenzie la vipi mbona??

Pili ukimya nao unachangia ni vema kama mnaanza kuwa pamoja na hamtuimii kinga basi kuwekane wazi kuwa hamna mpango wa watoto hivi karibuni kuliko kukaa kimya ukiassume kuwa mwenzangu ana 'ukubwa' wa kutosha kuelewa kuwa hatujaoana so hatutakiwi kuleta viumbe duniani kwanza.

Lakini la tatu na kubwa zaidi ni kuwa WOTE wawili mchukue tahadhari! Mkaka jua mzunguko wa mpenzio, kuwa makini katika utumiaji kinga kila mara, ukimwachia mdada peke yake kama ndo anazo hizo evil minds za kukushika pembe basi utakuwa umempa funguo mwenyewe!
 
........Si lazima ugonjwa Babu, hata kukinga ni sababu ya msingi pia!

Hahhahaahha nimedandia tren kwa mbele hata sijui mwaongeleani hapa...ngoja nisome

Karibu sana dada MwanajamiiOne,

Hii ni sub-item ya mada nzuri sana ya Mama Ashrati (which I have to acknowledge kwamba nimeipenda sana na ina mambo mengi mazuri kwetu sote, men and women). Kwa hapa, tunaongelea kama kuna haja ya ku-filter mambo ya kumwambia mpenzi wako au la (yale yanayohusu familia zenu na hata ukoo mzima).

Kuna wanaosema kuwa ni safe kumueleza kila kitu kuhusu familia yako (mfano, kama baba ni/alikuwa jambazi, shoga etc; au mama alikuwa mchawi, kahaba, mmbeya na mengine mengi). Pia tupo (Mie na Mbu) ambao tunasema kuwa haina haja kuanza kuanika familia yako. Ila tukaweka angalizo kwamba unaweza kusema baadhi ya mambo ambayo unadhani huko mbele yanaweza kuingia kwenye equation ya maisha yenu.

Binafsi naamini kuwa, kuna baadhi ya mambo ambayo hata GF/mchumba akigundua hawezi kuniuliza. I can't imagine my GF aniulize eti nimweleze jinsi mama yangu alivyokuwa kahaba/changudoa....!!! Nadhani nitapoteza appetite naye toka siku hiyo!!

Babu DC!!
 

Ehee kumbe. Nadhani msimamo wako wewe na Mbu na wengineo wenye mtazamo huo uko sahihi. Kuna mambo mengine ni bora yaendelee kukaa huko huko kwenye makabati na ikitokea yakaingilia utaratibu wenu wa maisha utayatolea maelezo yafaayo wakati huo,
 

Mama ashrat, nakuvisha taji la heshma...wambie bwana habarii za ndoa za siku mbili baada la kukutana sio ishu tushachoka sie
 
Ahsante sana ingawa hilo la mwisho nahisi linafaa kuambatana na kila unachofanya.

Kuna tatizo la wivu ambao hata makahaba wanao. Yaani unakuta mwanamke ni mpelelezi kuliko hata polisi
Na wanawake wengi mnadhani kumchimbachimba mwanaume ndo kuhakikisha anakupenda.
Wanasahau Mungu akipewa nafasi na wao kuwa na mienendo mizuri ya uamifu ni kipimo tosha mwanaume mwenyewe kujisema kuhusu anavyokufikiria. NB: Uaminifu sio pamoja nakutoa ngono haraka
 

Ndugu yangu MwanajamiiOne,

Wanaume/wakaka waonaweza kufuatilia hayo mambo ni wachache sana. Nilisikia hivi karibuni kwamba kuna wanaume ambao hata hawajui ni lini wake zao wanaingia kwenye mizunguko yao. Wanakuja kupata surprises baada ya kunawa kwa ajili ya dinner!

Nashauri wanawake/wadada wachukue precautions sana bila kujali kama wenzi wao wanawasaidia au la. Kwa sababu inapotokea mwanamke/msichana akapata mimba, yeye ndiye anayehangaika na hilo tukio na kubeba lawama nyingi!

Babu DC!!
 
Reactions: Mbu
Ehee kumbe. Nadhani msimamo wako wewe na Mbu na wengineo wenye mtazamo huo uko sahihi. Kuna mambo mengine ni bora yaendelee kukaa huko huko kwenye makabati na ikitokea yakaingilia utaratibu wenu wa maisha utayatolea maelezo yafaayo wakati huo,

MwanajamiiOne,

Karibu sana na shukrani kwa kuliona hilo. Binafsi naamini kuna mambo ambayo huwezi kukaa ukamsimulia mtu (achat tu mpenzi wako) kwa sababu hata wewe mwenyewe ukiyakumbuka unapata kiu ghafla na kutamani maji ya kunywa!

babu DC!!
 

The dirt paka,

Ni kosa sana kwa watu kudhani kuwa ngono za voda fasta zinasaidia kuimarisha mahusiano. Kwa ufupi zinasababisha mateso endapo mahusiano yanaishia njiani baada ya muda mfupi!!

Babu DC!!
 
Kama anakukera unatafuta jinsi ya kuliweka sawaKwa hekima na heshima
 
...Babu DC mie naomba kuuliza hapo kwenye bold...ni wakati gani muafaka wa kuongea mambo yanayohusu familia zenu? hasa kama kuna dosari/tuhuma dhidi ya wale waliomo ndani ya familia?


B. ukijiridhisha na kuamini uliyenaye anastahili kuambia baadhi ya mambo yanayohusu familia nasema baadhi kwa sababu kuna yakuambiwa mwanzo wa mahusiano na mengine kadiri mnavyoendelea na uhusiano
 

Babu DC kuna mambo mengine kwenye familia unaogopa hata kuyaweka hadharani kwa yale hayaathiri mahusiano yenu bora kuwa kimya imenikumbusha story ya dada mmoja alibakwa na baba yake mzazi akiwa mdogo alikuwa na akili za kutambua alichofanyiwa huwa najiuliza ataeleza hiyo story chungu kwa BF wangapi mpaka kujaolewa? nafikiri mengine yatajulikana safari inavyoondelea utapata maneno ya kueleza pindi muda wake ukifika
 
Vijana wa siku hizi hawana formula ya kuishi nao... unaweza ukamfanyia yote haya na mengine ya ziada na bado akakata kamba kutafuta "something" (kimada). tena ukimfanyia haya anajiona kuwa kumbe unampenda kupitiliza na ataanza kukudengulia na kukufanyia ndivyo sivyo... ni bora kupenda ila kutoonyesha kwa asilimia zote.... bakisha kiasi kwa ajili yako!!
 

Ahsante sana Blaki Womani,

Kwa ufupi, mie nisingependa kujua kama GF wangu alibakwa na baba yake mzazi....Naweza kumchukia sana huyo Baba mkwe mtarajiwa.

Nadhani watu hawajawahi kusikia shocking stories....hapana bwana, siwezi kuanza kujianika juani eti kwa sababu ya kujenga imani kwa mchumba wangu. Kama file langu binafsi halitoshi basi huyo siyo riziki!!

Babu DC!!
 
Reactions: Mbu

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…