Namna English Medium zinavyoua elimu yetu

Namna English Medium zinavyoua elimu yetu

sonofobia

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2015
Posts
1,249
Reaction score
4,537
Kwanza naomba mnivumilie wale nitakaowakwaza. Nataka nizungumzie kuhusu elimu yetu ya msingi haswa kwenye hizi English medium schools ambazo tumetokea kuziamini sana.

Hizi shule zinaua elimu ya nchi kwa sababu kubwa zifuatazo.

1. Watoto wanafanyiwa mitihani ya ndani mpaka ya mwisho. Mitihani ya ndani inafanywa na walimu ili kuwaonyesha wazazi kuwa watoto wanafanya vizuri, hii inavutia biashara ya shule. Pia mitihani ya mwisho haswa ya standard 4 na 7 inafanywa chumba cha mtihani yote ni sababu matokeo mazuri yanaitangaza vizuri shule.

2. Walimu wa kigeni haswa Wakenya na Waganda, hawa ni tatizo kubwa sana kwenye elimu yetu, najua hawa watu wa huko ni wazuri sana kwenye lugha ya kingereza hivyo hata wamiliki wa shule na wazazi wanawapenda sana, mwanzoni waliingia kama walimu wa English na science kidogo, ila sasa wanafundisha mpaka somo la kiswahili. Unashangaa mwalimu wa geography kutoka Kenya hajui hata ziwa Manyara lipo wapi, hajui hata kama Tanga ni jiji.

Mwalimu wa civics hajui hata TANU wala ASP, hamjui hata Waziri kawawa. Mwalimu wa history hajui hata Amboni caves ipo wapi. Hapa unategemea nini zaidi ya mtoto asiyejua vitu.

3. Watoto wanakaririshwa kama kasuku.

Matokeo yake ni nini.

Watoto wanamaliza elimu ya msingi wanaongea na kuandika kingereza lakini hawana uelewa kiundani wa mambo mengi. Fanyeni majaribio ya kuwatahini watoto majumbani muone matokeo yake mlinganishe na wanayopata darasani.

Watoto wanapofika secondary schools wanaonekana wameshuka baada ya kuachwa mbali na wanaotoka Kayumba. Kiukweli hawajashuka ila hicho ndio walichovuna huko English medium schools baada ya kulipia mamilion ya pesa.

Mwisho, Naomba Serikali ifanye ukaguzi wa kina kwenye hizi shule japokuwa nyingi ni za wakubwa. Kuna walimu wengi sana sio walimu ila ni waongea kingereza wazuri hawa ndio wanageuka walimu wa kutumainiwa bila kujali content zao.

Hizi ni shule ni bomu ambalo wazazi wengi na Serikali litawalipukia.
 
Umeongea kweli tupu mkuu pasipo kufuatilia vizuri maendeleo ya mtoto na kuwa nae bega kwa bega hakika utavuna mabua....mie mwanangu analeta matokeo ya mitihani nampa tena huo huo mtihani nione kama kweli alistahili hizo marks.
 
hili taifa lilishakufa....eti leo CCM wanawadanganya na mzee wa kukariri magufuli alafu mijitu inashangilia....mnaamini magufuli atafanya lolote chini ya mwongozo wa CCM...mkiamini Magufuli atakuwa huru tu kuamua.....tatizo nchi hii ni CCM.....si mtu....Watanzania watambue hilo.....tusaidiane kuelimishana hivyo....
 
hili taifa lilishakufa....eti leo CCM wanawadanganya na mzee wa kukariri magufuli alafu mijitu inashangilia....mnaamini magufuli atafanya lolote chini ya mwongozo wa CCM...mkiamini Magufuli atakuwa huru tu kuamua.....tatizo nchi hii ni CCM.....si mtu....Watanzania watambue hilo.....tusaidiane kuelimishana hivyo....

Out of topic
 
Umeongea kweli tupu aisee hizi shule wanapendezesha wazazi kwa ufaulu mkubwa mana hizi shule ni za binafsi wanataka biashara.
Tena hyo tendency ya kuwapa majibu inawafanya wawe vilaza na wasitumie akili na kusoma kwa bidii.
To me spoon feeding kwa watoto ni hatari sana ndo mana hawa huwazidi wa st kayumba English tu. Hata waliosema secondary za binafsi nao ni hvo hvo. Wakifika chuo ndo huongoza Ku disco wakati ufaulu wao ni mkubwa.
Hlo la walimu Wakenya nao ni tatizo kujua kingereza frequently sio sababu ya kufanya mtu kuwa mwalimu mzuri. Nao ni tatizo.
 
dah hapo kwenye kukaririshwa kama kasuku nakubaliana na wewe asilimia 100. Kuna siku nilikutana na watoto wa shule moja international nikawa nawauliza maswali, yaani ilikuwa ni kioja. Wote majibu ni sawa na yote siyo sahihi, kisha wote the way wanavyoanza kujibu maswali wote ni sawa. Yaani hizi elimu zimekuwa kituko sasa.
 
Siyo zote!.

Kama kuna za hivyo ni tatizo la supervisory system, imelala na kusubiri migawo ya mabaki ya mafungu.

Lakini English media schools nyingi zinafanya vizuri katika masuala mengi sana, ya kuajengea watoto uwezo na uelewa wa hali ya juu.
 
kuna watoto wa international school flani hivi ipo Arusha nilishangaa kuona eti hawajui ng'ombe ana miguu mingapi, moja kwa moja ikanipa picha kuwa yawezekana hata ng'ombe mwenyewe hawamjui... inasikitisha sana.
 
Siyo zote!.

Kama kuna za hivyo ni tatizo la supervisory system, imelala na kusubiri migawo ya mabaki ya mafungu.

Lakini English media schools nyingi zinafanya vizuri katika masuala mengi sana, ya kuajengea watoto uwezo na uelewa wa hali ya juu.

Kweli sio zote...Ila asilimia 95 zinafanya haya nayoyasema..Nimekuwa mwalimu kwenye hizi nazijua in and out..Wewe unasema zinawajenga watoto ndio wazazi wengi mnaaminishwa hivyo, zinawajenga kwenye nini labda?? wewe unazosema zinawajenga zipo ila sio hizi zenye wateja wengi..Wengi hapa hawawezi peleka hizo shule eg intl sc of Tanganyika, Feza nk zipo chache...

Mjiulize ile St Marrys iliyokuwa na watoto bora kabisa kwa nini imekufa? Ile product yake si mmesoma nayo mbeleni je walikuwa bora kama mlivyoaminishwa? ...Serikali iingie kuzikagua kiukweli kama ilivyofanya New Ambassador international ya zamani,hiyo shule ilikuwa ndio shule namba moja kitaifa kwa primary level ilipotegewa mtego ikakutwa ni haya nayoyasema...Leo ipo wapi?
 
dah hapo kwenye kukaririshwa kama kasuku nakubaliana na wewe asilimia 100. Kuna siku nilikutana na watoto wa shule moja international nikawa nawauliza maswali, yaani ilikuwa ni kioja. Wote majibu ni sawa na yote siyo sahihi, kisha wote the way wanavyoanza kujibu maswali wote ni sawa. Yaani hizi elimu zimekuwa kituko sasa.

Mkuu usichanganye international school na english media school. Ni vitu viwili tofauti kabisa.

Sema ulikutana na watoto wa academy/english media labda.

International schools hapa TZ ziko kama saba tu. Hapa unazungumzia shule kama International School of Tanganyika au Moshi n.k. Hizi zinachukua walimu wa viwango vya juu sana. Hata mwalimu wa Kiswahili anakua ni mwalimu aliyebobea kwenye hii lugha.

Ni hilo tu mkuu, nadhani mtoa mada kaeleza vizuri kuwa anazungumzia English Medium na hajasema international schools.
 
Kama kuna ka ukweli kwenye huu uzi.maana kuna watu nafanya nao kazi wazuri wa ki inglish sana tu ila uelewa wao wa mambo ni ziro.
Ngoja nifuatilie hili...
 
Mkuu usichanganye international school na english media school. Ni vitu viwili tofauti kabisa.

Sema ulikutana na watoto wa academy/english media labda.

International schools hapa TZ ziko kama saba tu. Hapa unazungumzia shule kama International School of Tanganyika au Moshi n.k. Hizi zinachukua walimu wa viwango vya juu sana. Hata mwalimu wa Kiswahili anakua ni mwalimu aliyebobea kwenye hii lugha.

Ni hilo tu mkuu, nadhani mtoa mada kaeleza vizuri kuwa anazungumzia English Medium na hajasema international schools.

Kweli mkuu watu wanachanganya sana, kila shule inayofundisha kwa kingereza wanadhani ni international school.

Uchawi wa kumloga mtanzania ni lugha ya kingereza, mtanzania akishaona mtu anaongea kingereza basi anamwona ni wa kimataifa ..Na ndicho wanacjowapatia wenye hizi shule . Nimefanya na watu akikuadithia huko kwao alikuwa anakata majani leo yupo bongo ni mwalimu wa vocational skills..International school haiwezi kutoa mwl Uganda kisha inampa mshahara laki 3 huyo sio mwl ni msanii tu.
 
kweli kabisa japo sio zote ila nyingi ni chenga sana, hakuna maadili wala heshima kuna mtoto nimekutana nae anajua Good morning tu kwa watu wote, hakuna tofauti hata kwa wazazi
 
Nimefundisha St Marrys, Hazina, Holly Cross, Tusiime. Najua faulo zote zinazofanyika najua furaha yenu wazazi na nini mnachotaka...


Ni kweli kabisa. Mimi baada ya kumaliza six nilipata kufundisha shule moja ya english medium kwa mda mfupi, uozo mtupu. Owners wanajua wapi pa kuwakamata wazazi-kiingereza tu. Mzazi akiona mwalimu anazungumza kiingereza anaamini shule ni bora kabisa. Kumbe hola tu. Hao waganda, wakenya na wazambia niliofundisha nao walikuwa average sana kwenye contents, walichowaweza owner ni fluency ya kizungu tu.
 
Back
Top Bottom