Namna bora ya kurefresh akili

careenjibebe

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2020
Posts
1,604
Reaction score
1,655
Yaani inafika wakati akili imechoka kabisa huna jipya unaloweza kufikiria, unajikuta huna hela ya kujitoa hata out na wa kuongea naye hauna. Unafanyaje ili kurudi kwenye hali yako ya kawaida!?

Yaani akili inakuwa kama imefunikwa na blancket hivi. Sijui unakuwa umepachoka unapoishi?
 
Ukipachoka unapoishi kama umepanga fanya mpango uhame, kama ni kwako na pesa ushasema huna pambana na mazingira kwa namna ingine. Jipe shughuli mbalimbali ambazo hazitakufanya ukawa idle muda mwingi, lima bustani, panda maua ilimradi uwe na shughuli na uyaepuke mawazo. Tembelea hata marafiki ubadilishane nao mawazo. ITASAIDIA.
 
Asante! Yaani natoka nikirudi ndani najikuta daaah!
Naona hii ya kutokukaa idle itanisaidia..wacha nijilazimishe tu
 
Mkuu ukitaka kurefresh mind, andika riwaya yoyote hata ya page kumi tu.
Utashangaa.
 
Unabadili fikra zako kutoka kwenye majuto na kuwa na amani ya kwamba 1 time utatoboa na ujione ni sawa na watu wengine wenye mafanikio
 

Karibu Yaeda......ukiona umechoka unaenda porini kurina asali.......
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…