Namba 10 pale Simba kitaalamu

Kwa uwezo wa wachezaji waliopo Simba kwa sasa na ukamuongeza mchezaji kama CHAMA anaweza kukupa kitu cha ziada chenye thamani zaidi kwenye mechi.
Sikatai. Chama ni zaidi ya Ahoua ila Simba mpya ilibidi ijengwe na sipendekezi kurudi nyuma maana itaendelea kupata shida kufunga ukurasa wake. Ni kama ilivyochukua muda kupata ujasiri wa kumuacha Zimbwe, bila kumuacha ingeendelea kusajili wachezaji mbadala na kusingizia hawatoshi kumbe zimwi la uwepo wake linafunika fursa ya kupata wachezaji wapya.

Ni tatizo hilo hilo lipo timu ya taifa. Mbona wenzetu wanaibua wachezaji wapya kila siku na ndiyo hao hao tunawakimbilia na kuwasifia, kwa nini na sisi tusipate ujasiri huo?
 
Simba wanatakiwa kusajili wacheza wa viwango vya juu sio akina Bajaber
 
Labda sijaeleweka. Hivi kwa kutumia akili tu ya kawaida Mutale ni wa kubaki Simba kweli? Akisema x-factor kwa uwiano wa zaidi ya Mutale yuko sahihi. Maema na Mutale wote wanacheza aina fulani ya pasi fupi kufungua timu na Maema ana uwezo wa pasi ndefu pia. Kuwaweka wote wawili ni upuuzi. Ni bora atafutwe mtu mwenye calibre kubwa zaidi kumtoa Mutale hapo. Mutale hapana kwakweli kubaki Simba. Hapana.
 
Nilimkataa Mutale toka msimu uliopita na niliwahi kushauri aachwe dirisha dogo ila nikashangaa akabaki.

Nilichoona ni kuwa Mutale baada ya kuanza kuonyesha uwezo fulani hasa mashindano ya FA na CAF, anahitaji maboresho maeneo kama mawili hivi ambayo kimsingi yanarekebishika.

Anahitaji kuboresha first touch zake (hili anaweza kuwa amechelewa ila anaweza kidogo kuboresha akilifanyia kazi) na pia kuongeza kidogo umbali wa pasi yake (hapa siongelei pasi ndefu ila naona mara nyingi pasi zake ni za hapa kwa hapa).

Simba ingekuwa na kocha msaidizi wa kumsaidia Fadlu ambaye kazi yake ni kufanyia kazi mapungufu ya mchezaji mmoja mmoja. Wachezaji wengi wa Simba mapungufu yao yanaoneoana kubaki pale pale. Nililiona kwa Che Malone, Zimbwe, Balua. Haya mapungufu hauyaondoi wala kuyapunguza kwa kuongea tu na mchezaji ila kwa kuingia uwanjani na kuyafanyia kazi.

Kwa jinsi nilivyomuona Maema CHAN katika game 1 au 2 nilizoangalia, Mutale ana nafasi kubwa kuwa na msaada kuliko Maema kama ataboresha hayo maeneo mawili.
 
Hivi Chama anamzidi Maema?
 
Phiri moses!?
Bonge moja la player, ndio hivyo tena kazi na umri.
Anaweza kucheza kama CF, kisha anacheza kama Ss, anazima kaka attacking midfielder, anaweza kicheza kama winger.. wachezaji wa vile nawapenda sana.. halafu ni miguu yote.
Mmoja wa wachezaji bora sana ambao Simba imewapata miaka ya hivi karibuni
 
Phiri moses!?
Bonge moja la player, ndio hivyo tena kazi na umri.
Anaweza kucheza kama CF, kisha anacheza kama Ss, anazima kaka attacking midfielder, anaweza kicheza kama winger.. wachezaji wa vile nawapenda sana.. halafu ni miguu yote.
Yap. Mpaka ana ondoka alikuwa top scorer kwenye team yetu, ila ali sugulishwa bench kisa majungu.
 
Hatimae CHAMA amereje Simba, kuna kitu kitaongezeka hasa kutengeneza nafasi kwa wafungaji.
 
huyu jamaa bado anaweza kuch3za angalau 2 yrs...

tumkumbuke pirlo...
Wamriufishe tu chama...
Akili imeshamrudi
Inakuwaje sasa baadhi ya mashabiki wasio ujua mpira kama cocastic wanalalamikia huu usajili wa Mwamba wa Lusaka?

Mimi nadhani Mangungu apewe tu miaka 5 mingine kwa kuifikisha simba hapa ilipo.
 
Ile pasi ya Chama kwenda kwa Mpanzu ndiyo kitu walikosa Simba kwa muda mrefu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…