Nakukemea Albert Chalamila, achana na Cocobeach

Nakukemea Albert Chalamila, achana na Cocobeach

Maswa Yetu

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2023
Posts
1,399
Reaction score
2,601
Mkuu wa mkoa wa Dares salaam Mh Albert Chalamila akiwa kwenye kikao cha ndani cha mkoa amesikika akilaani eneo la Cocobeach kuachwa wazi kwa ajili ya wananchi wote kutembelea bure kila wanapohitaji kufanya hivyo.

Chalamila amesema eneo la Cocobeach linahitaji uwekezaji mzito na wa kisasa.

Chalamila namkemea kutokana na wazo lake hilo kwa sababu hajatuambia kama hilo eneo likiwa la kulipia hao wananchi masikini wasio na hela ya kuingia Beach atawapeleka wapi.

Mh Chalamila ajue pia Tanzania ina eneo kubwa la bahari kwa ajili ya kujenga beach za kisasa anazozitaka hivyo siyo lazima ang'ang'anie kwenye eneo la wazi la Cocobeach.
 
muslim elites dont care about small people my friend, ndiyo maana wako hivyo, hiyo beach iko for public use tangia ukoloni, kila awamu ya uislamu ulijaribu kuipora coco beach ktk kwa wananchi na kugawia matajiri wachache, alianza raisi mwinyi akagawa kwa sea cliff ya wahindi/warabu, wakaja akina manji vivyo hivyo bahati nzuri awamu iliyofwatia ilizuia sasa wamerudi tena muslim na inaondoka hivyo na hakuna mtetezi …
 
muslims dont care about small people my friend, ndiyo maana wako hivyo, hiyo beach iko for public use tangia ukoloni, kila awamu wa uislamu ulijaribu kuipora coco beach ktk kwa wananchi na kugawia matajiri wachache, alianza raisi mwinyi akagawa kwa sea cliff kwa wahindi/warabu, wakaja akina manji vivyo hivyo bahati nzuri awamu iliyofwatia ilizuia sasa wamerudi tena muslim na inaondoka hivyo na hakuna mtetezi …
Inasikitisha sana
 
Mkuu wa mkoa wa Dares salaam Mh Albert Chalamila akiwa kwenye kikao cha ndani cha mkoa amesikika akilaani eneo la Cocobeach kuachwa wazi kwa ajili ya wananchi wote kutembelea bure kila wanapohitaji kufanya hivyo.

Chalamila amesema eneo la Cocobeach linahitaji uwekezaji mzito na wa kisasa.

Chalamila namkemea kutokana na wazo lake hilo kwa sababu hajatuambia kama hilo eneo likiwa la kulipia hao wananchi masikini wasio na hela ya kuingia Beach atawapeleka wapi.

Mh Chalamila ajue pia Tanzania ina eneo kubwa la bahari kwa ajili ya kujenga beach za kisasa anazozitaka hivyo siyo lazima ang'ang'anie kwenye eneo la wazi la Cocobeach.
Naunga mkono hoja.Nilikuwa Mombasa hivi karibuni.Nilibaini kuwa pamoja na nchi hiyo kuwa na sera za kibepari,lakini tangu enzi za Kenyatta fukwe zote zimeachwa kutumiwa bure na umma.
 
Kama kariakoo hakuna hata bustani uchwara ya kupumzika. Maeneo yote wameuza
Inasikitisha sana sijui wataalam na viongozi wetu wao wanatembelea nchi gani na kutoka na mfumo wa kwetu.
Yaani jiji la Dar hakuna buffer zone au misitu midogo kwa ajili ya kunyonya vumbi na kupoza joto.
Akili zetu zinawaza tu kwamba kila sehemu ni kujenga. Jiji lina eneo kubwa limeachwa kuwa squatters ila tayari walishakimbilia Mabwepande kuyachakata.
Huwa najiuliza sehemu za majeshi kwenye jiji la Dar zisingekwepo Jiji lingekuaje?
Huo ujinga nako imeshaanza Dodoma pia
 
Ule mbichwa wake unaakisi aina ya akili zake.

Chalamila is a comedian kila analofanya na kusema ni kwa ajili ya kuchekesha. Hana upeo wa kuchanganua jambo lolote.

Chalamila ni sawa na Mwijaku tu, kubwabwaja ovyo ili maisha yaende.
 
Inasikitisha sana sijui wataalam na viongozi wetu wao wanatembelea nchi gani na kutoka na mfumo wa kwetu.
Yaani jiji la Dar hakuna buffer zone au misitu midogo kwa ajili ya kunyonya vumbi na kupoza joto.
Akili zetu zinawaza tu kwamba kila sehemu ni kujenga. Jiji lina eneo kubwa limeachwa kuwa squatters ila tayari walishakimbilia Mabwepande kuyachakata.
Huwa najiuliza sehemu za majeshi kwenye jiji la Dar zisingekwepo Jiji lingekuaje?
Huo ujinga nako imeshaanza Dodoma pia
Njaa tumboni.
Muhindi akija na milioni 800, eneo la wazi watu wa ardhi wanauza na kubadilisha mchoro. Kariakoo unatembea kilomita mbili hukuti hata sehemu ya kukaa. Vifremu mwanzo mwisho. Pathetic
Moto ukianza ghorofa moja unaweza kuteketeza mtaa mzima
 
Ni muhimu kuwa na sehemu ya beach ambayo inatunzwa, kuangaliwa na kuhudumiwa vyema. Kuna thread humu jf inayoonyesha jinsi Serikali ilivyoshindwa kutunza kituo cha mabasi -Msamvu, Morogoro, Ili wakazi wa dar tuweze ku enjoy mandhari nzuri ya coco lazima uwekezaji ufanyike ktk hali ambayo Mtanzani wa hali ya chini ataimudu / PPP Inahitajika sanaCoco.
,ni ukweli mchungu lkn watanzania lazima tujue jinsi ya kuishi nao ""HAKUNA CHA BURE"" ukiona kuna kitu unaambiwa bure ujue kina gharama, wee chunguza walimu wengi wa gvnt secondary school watoto wao wanawapeleka private school, why ??
 
Back
Top Bottom