Nakimbia ndoa-Naogopa kuua

Nakimbia ndoa-Naogopa kuua

abbas-hassan

Member
Joined
Nov 21, 2013
Posts
11
Reaction score
15
Wana jf....mi nimeoa na nina watoto wa3. Huyu binti nilimtoa kwao nikawaahidi wazazi wake kua nitamsomesha mpaka elimu yeyote. Nikafanya hivyo mpaka sasa yupo na kazi. Ila kwa bahati mbaya mimi karibu mwaka sasa sina kazi ila pesa za kula hazinikosi.


Huyu binti wakati naenda kumtambulisha kwetu alinifanya nikosane na ndugu zangu wote. Lakin kwa kua nampenda nilisimamia show mpaka wakanielewa. Maisha yetu mimi na yeye yamekua ya magomvi sana kwa takriban miaka 7 sasa. Hakuna tulichofanya cha mafanikio mpaka muda huu.


Magomvi yetu mengi yamekua ni tabia za unafki,uzinzi,uongo,dharau,majibu mabaya ya kutia hasira na kutojali wala kumthamini mtu. Ni mzuri sana wa kuomba msamaha ambapo baada ya kuomba msamaha hurudia kitu kile kile alichofanya baada ya muda mfupi.


Sasa maisha yamebadilika sana....baada ya yeye kua na kibiashara ambacho kinamuingizia pesa licha ya anazopata kwenye mshahara. Unachomweleza hakusikii hata kidogo. Anajifanya yeye ndio yeye...misheni town...kugawa namba ovyo kwa wanamme...kua na namba tofautitofauti ambazo hata mimi sizijui ambazo huzitumia kuwasiliana na wanamme zake wa nje.



Kiukweli mpaka time hii....nimewahi kumfuma akicheat zaidi ya mara 7. Akiwasiliana na wanamme wapya au ma X zake. Ni mtu wa iringa. Anakiburi sana na dharau ya hali ya juu. Hajali kama tunawatoto au la.



Hutoa majibu ambayo hunifanya nipate hasira sana na ikafikia mahala nikampiga kama mara 3 ivi. Na jana ilikua mara ya nne. So nimefikiria sana na nimeona ngoja nikimbie mji nimwachie kila kitu niende ninakokujua.



Kwa hasira nilizokua nazo jana....nimemwambia...hata akisikia nimekufa...asije kuniona...wala mimi sitakuja kumuona. Koz kama ni kunipotezea muda kanipotezea muda mwingi sana na gharama nyingi sana. Lakin zaidi ya yote ni kuhusu watoto wangu ambao sikutaka kabisa waishi ktk malezi mabovu kwasababu yake.




Nawashauri wanawake wenye tabia hizi waache. Malipo ni hapa hapa. Mtu akikutoa ujinga usimdharau.
 
Mmmmmmmmh! *Covers face from shame!*

Huyo dawa yake wala si kukibia na kumuachia jiji ajitanue! Dawa yake ndogo sanaaa! We tafuta nyumba ndogo hapo hapo jirani utiize ule usemi ULIKIONA CHA NINI, WENZIO WASEMA WATAKIPATA LINI? Atanyooka kama nguo mbichi iliyopigwa pasi!

I realy do feel mercy for the kids! Wataisoma namba, chezea baba wa kambo na mama wa kambo!
 
abbas-hassan yaani ulivyoongea tu hapo, ninakufahamu, ulimsomesha chuo kikuu, unakaa jetrumo dsm, yeye anafanya kazi afisa mambo ya elimu, anasafiri sana mikoani, wewe ulikuwa unafanya kazi zamani katika ubalozi fulani hivi hapa dsm, uliachishwa kazi, na una kisukari, dada ana hela za kutosha tu na mmejenga nyumba yenu nzuri sana huko jet. yeye mtu wa iringa, wewe ni mngoni. hadi nakuonea huruma.

kumfumania mwanamke mara 7 yahitaji ujasiri. mwombe Mungu usiingie majaribuni ukaja kujutia maisha yako yaliyobaki, usichukue uamuzi mbaya kwani utakugarimu.
 
Last edited by a moderator:
pole sana mkuu hebu jaribu kutulia kama wiki moja kwanza jaziba iishe,tafakari kwa kina juu ya hatima ya watoto wako na wewe mwenyewe juu ya kazi zako....Mungu akusaidie kufanya maamuzi sahii amen.
 
Duh..hadi nimejiskia vibaya,mbona watu wanakosa utu?kisa anapesa ndio amekuona huna thamani?kweli binadamu hawaaminiki,hajali kwamba mna watoto,ni mbinafsi hana mapenzi na wewe.....duh pole sana kaka life is too short ohhh(in naija's voice).well tafuta mke wa pili akili imkae sawa.she doesnt deserve u a bit.
 
pole sana kaka. ngoja nitulie kisha nije nirudi na ushauri. Ila wewe ni kama nakufahamu vile...ngoja kwanza....
 
Duuuh Pole sana kwakweli eee Mungu niepushe na Ndoa isiyokua na amani, upendo, uaminifu na Heshima. Muombe Mungu akufanyie mlango wa kutokea.
 
abbas-hassan Ulifanya nini mpaka ukawa uko nje ya kazi abbas-hassan? kama kuna kaufisadi kalichopelekea wewe kuondolewa kazini matunda ya huo ufisadi ulitumia na familia yako au na rafiki zako?
 
Last edited by a moderator:
abbas-hassan Pole sana mkuu,wanawake wakati mwingine huwa wanakuwa wapumbav sana,hasa wakijiona wako juu na kuwa na kipato,tafadhali tumia akili sana ili watoto wasipate shida,kama na uwezo wa kuitunza familia wewe kuondoka is the best way,but usiende nje ya nchi wala mikoani,kuwa mjini humo humo na uwe unaivist familia yako kama kawaida.anza maisha mapya
 
Last edited by a moderator:
Ndoa hizi? Mmh!
Aisee kama hajawahi kukubamba unamcheat, i hate to say this lakini fuata ushauri wa mdogo wangu lara 1. Buy time na hela ikirudi usome upepo. Dawa ya jeuri ni kiburi.
 
Last edited by a moderator:
Wanawake mwalimu wao alishakufa siku nyingi anayewaongoza sasa hivi ni kipofu..Yaani umezaa watoto watatu bado unakimbizana na zakari za Dunia unadhani utazimaliza???
Siku zote nasema mwanamke ni kiumbe kisichokuwa na shukrani hata ukifanyie nini ni chepesi kusahau..nina mifano hai zaidi ya mia ya matendo kama hayo.
 
Pole sana kaka huyo mwanamke amekuwa katili sio kwako tu hata kwa watoto ila mimi nakushauri wewe tulia kimya usimfuatilie kwa chochote kaa kimya angalia wanao fanya kama vile mama yao hayupo, chukua jukumu la ubaba na umama kunusuru watoto kwani hawana hatia, pia usichukue maamuzi ya kuanza kuzunguka na wanawake tofauti kwani magonjwa ni mengi sana usijewaacha watoto mapema na laa ukishindwa kabisa kukaa bila kuwa na mwanamke chukua jukumu la kuwa na mwanamke mmoja walau akupunguzie shida zako ndogondogo, pia kukaa kimya bila kumfuatilia ni fimbo tosha kwake kwani huyo mwanamke anajua unampenda sana na hufurukuti kwake ndio maana anafanya vituko. Ebu tulia kaa kimya bila kumjali kwa lolote afanyalo uone atabadilika tuuu
 
Pole jamani.Nakuonea huruma ila ndo hivyo.jamani wanadamu heshimuni waume / wake zenu wa ndoa maisha yapo wapi siku hizi?

Mie toka nifiwe na mme wangu kipenzi kweli najuta sana kwa makosa niliyowahi kumfanyia mme wangu kipindi cha uhai wake.inaumiza sana kugombana ndani ya ndoa zenu acheni tafute amani ya ndoa zenu.

Leo mpo Hai siku mmoja wenu akitangulia mbele ya haki wewe unae bako utaumia sana nafsi yako kama haukuishi na amani na mme.mke wako wa ndoa.
 
Pole sana Mkuu,

Nimejifunza kwako kusikiliza na kuchunguza. Sikulaumu mkuu, ila ni somo kwetu wengine juu ya kuchunguza kwa tafakuri pana yale yasemwayo na watu wanaotupinga. Sio rahisi ndugu/jamaa hao wote wakawa hawakuona kitu hadi kukosana kiasi hiko, kuna kitu waliona ila wewe ndio ukawa umetia kiburi. Ushauri wa watu una nafasi kubwa sana ila maamuzi ni na mtu mwenyewe.

Guys tusipumbazwe na upendo na hisia tukawapuuza wengine.



Bahati mbaya hukuyatambua kwa wakati uliofaa.
 
Nyie watu wa ule mkoa inaonekana mnamiliki bastola sana. Sasa mkuu uliinunua ya kulindia wale vitimoto pale shamba afu unamwazima huyu tena!!!

Duh shem Kaizer, bistola yako iko karibu tumuazime mshkaji?

Yani kuna mdau hapa jana alini-pm nimemuazima!!!!
 
Watu wa Iringa ndivyo walivyo, kuna dada mmoja nafanya nae kazi ameolewa na anaishi na Mume lakini cha ajabu amejengewa nyumba nyumbani kwao na mume wa mtu tena hata wazazi wake wanajua.Pia anagawa uroda kwa vijana hapa ofisini kama vile ana pepo.Nilishamuita nikamuonya lakini hata hakunisikia maana naona ndiyo maisha aliyochagua.Pia kuna dada mmoja tulisoma nae chuo alikuwa anagawa uroda kwa vijana licha ya kuwa alikuwa ameolewa na Auditor wa wizara fulani na pia alikuwa anapata boom.Tatizo halikuwa fedha ila pepo la ngono.

Muache tafuta mke mwingine usichezee kaa la moto mwishowe litakuunguza.
 
Mmmmmmmmh! *Covers face from shame!*

Huyo dawa yake wala si kukibia na kumuachia jiji ajitanue! Dawa yake ndogo sanaaa! We tafuta nyumba ndogo hapo hapo jirani utiize ule usemi ULIKIONA CHA NINI, WENZIO WASEMA WATAKIPATA LINI? Atanyooka kama nguo mbichi iliyopigwa pasi!

I realy do feel mercy for the kids! Wataisoma namba, chezea baba wa kambo na mama wa kambo!
lara 1 unaufahamu wimbo mmoja sikumbuki jina la kwaya ila wanasema

........watoto wa nyumba zote njooni tuungane
tuwalilie wazazi chozi la damu...........
haki ya malezi bora tumepoteza
urithi wa maadili tumepotezaa
ooh duniaaa dunia ooh tumekusea nini

beti ya 3 anasema

..............familia moja baba na mama watano...........

its a sad thing.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom