Hii ameandika mwana JF mwenzetu
de'levis
============================== ========
Nilikuwa sina nia ya kuandika sana humu lakini baada ya kusoma comment yako nimelazimika kusema kitu...jambo lolote unaloambiwa , kuliona au kulisikia ni lazima ushughulishe akili kufikili ili ujiridhishe kama ni la kweli au la vinginevyo utakuwa unakubaliana na jambo ambalo si la kweli...jaribuni kuipa nafasi akili yenu kufikiri.... bahati mbaya sana katika siku za hivi karibuni imeonekana watanzania wengi sana wana tatizo la kutoipa akili nafasi ya kufanya maamuzi na kung'amua na mmoja wao ni Pasco....wachache wanaipa akili nafasi ya kufikiri.
Kuna matukio mengi sana na mengine wengi hamuyafahamu ambayo yanalenga kuichafua image ya taifa na kwa kuwa matumizi ya technolojia nchini yamekuwa yakikuwa kwa kasi hasa matumizi ya simu na intanet na kwa kuwa techolojia inakuwa kwa kasi na hivyo wengi wanashindwa kwenda sambamba na ukuaji wake na hivyo wanajikuta wanakubaliana na kila kitu wanachokiona ama kusikia..
katika mkanda huo ambao wewe pasco unauita ni ''bonafide and genuine'' nimefanikiwa kuuona jana mchana na mimi na wenzangu tumekaa na kuupitia kwa makini kabisa na kwa njia za kisasa zilizotusaidia kujua uhalisia wake... mkanda huo ni fake na tayari taarifa imeshatolewa....hata wewe pasco ukijipa mda wa kukaa na kuipa akili yako nafasi utagundua kuwa mkanda ule ni fake vinginevyo utakuwa unasumbuliwa na '' invincible ignorance''
Chini hapa nitakusaidia kidogo ili walau upate picha ya kuwa mkanda ule ni fake...
00:01 ------Sauti inaanza kwa kutamka MIKE na kisha kuuliza HAPO? maana yake watu hawa wanajiandaa kuanza kujirekodi na wakati wa nafanya editing waliyaacha maneno hayo
00:15 ..........sauti ya mtu wa pili inasikika ikisema TUTANOTE TENA HAPO ...inaelekea watu hawa kuna mahali walikosea na kusema watarudia mahali hapo...
00:28 .......Binti anaonekana akija dirishani na kisha anaondoka baada ya maongezi mafupi na mwenzake aliyoko upande wa pili wa dirisha.
01:45......Sauti ya mtu mwingine ambaye baadae alikuja kutambulika kama RICH anasikika akiwasalimia lakini aliyesalimiwa(lwakatare) kulingana na picha na mdomo wake inaonekana si yeye aliyeitikia marahaba..kuthibitisha hilo mara baada ya salamu msalimiwa hakugeuka kumwangalia anayesalimia ila aliendelea na shughuli zake na papo hapo kijana anayeonekana na kupewa maelezo mara moja anaanza mazungumzo na kijana (rich) aliyekuwa anasalimia na ndipo anamwita jina hilo rich na wanapeana pole za matatizo na habari za sikukuu nk. katika mazungumzo mtu anayeonkena kwenye clip(lwakatare) bado haeguki kumwangalia huyo rich badala yake anaendela kutoa maelezo namna ya kudhuru watu.... hapa kuna abrakadara katika clip hii......
03: 15......wakati mazunguzo na melekezo toka kwenye clip ya lwakatare yakiendelea kwa mbali anasikika binti anayemkaribisha mtu mwingine na pia anasikika akisema napanda maua na anamalizia na neno karibu ingia ndani..( ili kumsikia binti umakini unahitajika kidogo)
03:20.....inasikika sauti mtu akikoroga chai kwenye meza yalipokuwa yanafanyika mazungumzo na anarudisha kijiko kwa kugonga meza lakini picha inayoonekana haimuoneshi mtu huyo na wala hakuna dalili za kuwa kwenye meza ya lwakatare kulikuwa na kikombe cha chai na kuwa chai ile ilikorogewa pale.. ...na pia kwa kufatilia kwa makini mtu anayekoroga chai si yule aliyekuwa anapewa maelekezo.... kitu kingine ni kwamba clip nzima quality ya sauti ya lwakatare haisikiki sawa sawa kama sauti ya mtu wa pili (kijana anayepewa maelekezo) ...
05:35 .....sauti inasikika ikitamka UNAELEWA LAKINI? lakini ukiangalia kwa makini mdomo wa lwakatare hakutamka neno hilo badala yake mdomo unaonyesha ametamka UMELIONA HILI? ni sawa na pale alipokuwa akisalimiwa na RICH hakutamka neno marahaba na badala yake neno alilotamka kulingana na mdomo ulivyoonekana alitamka YOTE MUHIMU na ndio maan hakugeuka kumwangalia yule aliyekuwa anasalimia kama ilivyoelezwa hapo juu..
05:57... Sauti inasikika ikitamka kuwa kama tulivyofanya hii ya morogoro kisha kwenda igunga swali la kujiuliza hapa ni mauaji yapi yalitangulia? Ya morogoro au igunga?..... bado ushahidi unaonyesha video hii ni ya kupika..
07:36.....Sauti inasikika ikisema dawa aina mbali mbali vidonge, unga ama liquid form fanya utafiti ujue zinapatikana wapi na ni bei gani; ni rahisi mno kama tulivyofanya utafiti wa mgongolwa tukapata ile kitu hapa pia kunachanganya inawezekanaje kijana anapewa jukumu la kutafuta bei na upatikanaji wa madawa wakati huo huo akikumbushwa namna walivyopata ile kitu kwa mgongolwa ambapo kijana alishiriki ...maana yake kijana anajua bei na wapi yanapatikana...( who is mgongolwa by the way?)
15:59 ...sauti inasika ikisema unamuweka kwenye dilemma hajui adui ni nani yaani anakuja hapa anakukuta wewe LUDOVICK ndiye unamfatilia...huyu Ludovick ni nani?( some dots needs to be collected and connected here ) yawezekana ni mmoja wa vijana waliokuwa wanajirekodi na hili ni jina lake halisi na wametajana pasi kujua au ni code name?..
17:10 kijana anayepewa maelekezo (Ludovick) anauliza kwa hiyo kama kila kitu kitaenda well inakwenda mpaka lini? lakini katika kujibu clip inayomuonyesha lwakatarea akijibu swali hilo akisema Bahati mbaya umekuja na majibu yasiyojitosheleza ....katika majibu haya kuna mkanganyiko mkubwa maana hakuna uhusiano wa swali lililoulizwa na jibu lililotolewa....tangu dakika ya 15 ya clip hii maelezo ya sauti zinazosikika hayana mpangilio wa manaa... mengi yalilenga kufuatisha ishara na vitendo vya lwakatare alivyokuwa akiongea na ukitizama kwa makini hakuna uhusiano kati ya maneno yenyewe na mdomo wa lwakatare.............
19:20...Lwakatare anaonekana akiongea kwa mdomo na vitendo(kuchezesha mikono) huku kichwa chake na macho vikielekea kwa kijana(ludovick) aliyesimama/ kukaa mbele yake ..mara gafla kitu kinadondoka chini na kijana anainama kukiokota lakini bado lwakatare akiongea kichwa na macho vikiangalia juu alipo kijana na kijana anaitikia mmmh, mmmh mara gafla clip inakatwa na kuishia hapo... hapa pia kunamkanganyiko mkubwa... na hakuna uhusiano wowote wa maneno yale na picha inayoonekana na tukio la kudondoka kitu chini..... binafsi naamini clip ingeendelea kuanzia hapo sura ya mtu wa pili ingeonekana hasa mara baada ya kuokota kitu kilichodondoka na ndio maana clip imeishia hapo.......
Pasco unaweza kuishabikia clip hii kama bonafide genuine kama na wewe ni mmoja wa washiriki wake au basi ni ushabiki wa kipuuzi ...anyway hata hivyo taarifa juu ya uhalilisia wa clip hii imetolewa....