Nakala ya asili ya Goetia

Nakala ya asili ya Goetia

Watu wengi huwa wanachanganya elim-Dunia ya kiarab (Arabian black-mass) na QURAN kama ambavyo wanaweza kuchanganya hii Western black mass yako na Ukristo! Utasikia wakina Gwajima wakihusisha Uislam na majini kuwadanganya watu kuwa huo ndo uislam wenyewe! 😅
WACHAWI PEKEE HAPA TUNAWEZAMEGEANA MAWILI'MATATU Mshana Jr !
WACHAWI PEKEE HAPA TUNAWEZAMEGEANA😀😀😀 MAWILI'MATATU
 
Hapa tuna pepo aitwaye Lucifuge Rofocale kutoka kwenye nakala iliyoskaniwa ya toleo la asili la kitabu cha Red Dragon/Grand Grimoire. Kikirekodiwa mnamo mwaka 1750, kitabu cha Grand Grimoire ni mwongozo wa maelekezo ya jinsi ya kuwaita mapepo 27 tofauti, ambapo Lucifuge Rofocale ni mmojawapo na ndiye mlengwa mkuu wa kitabu hiki.
Grand Grimoire ni kitabu halisi na chenye nguvu, ingawa hakikuandikwa na "shetani mwenyewe" wala "hakijafungiwa huko Vatican." Kitabu hiki chenyewe ni sehemu ya mapokeo ya mamia ya vitabu vingine vinavyoaminika kuwa viliandikwa na Sulemani, au vinahusishwa na uchawi wake kwa namna moja au nyingine. Ndani ya Grand Grimoire, kuna mazungumzo kati ya pepo huyo na Sulemani yanayoenda hivi...


 
KWA PEPOMWIKO (ROHO)
Kama ungejitokeza nilipokuita mara ya kwanza, nisingekuwa na haja ya kukupiga, lakini usipokubaliana na yale ninayokwenda kukuomba, nitakutesa milele. SULEMANI
JIBU LA PEPOMWIKO (ROHO)
Usinitumbuize hapa na usinitese tena: Niambie mara moja unachoniomba.
LUCIFUGE ROFOCALE
OMBI KWA PEPOMWIKO (ROHO)
Nakuomba uje uzungumze nami mara mbili kila siku ya juma, wakati wa usiku, mimi au wale watakaowasilisha kitabu changu, ambacho utakikubali na kukisaini, kwa hiari na kwa wakati utakaochagua mwenyewe ambao unaweza kukufaa, ikiwa hutaziidhinisha hizi zilizowekwa alama hapa chini:
Kama ifuatavyo:
Jumatatu, saa 3 kamili usiku na saa 6 kamili usiku (saa sita ya usiku).
Jumanne, saa 4 kamili usiku na saa 7 kamili usiku.
Jumatano, saa 5 kamili usiku na saa 8 kamili usiku.
Alhamisi, saa 2 kamili usiku na saa 4 kamili usiku.
Ijumaa, saa 1 kamili usiku na saa 6 kamili usiku (saa sita ya usiku).
Jumamosi, saa 3 kamili usiku na saa 5 kamili usiku.



FB_IMG_1704452556590.jpg
 
1. Zaidi ya hayo, nakuamuru uniletee hazina kubwa zaidi iliyo karibu na hapa, nakuahidi kama thawabu yako kipande cha kwanza cha dhahabu au fedha nitakachogusa siku ya kwanza ya kila mwezi. Hiki ndicho ninachokitaka kutoka kwako. SULEMANI
JIBU LA PEPPO (ROHO)
Siwezi kukubali yale unayodai kutoka kwangu chini ya masharti haya wala mengine yoyote, isipokuwa ujitoe kwangu baada ya miaka hamsini, nifanye na mwili wako na roho yako upendavyo. LUCIFUGE ROFOCALE
MPELEKEE PEPPO (ROHO) MANENO HAYA
Nitakupiga wewe na kizazi chako chote, kwa nguvu ya Adonai mkuu, ikiwa hutatimiza matakwa yangu yote. SULEMANI
TAHADHARI: Sasa tumbukiza ncha ya Fimbo ya Mlipuko (Blasting Rod) ndani ya moto na urudie Mwaliko mkuu wa Ufunguo (Invocation of the Key), hadi peppo atakapojisalimisha kwa matamanio yako.
JIBU NA MAZUNGUMZO YA PEPPO (ROHO)
Usizidi kunipiga, nakuahidi kufanya yote unayotaka, kwa muda wa saa mbili kila usiku wa juma. Yaani:
Siku ya Jumatatu saa 4 usiku na saa 6 usiku, siku ya Jumanne saa 5 usiku na saa 7 usiku, siku ya Jumatano saa 6 usiku na saa 8 usiku, siku ya Alhamisi saa 2 usiku na saa 5 usiku, siku ya Ijumaa saa 3 usiku na saa 6 usiku, siku ya Jumamosi saa 4 usiku na saa 7 usiku
 
Pia nakubali kitabu chako, na ninakupa Sahihi yangu ya kweli kwenye Ngozi, ambayo utaiweka mwishoni, ili ikusaidie katika hitaji lako, nitajinyenyekeza pia na kutokea mbele yako kila wakati utakapotaja jina langu au unapofungua kitabu hiki, ukiwa umetakasika, na utakapokuwa na Fimbo kuu ya Maangamizi, na ukiwa umejenga Duara kuu la Kabbala, na utakapolitaja Neno ROFOCALE; ninaahidi kutokea katika umbo la kupendeza kwa wale wanaomiliki kitabu hiki, ambapo kuna sahihi yangu ya kweli, mradi tu wananiita wakiwa katika hali nzuri na kwa mujibu wa sheria, mara ya kwanza wanaponihitaji.Ninaahidi pia kukukabidhi hazina uliyoniomba, mradi tu uweke siri hii daima, uwe na hisani kwa masikini, na unipe sarafu moja ya dhahabu au fedha katika siku ya kwanza ya kila mwezi, ukikosa kufanya hivi, utakuwa wangu milele. LUCIFUGE ROFOCALE, ImekubaliwaJIBU KWA JINI (ROHO)Ninakubali masharti yako. SOLOMONZingatio: Kuna uchawi mwingi katika maneno haya ikiwa unajua jinsi ya kusoma kati ya mistari.
 
Back
Top Bottom