Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,421
- 40,409
Nimekuwa kwenye mahusiano na michepuko kwa nyakati tofauti, na wote wanajua nina familia, ila kutokana na mazingira ya kuwajali na kuwa mchangamfu, wakajikuta wananogewa, na wengine mpaka wakaamua kunizalia.
Kwa wale walionizalia, nikawa nawapa nafasi ya mbali kidogo ili wasije kujipandisha cheo na kuwa mke, au kufanya mapinduzi kwenye ndoa iliyopo.
Kwa sasa nipo kwenye harakati za kuachana na michepuko, ili niweze kutulia na familia yangu, pamoja na kulea uzao wangu uliopatikana, bila kufanya mapenzi nje ya ndoa; kwa sababu uzee umeshanianza, na ndevu zimeshakuwa na mvi; wanasema simba mzee akizeeka, hata uwezo wa kuwinda hupungua.
Bahati nzuri, michepuko miwili imekubali matokeo kishingo upande, lakini ndio hivyo, kila kitu kina mwanzo na mwisho pia.
Waliobaki wawili, bado kukubali matokeo; kuna mmoja atajifungua hivi karibuni, ananiuliza ''utaniachaje mwanamke mzuri kama mimi, hujui mimi ni mzuri?'' Najaribu kumwambia nataka, nipate muda mzuri kwa ajili ya kuwekeza kwa hao wanaokuja.
Mwingine, chura matata, ni mke wa mtu; haelewi kabisa, na hataki kusikia mapendekezo yangu.
Nimebaki, kuwafariji tutaendelea na mahusiano; ila kiuhalisia akili yangu inaniambia sasa ni muda wa kutulia na familia yangu, kwa sababu umri unanitupa mkono.
Kweli umri mkubwa ni kuwa na busara.
Najuta sana kuwakoleza kwenye mahusiano; kwa sasa inaniwia vigumu kuwaacha.
Kwa wale walionizalia, nikawa nawapa nafasi ya mbali kidogo ili wasije kujipandisha cheo na kuwa mke, au kufanya mapinduzi kwenye ndoa iliyopo.
Kwa sasa nipo kwenye harakati za kuachana na michepuko, ili niweze kutulia na familia yangu, pamoja na kulea uzao wangu uliopatikana, bila kufanya mapenzi nje ya ndoa; kwa sababu uzee umeshanianza, na ndevu zimeshakuwa na mvi; wanasema simba mzee akizeeka, hata uwezo wa kuwinda hupungua.
Bahati nzuri, michepuko miwili imekubali matokeo kishingo upande, lakini ndio hivyo, kila kitu kina mwanzo na mwisho pia.
Waliobaki wawili, bado kukubali matokeo; kuna mmoja atajifungua hivi karibuni, ananiuliza ''utaniachaje mwanamke mzuri kama mimi, hujui mimi ni mzuri?'' Najaribu kumwambia nataka, nipate muda mzuri kwa ajili ya kuwekeza kwa hao wanaokuja.
Mwingine, chura matata, ni mke wa mtu; haelewi kabisa, na hataki kusikia mapendekezo yangu.
Nimebaki, kuwafariji tutaendelea na mahusiano; ila kiuhalisia akili yangu inaniambia sasa ni muda wa kutulia na familia yangu, kwa sababu umri unanitupa mkono.
Kweli umri mkubwa ni kuwa na busara.
Najuta sana kuwakoleza kwenye mahusiano; kwa sasa inaniwia vigumu kuwaacha.