ndugu KICHUMVI, mimi sioi tatizo wala kitu cha kukusababisha uwaze kiasi hicho, katika mahusiano hasa kwa mtu ambaye bado hajaoa ni mambo ya kawaida sana kutokea, maana wakati huo huwa na wakati mgumu sana kuushinda moyo na kuamua kwa majaribu kama hayo. Hali hiii pia hutokea hata kwa mtu aliyeoa, mara kadhaa wanandoa pia huingiwa na majaribu kama haya, hasa pale wenzi wao wanapokuwa mbali nao.cha msingi chukua uamuzi wa busara, ambao ni kufuata moyo unapopenda na siyo kulazimishwa na mazingira, kumbuka hakuna kitu kibaya katika maisha kama kuoa mtu kwa kigezo cha mazingira kama mali, pesa, madaraka ama kumuonea huruma kwa kujifanya kumsaidia, ndoa khaijengwi kwa huruma bali kwa upendo unaotoka rohoni. Uzoefu unaonyesha kwamba, watu walioooana kwa kigezo cha mazingira kama nilivyoeleza hapo juuu ndoa zao hazidumu, na kama zikienda wa muda fulani basi ni kero sana upande mmoja wa ndoa. KUMBUKA, MARRIAGE IS TOO WAY TRAFICK, YOU GIVE LOVE AND YOU RECEIVE IN THE SAME WAY (at least in some amount). chukua hatua za kuwa mkali na kuachana na huyo wa pili haraka sana ili uende moyo unakopenda.
Heshima mbele