ulaya12
JF-Expert Member
- Nov 16, 2017
- 834
- 898
Huwa ninajiuliza hadi nakosa jibu labda wenzangu mtanisaidia,wazazi wangu ndiyo walifanya mipango hadi mimi wamenizaa wakati huo mimi wala hawakunishirikisha na nilipokuwa mtoto walinijali sana kila kitu walikuwa wananihudumia hadi nimeanza kupatapata akili walikuwa wananijali sana namimi nikayaona maisha ni mazuri sana,lakini nashangaa miaka ilivyokuwa inasonga nao wamenitelekeza sipati huduma kama zamani wanasema nijitegemee yaani maisha yamekuwa magumu kupita kiasi naona hapa wameniingiza mkenge kwanini wanifanyie hivi wakati mimi sikuwaomba wanilete huku duniani wangeniacha hukohuko walikonitoa hapa hawajanitendea haki kabisa" nawasilisha