Najuta kupiga kura 2015, sitokaa nipige kura tena

Marire

JF-Expert Member
May 1, 2012
12,326
5,267
Wakuu
Huu uchaguzi umeniacha na majonzi sana!!!
Nawashangaa wanaoshabikia vyama vyao kushinda maana huku mtaani tumeshuhudia mabox ya kura na karatasi za kura za wizi zikizagaa kama njungu na tume haijatoa tamko lolote

Nchi imeingia kwenye gharama kubwa kwa ajili ya uchaguzi,chama cha siasa kama ccm wametumia gharama kubwa kwenye kampeni na kuwalipa wasanii ili hali mwisho wa siku kumbe wanakuja kuiba kura na kutoa matokeo ya uongo,kulikuwa na haja gani ya uchaguzi??

Jeshi la police wameagiziwa magari brand new 777 napiga hesabu ukigawa kwa kwa majimbo 264 kila jimbo linapata gari 2 na yatabaki cha kushangaza kuna jimbo halina ambulance hata moja wala kituo cha afya wala maji safi na salama!!

Kwa binafisi yangu sioni haja ya kuwa na vyama vya siasa wala kuwepo kwa kampeni maana zinagharimu pesa nyingi na maisha ya watu kama jimbo la nyamagana wameuana vijana wanne kwenye hizi kampeni...
Kwanini tusiwe na chama kimoja kama china???

Kama hali hii itaendelea sioni sababu ya kuwa na uchaguzi
Tuanze na hii quotation kwanza afu baadaye utajua namaanisha nini.

?I have never voted in my life... I have always known and understood that the idiots are in a majority so it's certain they will win.?
― Louis-Ferdinand Celine

TASFIRI

Sijawahi kupiga kura maishani mwangu....nimekuwa na uelewa kuwa walio wengi ni wapumbavu na ni lazima wapelekee ushindi
―Louis -Ferdinand Celine

Wapumbavu ni pamoja na wanaobadilisha matokeo ya kweli kuwa uwongo na ya uwongo kuwa kweli sitakuja kupiga kura Kama Tume itaendelea kuwa hii ya Lubuva hutakuja kamwe kuniona napanga foleni Kama katiba itaendelea kuwa hii hii ya Chenge.

Nipige kura ili iweje wakati badara ya kuokoa vuguvugu linarohatarisha uwepo wa Tanzania kule Zanzibar mnatuletea maigizo ya ziara za kushitkiza huu si mda wa kudunduliza Iman ya watanzania kwa serikari kwa ubadhilifu uliofanyika kipindi uchaguzi kwa kufanya ziara za kushtukiza?

Mh. Rais dk John P Magufuli ameanza kazi kwa mtindo wa ziara za kushitukiza ili kujionea ufanisi wa sekta mbalimbali hapa nchini .Mimi binafsi napongeza hili lakin ukiliangalia kwa undani si kweli kwamba Magufuli hajui kuwa Muhimbili wagonjwa wanalala chini, Ntashangaa Sana ukiniambia kwamba Magufuli alikuwa Hana taarifa kuwa Muhimbili mashine za kupigia picha ndan ya mwili( medical imaging) kama magnetic resonance imaging (MRI) ni mbovu?

Kiukweli ziara hizi za kushtukiza zina lengo la kurudisha Iman na Upendo kwa wananchi kwa serikari hasa baada ya uchaguzi mkuu uliomalizika October kujaa na mizengwe na utapeli wa hali ya juu (Racketeering of the highest order) hali iliyopekea siku ya kuapishwa raisi( inauguration) nchi kupoa Kama imemwagiwa uji.

Eti wewe Unadhan raisi alikuwa hajui kuwa muhimbili wagonjwa wanalala chin au muhimbili hakuna machine za kupigia picha ndani ya miili ya binadamu(medical imaging) ziara gani za kushtukiza wakat utendaji unafahamika.

Hembu tuache mazingaombwe Rais aliyemaliza mda wake yeye aliona suruhisho ni kupeleka magari ya kivita ili kutisha wanzanzibar na ww Mh unazani ziara za kushtukiza ndo zitaookoa muungano?

Siji kupiga kura Kama raisi wangu badara ya kuinusuru Zanzibar ambao ndo msingi wa Tanzania anaendelea kushitukiza sehemu ambazo utendaji wake unajulikana hembu tujiulize wewe umenunua maembe ukayaweka kwenye friji afu kesho uishitukize friji ili uone Kama maembe yamebadilika kuwa machungwa hahahhahaha tusitaniane ni dhahiri yatabaki maembe labda ukute yameoza ila ukitarajia kukuta machungwa ni dhahiri unahitaji daktari wa magonjwa ya akiri.

Kuna haja gani ya kupiga kura Kama Tibaijuka na Chenge wanarudi kuwa watetezi wetu bungeni nchi yangu Tanzania bana eti tunatetewa na kuwakilishwa na wezi.

Neno Tanzania lina Zanzibar ndani yake ni lazima tuiokoe Tanzania kwa kuinusuru Zanzibar kwanza.Hayo maigizo ya kufuta safari ya nini au hizo fedha mnataka mzihamishie kwenye uchaguzi mwingine aliousema Jecha au mnataka hizo fedha walipwe ma IT waliobobea kwa kuongeza kura ili yule mnayemtaka Zanzibar ashinde.

Labda kwa mbari ntaanza kujifikiria kupiga kura Kama hizi ziara za kimazingaombwe zitafanyika NEC na ZEC yani raisi ashtukize ZEC afu amuulize Jecha "aliyekwambia ufute matokeo wakati katiba haikuruhusu nani??" au ashitukize NEC afu amuulize Lubuva "aliyekwambia unitangaze Kama raisi wa Tanzania nani wakati kura za Zanzibar zilikuwa batili"

Pengine huenda nikabadirisha dhamira Kama Rasimu Ya warioba itasimamiwa mpaka ipite.

Au naweza nikashawishika kupiga kura Kama maneno aliyosema Nnape BBC kuhusu mahamaka ya mafisadi yawe ya uongo eti hatukuelewa waliposema mahakama ya mafisadi

Je na wewe hutakuja kupiga kura Kama Mimi au utapiga?
Sababu zipi zinazokupeleka uwe na maamuzi hayo je zinafanana na zangu au Una zako ni zipi hizo?
(Black days my country is crying����)

KARIBU
attachment.php
 
Nami nimeapa kwa mizimu ya kwetu yote, siku zote nitakazokuwa Dunian hapa sitapiga KURA mpk ccm ikiwa imeondoka madarakani, kinyume chake acheni wajinga wachache waendelee kupiga kura. Mimi basi.
Sasa kuapa kwako kunatusaidia nini? Hayo ni maamuzi yako binafsi huna haja ya kutuambia. Those are personal issues dont waste our time plse
 
acha upotoshaji ww, watu kama nyie ndo hatari sana, ukishindwa kubali kushindwa acha visingizio na kupotosha inakusaidia nn?
 
Inasikitisha sana, ukweli kinachotokea mwaka huu unaweza kukilingalinisha na mwaka ule ambao mitihani ya form four ilivuja. Ikatapakaa kila mahali. Mwaka huu hayo mabox na nyaraka za tume ni kama zilichapishwa Manzese au Kariakoo na hazikuwa na mwagalizi. Kinachoonekana dhahiri ni kuwa nyaraka hizo ziligawiwa kwa Chama tawala kabla ya uchaguzi na kuanza kufanyiwa kazi. Inashangaza sana nyaraka hizo kukutwa kwenye nyumba au magari ya watu binafsi badala kukutwa zikiwa mikononi mwa watu wa tume.
 
Mkuu Marire, Nimeshangazwa na matokeo ya sehemu kadhaa zikiwepo Nyamagana, Ilemela.

Ni kweli kulikuwa na dosari kubwa sana katika Uchaguzi mwaka huu;

1. Ucheleweshwaji wa daftari la wapiga kura na uandikishwaji pia.

2. Usiri wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa vyama vya siasa.

3. Kauli mbaya na hatarishi zenye uchochezi mf. Ushindi ni lazima, kwani maarifa" tunayo. "Lowassa akishinda uchaguzi,ikulu haendi", " CCM ni lazima ishinde hata kama kwa bao la mkono.

4. Unyimwaji wa haki wa makusudi kwa wanafunzi wa vyuo na wananchi wengine(wasio wanafunzi) katika kupiga kura.

5. Ujanja/Hila/wizi kufanyika hadharani ukifumbiwa macho.
-Karatasi kuisha
-Masanduku ya kura kukamatwa
-


Niseme wazi hata UPDP au TADEA ndiyo wangekuwa wameshika dola, bado isingekuwa kazi rahisi kwao wao kuachia dola(hili halihitaji ufikiri). Lakini tunapokuja katika mustakabali wa Taifa ni lazima kipaunbele kiwe nchi na si Chama.

Tumeona, tumesikia na tumekuwa wahanga wa mengi. Jambo moja Serikali inalopaswa kutambua ni kuwa imeanzisha vita ya wazi na wanachi wake! Kuna usemi unasema "Don't fight with someone who has nothing to loose". Hapa ndipo Serikali inapopaswa kuangalia hasa.

Ninakubaliana na wewe kuwa hakukuwa na haja ya uchaguzi hasa kwa haya tunayoyaona yanatokea(Tume ya Taifa ya Uchaguzi kukaa kimya katika hili la masanduku kukamatwa, eti kituo kinaishiwa karatasi(kana kwamba taarifa ya Uchaguzi mkuu Tanzania ilijulikana tarehe 24/10/2015,n.k).

Upande wa pili, Ni jukumu la Tume kuwa huru, wazi na kusimamia haki na kuuweka msimamo huu kabla na wakati wa uchaguzi(KWA KUMAANISHA, refer hotuba ya Mwl. Nyerere). Hii huwaandaa wagombea kisaikolojia kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi na hivyo pande zote za Upinzani(kwa vyama vyake) na Chama tawala pia. Vinginevyo kila mtu atakuwa na sauti.

Ninachoweza kusema, tutegemee mengi hivi karibuni(assasinations, ubabe wa wazi(kuchoma magari, nyumba, watu kujeruhiwa), kupingana kwa viongozi hadharani(tena jukwaa moja).

Soon tutaheshimiana, very soon.
 
Last edited by a moderator:
Sikuwahi kupiga kura toka mwaka 1995 na nimekuwa nikiwaambia humu vyama visiingie kwenye uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi hata kama ccm na vibaraka wake watashiriki lakini dunia itasikia,..mwaka huu nikajua uwepo wa EL huku tume itatenda haki nikasafili mpaka kijijini kwengu ileje nilipojiandikisha kupiga kura...dah nimejuta! nimeuza mahindi yangu kwa ajili ya nauli kumbe wao wameshapanga mshindi wao.
 
Wakuu
Huu uchaguzi umeniacha na majonzi sana!!!
Nawashangaa wanaoshabikia vyama vyao kushinda maana huku mtaani tumeshuhudia mabox ya kura na karatasi za kura za wizi zikizagaa kama njungu na tume haijatoa tamko lolote

Nchi imeingia kwenye gharama kubwa kwa ajili ya uchaguzi,chama cha siasa kama ccm wametumia gharama kubwa kwenye kampeni na kuwalipa wasanii ili hali mwisho wa siku kumbe wanakuja kuiba kura na kutoa matokeo ya uongo,kulikuwa na haja gani ya uchaguzi??

Jeshi la police wameagiziwa magari brand new 777 napiga hesabu ukigawa kwa kwa majimbo 264 kila jimbo linapata gari 2 na yatabaki cha kushangaza kuna jimbo halina ambulance hata moja wala kituo cha afya wala maji safi na salama!!

Kwa binafisi yangu sioni haja ya kuwa na vyama vya siasa wala kuwepo kwa kampeni maana zinagharimu pesa nyingi na maisha ya watu kama jimbo la nyamagana wameuana vijana wanne kwenye hizi kampeni...
Kwanini tusiwe na chama kimoja kama china???

Kama hali hii itaendelea sioni sababu ya kuwa na uchaguzi

Ndugu yangu. Na kwa wale wote wenye mtazamo kama wako. Nawasihi msikate tamaa.

Demokrasia kwenye bara la Africa bado sana lakini hatua kwa hatua itakuwa kama wananchi hawatokata tamaa.

Kwa sasa nchi za Africa zina demokrasia ya unafiki. Ni tu kwa sababu wamelazimishwa na mataifa makubwa kufanya hivyo lakini bado tawala nyingi hazijawa tayari kufanya hivyo.

Mataifa makubwa bado yanaendelea kuwabana viongozi wa Afrika kama vile baba anavyowabana watoto wake ili wakae kwenye mstari sahihi ama sivyo utachapwa viboko au utanyimwa chakula. Ndivyo hali ilivyo kwa sasa.

Kwa sasa mnaweza kuwa na hasira na kukata tamaa lakini kura yako katika uchaguzi huu ni ushindi mkubwa sana kwa wananchi kuelekea kwenye hatua inayofuata ya CCM kulazimishwa kukuza demokrasia ndani ya nchi yetu. Mtaona matukio haya ndani ya mwaka huu.

Hivyo, hima wananchi. Mmefanya kazi kubwa na nzuri kuelekea kwenye hatua nyingine ya kukuza demokrasia ndani ya nchi yetu na hivyo mnastahili kujipongeza badala ya kukata tamaa.

Endeleeni kuunga mkono mapambano ya msingi ndani ya Taifa letu nayo ni kupata Katiba mpya na mtaweza kufanya hivyo tu kama hamtakatishwa tamaa na yale yanayojiri kwa sasa.

Ikitokea ama uchaguzi wote unatakiwa kurudiwa au kuna jimbo uchaguzi unatakiwa kurudiwa basi tokeni kwa wingi ili muunge mkono upinzani badala ya kukata tamaa.
 
Kwa kweli huwa nawashangaa sana mnaokwenda kupiga kura kwa matarajio makubwa...,.nashangaa wao wanavyonishangaa kwamba kwa nini mimi huwa sipigi kura....kwangu sioni sababu kusimama foleni ,kupigwa na jua ,vumbi nk....huwa nawashangaa mnafikiri kuachia dola ni kama kuachia ushuzi katika mazingira kama haya.....mimi sijawahi kupiga kura zaidi ya kura ya maoni mwaka huu ambapo mgombea wangu alifanyiwa uhuni wa wazi wazi na CCM...nikaapa sintojaribu tena!!!! sababu dhamira yangu inakataa kabisa kwamba mabadiliko yataletwa kwa kuchovya wino...dhamira inakataa....
 
Mimi pia nasitisha kupiga kura mpaka pale tutakapokua na katiba mpya itakayozaa tume huru na haki ya uchaguzi. vinginevyo nipo tayari kuendelea kuishi kenye taifa hili ambalo Rais anachaguliwa pale chamwino na kundi la watu wachache kati ya watanzania mln 44
 
Trump kashasema ngozi nyeusi mnachoweza ni kulalamika,kula kula na kutiana basi. Ukitaka vielelezo vya tired minds,waokote waafrika kadhaa uone watakavyofit hadi ushangae.Kwa hiyo kwako wewe solution ni kutokupiga kura?Tunaishi katika dunia ambayo wanadamu wanaficha busara na ku-expose kiwango cha ujinga wao.So sad!!MARUFUKU KUKATA TAMAA.
 
Nami nimeapa kwa mizimu ya kwetu yote, siku zote nitakazokuwa Dunian hapa sitapiga KURA mpk ccm ikiwa imeondoka madarakani, kinyume chake acheni wajinga wachache waendelee kupiga kura. Mimi basi.
Mkuu, usipopiga kura nani atawaondoa ? Endelea kupiga kura na kuwaondoa taratibu taratibu kuanzia majimboni ili kupunguza majimbo yao, hatimaye ngazi ya juu. Kama ningekuwa na uwezo wa kuwashauri UKAWA, ningewashari wakubali matokeo. Huwezi kuoa siku hiyo hiyo na kutarajia kupata mtoto siku hiyo hiyo na kumwandikisha shule siku hiyo hiyo. Hata Mbuyu ulianza kama Mchicha, EL amewasaidia kuongeza idadi ya % ya kura za Urais huenda hata wabunge wa viti maalum wataongezeka, hiki sio kitendo cha kubezwa, ndege aliyeko mkononi ni bora zaidi aliyeko juu ya mti. Kitendo cha UKAWA kuungana katika uchaguzi huu kimewapatia nguvu na wamefanya vizuri sana ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Hata hivyo, imeshuhudiwa muungano huu kutoheshimiwa miongoni mwao wenyewe kiasi cha kusimamisha wagombea wawili kutoka vyama shirika kitu ambacho kimewachanganya baadhi ya wapiga kura kutoamini kama kweli ni muungano wenye tija, na wengine kuchanganya kura na kusababisha wagombea kushindwa; Katika hali kama hii, UKAWA wanapaswa kuchukua changamoto zilizojitokeza na kuanza kuzifanyia kazi kuanzia leo ikiwa ni pamoja na kuimarisha Muungano wao kwa malengo maalum. Kitendo cha kugomea matokeo hakitakuwa na tija kwa sababu Rais akishatangazwa ataanza kutumia ngivu zake za Urais nao kuendelea kulalamika bila kuhudumia wapiga kaura wao kama ilivyotokea mwaka 2010 walivyogoma kutomtambua Mhe. JK, lakini mbona JK amekuwa Rai hadi leo. UKAWA WENYEWE HAWAKUWA NA MUUNGANO THABITI, IMESHUDIWA WAKIPOTEZA BAADHI YA MAJIMBO KWA KUWA WALISHINDWA KUWEKA MGOMBEA MMOJA !!!
 
Inauma kwa kweli,,,,,ni bora kusiwe na uchaguzi wa rais,,pawe na uchaguzi wa wabunge,,, rais awe wa ccm kwa vipindi vyote viwili,, mi mwenyewe naapa sitokuja kupiga kura ya kumchagua rais,,zaidi ya mbunge na diwani tu,, labda km kutakuwa na tume huru ya uchaguzi,,,
 
Mtoa mada usijute kupiga kura wala usikate tamaa.
Mgombea wa urais kwa ticketi ya UKAWA ameitaka tume kusitisha utoaji wa matokeo ya rais baada ya kubaini kasoro ambazo ameziainisha.
Logically Lowasa ana pointi. Kama katika majimbo ya Dar es salaam ambapo wagombea walikuwa makini kufanya majumuisho ya matokeo kutoka vituoni na tumesikia kuna maeneo watumishi wa tume ya uchaguzi walidai nakala zao za matokeo zimepotea hali wakiwa na lengo la kuingiza nakala feki. Pia tumeona wagombea waliwabana watumishi wa tume kutumia nakala za matokeo kutoka vituoni na sio kuhesabu kura na wakafanikiwa wakapata ushindi. Hii inaonyesha hali hii huenda imetokea pia katika majimbo mengi kama sio yote yakiwemo ya mikoani. Hivyo kuna kila sababu tume ikubali matokeo ya rais yahakikiwe. Hii itaweza kuongeza % za ushindi. Na sehemu ikitokea tume inasema imepoteza nakala za matokeo basi uchaguzi nafasi ya rais urudiwe katika eneo hilo.
 
UKAWA mjilaumu wenyewe kwa kusimamsha Mgombea dhaifu na mwenye tuhuma za ufisadi!

Mtoa mada usijute kupiga kura wala usikate tamaa.
Mgombea wa urais kwa ticketi ya UKAWA ameitaka tume kusitisha utoaji wa matokeo ya rais kwa kubaini kasoro ambazo ameziainisha
Logically Lowasa ana pointi. Kama katika majimbo ya Dar es salaam ambapo wagombea walikuwa makini kufanya majumuisho ya matokeo kutoka vituoni na tumesikia kuna maeneo watumishi wa tume ya uchaguzi walidai nakala zao za matokeo zimepotea hali wakiwa na lengo la kuingiza nakala feki. Pia tumeona wagombea waliwabana watumishi wa tume na wakapata ushindi. Hii inaonyesha hali hii huenda imetokea katika majimbo mengi kama sio yote yakiwemo ya mikoani. Hivyo kuna kila sababu tume ikubali matokeo ya rais yahakikiwe. Na sehemu ikitokea tume inasema imepoteza nakala za matokeo basi uchaguzi nafasi ya rais urudiwe katika eneo hilo.
 
Nimepiga Sana Kura za Mabadiliko, nimefanikiwa Sana ngazi ya udiwani Na ubunge, Na wameniwakilisha vema kabisa, ngazi ya uraisi ndio figisufigisu lakini sitaacha kupiga Kura yenye fikra ya Mabadiliko kwani naamini katika maisha yangu hakuna dhambi mbaya Kama kukata tamaa katika kile ninachokiamini.
 
Back
Top Bottom