Dah! Walokole weengi n kama wameshikiwa akili zao, manake wayafanyayo n tofaut na akili ya kawaida ya kufikiri, jamaa yangu flani pamoja na kupata zero form 6 pale kibaha baada ya kujaza vitu vya ajabu kwenye paper mpaka leo bado mlokole
Yaan kama vile wamemuazima mtu akili
yaani mtu baada ya maisha kumpiga ndo anajifanya mlokole, muda wote kanisani unafanya nini kama sio kudata, makanisa yenyewe haya ya kina lus.eke.lo
Kwa maelezo yako na uwelewa wangu nianze na jinsi ninavyo kuona:
Ulipaswa kabla ya kuoa, uchunguze kwanza: Unataka mke wa kushinda kwenye baa au saloon ama kitchen party, maana hawa nao wapo ni wewe tu na upendeleo wako. Si rahisi kumbadilisha mtu mlevi akawa mlokole na mlokole akawa mlevi hivyo ulipaswa upate ready made kuliko kutransform. Mkeo, licha ya mapenzi yako ya kizamani ya kupigana pigana, amekusamehe, anataka mrudiane wewe hutaki. Maana yake huna roho ya msamaha. Waswahili husema 'Asiye samehe haliwezi penzi.' Kumbe wewe huwezi penzi ingawa unaweza kupanda.
- Mosi, unaelekeakuwa una wivu wa kupindukia kiasi kuwa hupendi mkeo atoke nyumbani hata kwa kwenda kanisani.
- Pili una udikiteta fulani, ndani mwako ni amri tu hakuna mjadala (negotiation), Unalotaka ndilo linakuwa.
- Una mapenzi ya kizamani ya kikurya ambayo yanahusisha kupigana pigana.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa uhuru wa kila mtu kuabudu imani aitakayo, lakini wewe unataka mkeo aabudu namna unavyotaka wewe, hivyo bila kujua, unataka kuwa juu ya Katiba ambayo ndiyo sheria mama ya sheria zote nchini. Masikini nduyu yangu hata hujui kuwa kuvunja Katiba ni kosa. Unaishi katika jamii ya watu wasiostarabika, wastaarabu huheshimu sheria zilizowekwa. Ni wanyama wa porini ndiyo wanaoishi kama unavyotaka wewe na mkeo muishi.
Sijazungumzia upande wa mkeo wala wazazi wake kwa sababu sijawasikia, lakini kubwa ni wewe uliyeomba ushauri na wao hawajaomba chochote. Ndoa ni taasisi inapaswa iheshimiwe na watu wote ukiwemo wewe mwenye ndoa. Mtu yeyote aliyemo kwenye ndoa hushawishiwa wakati wote na mtu mmoja mmoja vikundi vya watu marafiki mbalimbali wakike kwa wakiume, lakini wewe mwenye ndoa unapaswa kuwa na ushawishi mkubwa kushinda makundi yote. Tunapomshawishi mke hatumshawishi kwa mabavu, tunamshawishi kwa hoja huku ukinyunyiza juu yake UPENDO usiopatikana mahala pengine popote isipokuwa kwako tu
Mkuu huwapend sasa walokole..dah
sio siwapendi bali nawajua a-z wengi ni wanafiki, nimekuwa nikihudumu kanisani kwa muda kiasi Mungu amlaze pema mchungaji wangu Samwel Chumu alinifundisha vitu vingi sana kuhusu hawa wanaojiita walokole na wachungaji wao wachumia tumbo
Mkuu unanikumbusha..mimi nlimfatilia msichana tulikuwa tunasali nae, alikuwa na tabia kama za huyu ila yeye hta smartphone alikuwa hataki et inawatsup so itamtia dhambin
Mwisho akawa anadate na mlez wa kikund church..
Paka leo sina ham naooooo
But life is a very interesting game, MTU akioa mke anayetulia home analalamika oo mywifewangu golikipaflan ivi, kujibwetekea sake home, akioa mcharuko basi kila siku analalama kaibiwa, akioa chapombe basi ndo usiseme, akioa mfanyakazi analalamika all time yuko ofisini, wengi humu vihoro juu wakihofia wake zao kuchepukia kwa mabosi wao.
Basi Dunia vurugu, ukioa mpenda Dini ndo hivi Tena. Kwanini mnaoa si mkae tu msioe.?
Umesema vema mkuu
Lakin umehalalisha tabia ya mwanamke..
Ila kimsing jamaa hapingani na iman ya mwanamke ila ratiba iliyo kisiri
Sijahalalisha, ila kinachotakiwa mume amshawishi mkewe kwa upendo. Mimi binafsi mke wangu alikuwa akisali kanisa fulani sitaki kulitaja, lilikuwa na ratiba kama ya mke wa mtoa uzi. Nilimwacha mke wangu akiendelea kusali kama kawaida huku nikimshawishi kujali familia yake kwa kutumia biblia ileile. Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa soma mwanzo. Mke anapaswa kumtii mumewe na mume anapaswa kumpenda mkewe kama mwili wake. Mtu amwenye upendo hawezi kuupiga mwili wake hadi kuutengua ubavu. Biblia inatuasa ' mke anayeishi na mume asiyeamini asimwache kwa maana mume aweza kuokoka kwa kuangalia matendo ya mkewe. Mke mwema ana wajibu wa kutunza familia yake kwa umahiri mkubwa.
Mwisho, kwa kuwa nilikuwa natumia pia mafundisho ya biblia, mke wangu akaona ni kweli. Dini inapswa iwe ile iletayo upendo katikati ya chuki, ilete faraja miungoni mwa wenye ndoa, ilete gundi ya kuwaunganisha badala ya kuwatenganisha, kwa maana imeandikwa 'alichokiunganisha Mungu mwanadamu asitenganishe. Biblia inasema tuonyane kwa upendo siyo kwa kutenguana mbavu. Shughuli nzima ya mapenzi ni ya kubembelezana, kama huwezi kubembeleza na kubembelezwa hakika huwezi mapenzi. Acha fanya kazi nyingine, lakini hakuna kazi nyingine mbala wa mapenzi