Hello wanajamvi.
Kwa kweli ukweli na uwazi ni kitu kizuri katika mahusiano kwani kinajenga hisia za kuaminiana na kuwa huru kwa kila mmoja (Ni fikra zangu).
Back to the topic: Niko kwenye uhusiano na mwanamke ninayempenda sana na ambaye natamani ikimpendeza Mungu nimuoe. Huyo mrembo wangu hatujawahi kugegedana na hatuna mpango wa kufanya hivyo hadi tutakapofunga ndoa na sababu kubwa ya kuwa na maamuzi haya ni imani yetu kutokuruhusu na sisi tumechagua kumcha Mungu. Sasa huyu dada amekuwa akitaka kujua taarifa za mahusiano yangu ya siku zilizopita kabla hatujakutana na lengo kuu (kama anavyosema ni kuijua misingi yangu ya kimahusiano) na msisitizo wake mkubwa ni kutaka kujua kama huko nyuma niligegeda au sikugegeda. Mwanzoni nilimdanganya kidogo kuepusha matatizo ila jana katika story akauliza tena na nikajikuta nampa ukweli wote kwamba niliwahi kugegeda wasichana wawili niliokuwa nao kwenye uhusiano. Taarifa hizi zimemkwaza sana na mpaka sasa anadai hana amani kabisa na mimi jambo linaloninyima raha kwani kwa hakika hako ka tabia nilisha kaacha zamani na sina mpango wa kukarudia kabisa, ninampenda yeye peke yake na kwa sasa nina kusudio imara la kutokutenda hiyo dhambi.
nimwemwomba msamaha kwa kutokumweleza ukweli mwanzoni kasema amenisamehe lakini furaha ya awali haijarejea na hilo linaniumiza zaidi. Wadau nafikiria labda nisingemwambia ukweli leo furaha ingeendelea lakini sasa uongo nao dhambi (hata kama niliitenda mwanzoni hilo halinipi uhalali wa kuirudia na sitaki kabisa makosa ya siku zilizopita, nataka kutengeneza usahii sasa na wakati ujao). Nifanye nini kurejesha furaha yetu wapendwa?
Natanguliza shukrani.
Kwa kweli ukweli na uwazi ni kitu kizuri katika mahusiano kwani kinajenga hisia za kuaminiana na kuwa huru kwa kila mmoja (Ni fikra zangu).
Back to the topic: Niko kwenye uhusiano na mwanamke ninayempenda sana na ambaye natamani ikimpendeza Mungu nimuoe. Huyo mrembo wangu hatujawahi kugegedana na hatuna mpango wa kufanya hivyo hadi tutakapofunga ndoa na sababu kubwa ya kuwa na maamuzi haya ni imani yetu kutokuruhusu na sisi tumechagua kumcha Mungu. Sasa huyu dada amekuwa akitaka kujua taarifa za mahusiano yangu ya siku zilizopita kabla hatujakutana na lengo kuu (kama anavyosema ni kuijua misingi yangu ya kimahusiano) na msisitizo wake mkubwa ni kutaka kujua kama huko nyuma niligegeda au sikugegeda. Mwanzoni nilimdanganya kidogo kuepusha matatizo ila jana katika story akauliza tena na nikajikuta nampa ukweli wote kwamba niliwahi kugegeda wasichana wawili niliokuwa nao kwenye uhusiano. Taarifa hizi zimemkwaza sana na mpaka sasa anadai hana amani kabisa na mimi jambo linaloninyima raha kwani kwa hakika hako ka tabia nilisha kaacha zamani na sina mpango wa kukarudia kabisa, ninampenda yeye peke yake na kwa sasa nina kusudio imara la kutokutenda hiyo dhambi.
nimwemwomba msamaha kwa kutokumweleza ukweli mwanzoni kasema amenisamehe lakini furaha ya awali haijarejea na hilo linaniumiza zaidi. Wadau nafikiria labda nisingemwambia ukweli leo furaha ingeendelea lakini sasa uongo nao dhambi (hata kama niliitenda mwanzoni hilo halinipi uhalali wa kuirudia na sitaki kabisa makosa ya siku zilizopita, nataka kutengeneza usahii sasa na wakati ujao). Nifanye nini kurejesha furaha yetu wapendwa?
Natanguliza shukrani.