Najiuliza, BBC Swahili kwanini mna habari za kichochezi?

bomouwa

JF-Expert Member
Jun 19, 2014
1,149
797
Habari wanajamvi?
Leo katika kipindi cha Dira ya Dunia wameongelea juu ya habari ya Rais Magufuli kutembelea Rwanda, ofcoz ni jambo jema kutuhabarisha lakini kwa walioangalia habari na kusikiliza kwa umakini muandishi badala ya kuzungumzia ziara kama habari kuu akajaribu kutoa theme ya ari na badala yake akasema "ziara hiyo ni ya kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili uliokua umepwaya".

Analysis
Naomba I am humbled to declare that there is no any gaining interest on this thread. Lakini kwa chombo kikubwa cha habari tena chenye wahariri wa kitanzania na Kenya n.k ni jambo la kushangaza ambalo mimi naita uchochezi (I accept corrections) kulikua na haja gani kwa mhariri kurusha habari kua "safari ya Magufuli ilikua ni kuimarisha uhusiano uliopwaya"?

Kwanini mhariri hajaona umuhimu wa swala la daraja huko Rusumo na badala yake habari ikawa ya uimarishwaji wa mhusiano? Nilichoona habari hii ilijaa uchochezi kuliko kusifia jitihada zinazofanywa katika kuimarisha uchumi wa nchi zetu hizi.

My take
Wahariri wa kitanzania waliopo katika shirika hili wafanye kazi kwa uweledi kwa maana kufuatia na sakata la MCC inaonuesha kuna nguvu ya ziada kuonyesha Tanzania haijimudu kwa habari ambazo mimi naziita za kipuuzi.

Ifike mahala tujivunie utanzania wetu hata kama mkate wetu wa kila siku utakua matatani na hii ndio proffesionalism mahala popote na ndio uzalendo.

Wewe unaonaje?
Nawasilisha
 
Kwan hujui Kagame na Kikwete walitofautiana kidogo? Marais wakitofautiana,automatically nchi zinakuwa hazina mahsiano mazuri hivyo hupwaya. That is what they meant.
Does that conclude a scope for the two countries being in conflict?
 
There was no any conflict but there was no any good relation as well.
If that was the case then,there were no sense to bring up such comment especially to such an international media...
 
Nimesikiliza hii ya saa 3 na hata ya 12 jioni mwandishi hakusema moka kwa moja kama ulivyosema wewe alisema kuwa "ziara hiyo inadhaniwa kuwa ilikiimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili uliyoyumba kipindi chabutawala wa jk"

Kama ulisikiliza vizuri hasa ile ya saa 12 walisema hata sababu zilizopelekea nchi hizo kuwa na uhasama walisema ni suala la wanyarwanda kudaiwa vitambulisho na issue za personalities kati ya jk na PK.

Uandishi una engle tofauti unaweza kuandika habari yako so wao walichagua engle hiyo hasabuoizingitia hicho ni chombo cha habari cha kimataifa.
 
Mkuu mara zote kila linapokuja suala la kufanya kazi au kutoa maamuzi, payroll ina nguvu sana kuliko kitu kingine. Ni wachache sana wanaweza kuhatarisha kazi/maisha ili kusimamia wanachokiamini.

Ni ukweli usiopingika kwamba kulikuwa na mgogoro kati ya hizi nchi mbili, lakini haipingi wala haiondoi ukweli kwamba hii ziara pia ina mambo mengine mengi mazuri, nani anareport, anareport kitu gani na anafanya hivyo kwa maslahi yapi inabaki kuwa uamuzi wa vyombo husika.

Nilichokipenda kwenye huu uzi, ni tuwe watu wa kupembua mambo na kuchambua ili kuweza kupata maana tofautitofauti ya habari zinazotufikia. Umeitazama hii ziara kwa upande chanya, wachache sana wangekua na huo muelekeo. Shukrani
 
Nimesikiliza hii ya saa 3 na hata ya 12 jioni mwandishi hakusema moka kwa moja kama ulivyosema wewe alisema kuwa "ziara hiyo inadhaniwa kuwa ilikiimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili uliyoyumba kipindi chabutawala wa jk"

Kama ulisikiliza vizuri hasa ile ya saa 12 walisema hata sababu zilizopelekea nchi hizo kuwa na uhasama walisema ni suala la wanyarwanda kudaiwa vitambulisho na issue za personalities kati ya jk na PK.

Uandishi una engle tofauti unaweza kuandika habari yako so wao walichagua engle hiyo hasabuoizingitia hicho ni chombo cha habari cha kimataifa.
Ndio maana liandika "I accept corrections"
 
Kwenye diplomacy ya kimataifa ni dhahiri kuwa uhusiano ulikua umepwaya.

Ile operation aliyoiendesha kikwete kutimua raia wote wa kigeni ukanda ule, ililenga hasa kutimua wanyarwanda.
Matamshi ya PK dhidi ya JK kwamba ipo siku "atamfanyizia kitu mbaya" kidiplomasia si kauli nzuri.
Kupeleka Jeshi Kongo kubana mirija ya Rwanda kwenye madini ya Congo ilikua ni ishu pia ya vita baridi.
Kagame kukataa wanajeshi wa Tanzania kupita ardhi ya nchi yake walipokuwa wanatoka Congo pia ni signal katika diplomasia.

Kitendo cha Rwanda na Kenya kuunda Coalition of the willing pia ni signal tosha.

Haihitaji PHD kujua kuwa kulikua na vita baridi kati ya Tanzania na Rwanda...
 
Watanzania acheni unafiki.
BBC Swahili hawajakosea wameelezea hali halisi.
Mlikua mnamtukana Kagame leo hamna namna inabidi mumpende tu kwa kuwa Pombe amewatangazia kuwa Kagame ni rafiki yake mpendwa.
Mkuu, tena nakumbuka hata wakati wa kuapishwa kwa JPM, wakati Kagame anatambulishwa, juna mijitu ilizomea pale uwanjani, na akaoneshwa JK akiwa kama anatoa body language ya kukubaliana na hali hiyo, wakati nadhani alitakiwa kuonyesha sura ya kutoapprove hali hiyo...
 
Mimi sipo sana kwenye maoni ya BBC juu ya ziara hii. Lakini nataka niwarudishe nyuma; naamini wengi mnakumbuka, Mhangwa na mchambuzi maarufu na stadi Tz aliwahi kuandika juu ya "BAHIMA EMPIRE" si mnakumbuka? Alitengeneza empire ya kufikirika kuwa Eastern Congo, Burundi, Rwanda, Uganda..... kuwa kuna mpango wa siri nzito za kumuhusisha Kabira (DRC) kuachia vurugu Eastern Congo ni kwa sababu ya hiyo siri nzito. Where as sasa the Bahima empire has grown and has more off springs. Is that what Mhangwa the great analyst was foreseeing? That may be, underline may be, Mzinza is now joining in?
 
Back
Top Bottom