Najihisi nina mkosi kwenye mapenzi

Najihisi nina mkosi kwenye mapenzi

Zakithi

Member
Joined
Jun 17, 2019
Posts
69
Reaction score
72
Mimi ni mwanamke wa miaka 27,sijaolewa,Sina mtoto,Sina mpenzi,nimepanga naishi na mdogo wangu mmoja yuko kidato cha nne sasa.

Tatizo langu ni moja tangu nianze kujihusisha na mapenzi napata wanaume ama wapenzi wanaoniomba hela na kutaka mie ndiyo niwahudumie.Nina kazi ndio ya kawaida tu ila sijui kumwomba mwanaume hela.

Ni mtoto wa pekee,niliyelelewa na wajomba baada ya wazazi kuondoka duniani.Nilipitia kipindi kigumu sana wakati nakua na kwenye elimu yangu,hiyo ikanijengea kujiamini na kujitafutia vyangu.

Sijui kujigamba,sichezei pesa kwa mambo yasiyo ya msingi ila nina roho ya huruma sana. Naweza kuwa na milioni hata 5 kwenye akaunti na bado nikapanda daladala ama kula kwa mama ntilie mtaani au kazini.

Mpenzi wa Kwanza alikuwa ananipiga mizinga sana baada ya kuja kwangu na kuona navyoishi,hatukudumu tukaachana sababu hiyo,kwani hakuwahi nipa hata senti yake ila yeye amenilia hela zangu nyingi.

Wa pili ilikuwa hivyo hivyo kila leo alikuwa anapanga mbinu za kunitoa hela,nikaona isiwe shida nikaachana naye. Wa tatu alikuwa ananisema niache kuwapa watu hela ila akishika simu yangu anajifowafia hela toka line yangu ya mpesa,halafu ananikashifu kuwa najidai kuwa na hela wakati sijawahi mweleza hayo,ila alikuwa anachunguza akaunti zangu za m-pesa na benki akanifosi nikampa hadi pasiwedi akawa akihitaji hela anatoa bila kunitaarifu. Nikaona isiwe tabu nikaachana naye.

Sasa hivi yapata mwaka niko single na nimeamua kutokudate tena manake napata magarasa tu.

Naombeni ushauri nakosea wapi? Kiukweli siwezi kuomba hela na nikiomba kama nina uhitaji nisipopewa basi najikalia kimya tu.

Kwanini wanaume waniombe hela?kasoro yangu ni Nini?na katika wote hao hakuna niliyemtongoza walinotongoza wenyewe.

Mie sipendi kuomba wala kuombwa hela. Naumia sana kama mwanamke. Naona wananitongoza kwa lengo la kunichuna,lakini mbona mie navaa kawaida,nala kawaida,siyo mtu wa starehe. Tatizo ni nini?
 
Njoo kwangu mama ni mapenzi kwenda mbele maana kuombana pesa hata mimi sipendi.
Huna tatizo labda life style yako unapokutana nao unaonekana unazo so wanakuwa na wewe kwa mlengo huo wa kukutoa pesa. Swali ni je unajiamini ni mrembo?
 
Pole sana dada usiwe unasema kila kitu kwa wapenzi wako
Sisemi,nashangaa wanajuaje mambo yangu
Mimi msiri sana hata kazini sina mashoga na kulialia shida siwezi hata kama sina kitu
 
Hili ndilo jibu sahihi. Jipe muda wa kutosha kabla ya kuwa wazi kwa mpenzi juu ya kila kitu. Ilimchukua miezi mitano mpenzi wangu kujua jina langu halisi,kabila langu na kazi yangu. Na bado vingi tu namficha!!
Pole sana dada usiwe unasema kila kitu kwa wapenzi wako
 
Njoo kwangu mama ni mapenzi kwenda mbele maana kuombana pesa hata mimi sipendi.
Huna tatizo labda life style yako unapokutana nao unaonekana unazo so wanakuwa na wewe kwa mlengo huo wa kukutoa pesa. Swali ni je unajiamini ni mrembo?
Ukisema mrembo wamaanisha nini?
 
Sisemi,nashangaa wanajuaje mambo yangu
Mimi msiri sana hata kazini sina mashoga na kulialia shida siwezi hata kama sina kitu
Kuna namna wanajua mambo yako, ambayo wewe huijui
 
Naelewa hali ni ngumu ila wajisokoaje kumwomba hela mwanamke ambaye hijawahj mpa hata buku?ama hajawah kuomba hata senti?huoni ukakasi?
Maisha magumu Sana tuoneeni huruma kidogo wanaume zenu tunapitia kipindi kigumu Sana
 
Ipi hiyo?au kwasababu siombiombi hovyo?
Kuna wakati hadi walinizushia kuwa ni mtu wa system kutokana na haiba yangu
Ni sababu moja wapo, pamoja na ile kuona una wategemezi wachache, kama hivyo wazazi wamefariki, unakuwa na extra money endapo unajishughulisha sasa na unaingiza kipato, pole sana vijana wa siku hizi sijui tumekuwaje wengi tunaangalia fursa katika mapenzi
 
Back
Top Bottom