Kuna siri nzito ndani ya JF
Kwanza napenda tu kuwapa pole na majukumu ya kila siku,nimeamua kusogeza hapa mtazamo wangu ili na mimi kidogo nijione mwenye kufanana na ninyi kwa mawazo,mijadala na michango mbalimbali ,lakini kuna kitu ambacho huwa kinanifanya mimi nijione wa tofauti kidogo na wenzangu humu ndani hadi kufikia hatua ya kushindwa kuandika nyuzi za kuelimishana kwa kushindwa kuwatambua vyema watu wa humu ndani kuwa ni wa namna gani, baadhi ya vitu vinavyoniashiria kuwa mimi ni watofauti ni kama vile
1.watu wanaonizunguka; yaani kila nikiwaangalia watu wanaonizunguka na kuwafuatilia maongezi yao sijawahi kuona wakizungumzia maswala ya jamii forum kama ilivokuwa kwa mitandao mingine kama facebook,instagram,twiter,whatsapp,youtube lakini kuisikia JF sijawahi ila naweza kuisikia mara moja kwa miezi miwili kupita
2.michango,majadiliano,na hoja ndani ya JF, kila nikifuatilia michango na hoja za watu mbalimbali humu ndani huwa nahisi kuwa hawa watu ni wa familia moja,ni kikundi cha watu,au wanafahamiana maana asilimia kubwa maongezi yao kama yanafanana ivi na kila nikisoma baadhi ya hoja na comments huwa naishia kustaajabu na kufurahia saana maana watu wa humu kidogo wamejaariwa kauli
3.misamiati inayotumika;kuna baadhi ya misamiati huwa naisikia humu tu kwenye majukwaa mbalimbali ya JF na haijakuwepo kwenye social network zingine kama vile watu wa lumumba,buku saba na mengine mengi ambayo yamepata kibali mbele ya jf na si mitandao mingine
4.watu wa mtaani na simu zao;kuna watu wengi sana ambao nipo karibu nao au nawaona barabarani,kwenye daladala na maeneo mengi sijawahi kuwaona wakisoma habari yoyote kwenye app ya JF ila utawakuta fb,insta,whatsapp na mitandao mingine ila siwaoni JF, lakini pia hata nikipekua simu zao ili nione app walizonazo sijawahi kuona app ya JF na inafikia kipindi nawafundisha na kuwasaidia kuinstall app ya JF na kisaikolojia ukiwaangalia watu wengi wanaonekana kutoijua vizuri app hii ambayo pia watu wengi wanaonekana kuitumia
Sasa hao wanaoitumia wako wapi?
5.baadhi ya hoja zinazotolewa/kuanzishwa na watu humu ndani:KUNA BAADHI YA HOJA HUMU HUWA ZINAANZISHWA NI HOJA AMBAZO SI ZA KAWAIDA YAANI INAONEKANA MTU ALIYEIANDIKA ANA AKILI ZA JUU SANA YAANI KILA UKIANZA KUISOMA UTAONA KUWA ENDAPO HUYU MTU ANGEKUWA KIONGOZI ANGEISAIDIA NCHI PAKUBWA SANA ILA UKIJA KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA HUWAONI WATU WENYE HOJA KAMA HIZO KWENYE MITANDAO KAMA YA WHATSAPP HUKO NA KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA
SASA HAWA WATU WAKO WAPI WAJITOKEZE HADHARANI NA WATOE MICHANGO ILI KUSUDI WAHUSIKA WANAOKUSUDIWA NA HOJA HIZO WAJIREKEBISHE NA KUFUATA USHAURI WENU KULIKO KUJIFICHA HUKU JF??
Nina vielelezo vingi sana ambavyo vinanifanya mimi niwe wa tofauti humu ndani
Kwani mara nyingi huwa naishia kusoma tu comment za watu kwani sijajua type ya watu wa humu sijui mkoje yaani utafikiri hampo kwenye nchi yenu ni wakati sasa wa wanaJF kujulikana kuwa nanyie mpo kwenye mazingira yetu maana inaonekana mtu akiwa JF ni mtu tofauti na mimi
Haya ahsante na maandalizi mema ya sikukuu yetu ya muungano wa zanzibar na Tanganyika tarehe 26april
Kwanza napenda tu kuwapa pole na majukumu ya kila siku,nimeamua kusogeza hapa mtazamo wangu ili na mimi kidogo nijione mwenye kufanana na ninyi kwa mawazo,mijadala na michango mbalimbali ,lakini kuna kitu ambacho huwa kinanifanya mimi nijione wa tofauti kidogo na wenzangu humu ndani hadi kufikia hatua ya kushindwa kuandika nyuzi za kuelimishana kwa kushindwa kuwatambua vyema watu wa humu ndani kuwa ni wa namna gani, baadhi ya vitu vinavyoniashiria kuwa mimi ni watofauti ni kama vile
1.watu wanaonizunguka; yaani kila nikiwaangalia watu wanaonizunguka na kuwafuatilia maongezi yao sijawahi kuona wakizungumzia maswala ya jamii forum kama ilivokuwa kwa mitandao mingine kama facebook,instagram,twiter,whatsapp,youtube lakini kuisikia JF sijawahi ila naweza kuisikia mara moja kwa miezi miwili kupita
2.michango,majadiliano,na hoja ndani ya JF, kila nikifuatilia michango na hoja za watu mbalimbali humu ndani huwa nahisi kuwa hawa watu ni wa familia moja,ni kikundi cha watu,au wanafahamiana maana asilimia kubwa maongezi yao kama yanafanana ivi na kila nikisoma baadhi ya hoja na comments huwa naishia kustaajabu na kufurahia saana maana watu wa humu kidogo wamejaariwa kauli
3.misamiati inayotumika;kuna baadhi ya misamiati huwa naisikia humu tu kwenye majukwaa mbalimbali ya JF na haijakuwepo kwenye social network zingine kama vile watu wa lumumba,buku saba na mengine mengi ambayo yamepata kibali mbele ya jf na si mitandao mingine
4.watu wa mtaani na simu zao;kuna watu wengi sana ambao nipo karibu nao au nawaona barabarani,kwenye daladala na maeneo mengi sijawahi kuwaona wakisoma habari yoyote kwenye app ya JF ila utawakuta fb,insta,whatsapp na mitandao mingine ila siwaoni JF, lakini pia hata nikipekua simu zao ili nione app walizonazo sijawahi kuona app ya JF na inafikia kipindi nawafundisha na kuwasaidia kuinstall app ya JF na kisaikolojia ukiwaangalia watu wengi wanaonekana kutoijua vizuri app hii ambayo pia watu wengi wanaonekana kuitumia
Sasa hao wanaoitumia wako wapi?
5.baadhi ya hoja zinazotolewa/kuanzishwa na watu humu ndani:KUNA BAADHI YA HOJA HUMU HUWA ZINAANZISHWA NI HOJA AMBAZO SI ZA KAWAIDA YAANI INAONEKANA MTU ALIYEIANDIKA ANA AKILI ZA JUU SANA YAANI KILA UKIANZA KUISOMA UTAONA KUWA ENDAPO HUYU MTU ANGEKUWA KIONGOZI ANGEISAIDIA NCHI PAKUBWA SANA ILA UKIJA KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA HUWAONI WATU WENYE HOJA KAMA HIZO KWENYE MITANDAO KAMA YA WHATSAPP HUKO NA KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA
SASA HAWA WATU WAKO WAPI WAJITOKEZE HADHARANI NA WATOE MICHANGO ILI KUSUDI WAHUSIKA WANAOKUSUDIWA NA HOJA HIZO WAJIREKEBISHE NA KUFUATA USHAURI WENU KULIKO KUJIFICHA HUKU JF??
Nina vielelezo vingi sana ambavyo vinanifanya mimi niwe wa tofauti humu ndani
Kwani mara nyingi huwa naishia kusoma tu comment za watu kwani sijajua type ya watu wa humu sijui mkoje yaani utafikiri hampo kwenye nchi yenu ni wakati sasa wa wanaJF kujulikana kuwa nanyie mpo kwenye mazingira yetu maana inaonekana mtu akiwa JF ni mtu tofauti na mimi
Haya ahsante na maandalizi mema ya sikukuu yetu ya muungano wa zanzibar na Tanganyika tarehe 26april