Naitaji mkopo kugaramia Arusi yangu.

kwani harusi lazima iwe na sherehe?kisa cha kujitia madeni?jikune unapojifikia bana...
 

unaoa mke au unaoa sherehe??

mkuu, hebu achana na huo upuuzi wa harusi za kifahari... unahitaji pesa kwa mambo mengine sio harusi
 
Wakusamehe bure. Yani mkopaji, mpanga riba, muda wa kurudisha ni wewe mwenyewe basi jikopeshe mwenyewe.
 
Mkuu umenichekesha sana yani mtu akukopeshe 2mil. kwa faida ya 716,666.67 ndani ya miaka 4 kasoro? Wakati hiyo hela nikiizungusha ndani ya wiki moja napata hiyo faida hapo juu.
 

Heri ya mwaka mpya, 2014! I concur.
 

Kwa mawazo hayo nchi yetu itazidi kudidimia.
 
Mkuu cdhani km uko Serious! naona umekuja kuchangamsha baraza hapa! Zamani ndo MKE alikuwa issue kwa7bu kwanza Mwanamke mwenyewe alikuwa anatambua thamani ya yy kuolewa sio cku hizi wanawake wenyewe viBIRITI NGOMA unajitia madeni 7bu yakuoa cku mbili mnarushia STULI achana nahiyo maneno Wee nenda kajitambulishe kwao wazazi wake wakizingua mkikubaliana na my yf wako Nyie lisongesheni2!
 

kwa bandiko lako linanikumbusha kitabu cha "i will marry when i want" harusi wakti mwingine ni janga!
 
unaoa mke au unaoa sherehe??

mkuu, hebu achana na huo upuuzi wa harusi za kifahari... unahitaji pesa kwa mambo mengine sio harusi

looh mil 2 ni harusi ya kifahari kwa pesa yetu hii mkuu mil 2 ni kitu gani kwa miaka hii? kumbuka amesema "Pesa hii ni ya kulipa mahari, kupage, gharama za kwangu na bibi arusi"
 
looh mil 2 ni harusi ya kifahari kwa pesa yetu hii mkuu mil 2 ni kitu gani kwa miaka hii? kumbuka amesema "Pesa hii ni ya kulipa mahari, kupage, gharama za kwangu na bibi arusi"
Bado ni -----.... Ukiona unakopa ili uoe ujue hauko tayari
 
Bado ni -----.... Ukiona unakopa ili uoe ujue hauko tayari

hiyo ndo hoja jamaa hajawa tayari kukaa na mke kama hata mahali hawezi kulipa! akianzisha familia na akajaliwa watoto itakuwaje, acaha hilo kumtunza mke itakuwaje? aahirishe/aache ajipange zaidi.
 
mimi nakushauri usioe!

wewe endelea tu na maisha hayo hayo uliyonanyo!

kwa kutoelewa kwako, kuoa kwako kunamaanisha kutuongezea idadi kubwa ya watoto ambao hawatopata elimu bora, matibbabu, mahitaji muhimu sana kutoka kwa wazazi, na hata chakula nacho kitakuwa cha shida sana!

kwa jinsi hii, hata mkeo ataishia kutunzwa na wenye maduka na wachache wenye vijisenti. familia yako always itakuwa na matatizo ya hapa na pale ambayo hayatokuwa na maana! kwa jinis hiyo, pesa ya watu utairudisha vipi?

kwa jinsi hii, ndio maana wanawake za watu wanajipanga shekilango, sinza, buguruni, makoroboi na maeneo mengineyo mengi kwaa ajili ya kuuzia miili yao ili kuzilinda familia zao zisife kwa njaa, kwa sababu tu ya kuwa na kichwa cha familia ambacho hakijitambui!

mi nakushauri, rudi shamba kwanza ukatafute hayo unayoyaita maisha vizuri. fanya kazi kwa passion.. amini utafanikiwa katika tafuta yako! baada ya hapo usiende kukesha bar, jenga familia ambayo haitokuja kufa kwa njaa wala kukosa basics za maisha!
Excel.
 
Last edited by a moderator:

Oa tu mwana usiwasikilize wote hawa haruc jambo la kheri na kuna wazazi wengine hawaelewi kuhusu mahari. Pia ukiona mahari inakushinda ujue huyo mke si hadhi yako tafuta kwingine. Tafuta ambaye mahari elf 50.
 
Ina maana hajawahi kuchangia harusi yoyote? Ukipata watu 40 wakatoa 50,000 utapata 2,000,000/=. Watu 80 @ 25,000/=.

Haya mambo ya kuchangishana na kufuatana nyuma watu ndio hawayataki. Maana ushaweka kiwango eti 50,000!'
 
looh mil 2 ni harusi ya kifahari kwa pesa yetu hii mkuu mil 2 ni kitu gani kwa miaka hii? kumbuka amesema "Pesa hii ni ya kulipa mahari, kupage, gharama za kwangu na bibi arusi"

Kama mil. 2 sio hela si atoe! Watu wanapenda mbwembwe uwezo hawana
 

If you are not joking in this issue,ushauri wangu ni huu,kwanza watakiwa utambue "This is your show" so huna haja ya kukopa kwa ajili ya kufurahisha watu,pili napata mashaka kama unataka kujilinganisha na ndoa za either your friends au nduguzo,hapo kimjini twasema unabugi,You are what you are, never forge the image itakuja ikucost dearly,sasa three years walipa deni,are you sure ndani ya hiyo three years kajunior kakija si ndo life itakuwa tight zaidi,utaweza kucary hizo double responsibilities?Jipange upya mkuu na pengine ukitazama kwa upana zaidi utajikuta haupo tayari kwa hiyo res[ponsibility unafuata fashion,kuoa sio fashion mkuuu ohoooo
 
Omba mchumba wako huyo akulipie utamlipa mkiwa room!!! Never try this!
 
mkuu unamshauri akakope kwa ajili ya Harusi? Itamsaidia nini zaidi ya kuleta machungu baada ya harusi,akope kwa ajili ya mambo mengine bwana,raha ya ndoa siyo siku ile mnavopigiwa matarumbeta iala ni jinsi mnavoweza ishi kwa upendo kila siku hadi kupelekea watu kutamani kuishi kama unavoishi na mkeo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…