JERUSALEMU
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 3,106
- 3,523
Habari wanajamvi.
Rushwa ni adui wa haki! Hii zamani ilikuwa ni ahadi ya Mwana TANU lakini kwa bahati mbaya haikurithiwa na wana CCM.
Juzi tumeona tausi lukuki wakitolewa kwa Marais wastaafu kama zawadi. Kwangu mimi ile ni rushwa tena first class. Nitafafanua.
Kwangu mimi ile ni rushwa kwasababu siku chache zijazo vikao vya maamzi makubwa ndani ya chama cha mapinduzi, CCM vitaanza. Jamaa akisoma alama za nyakati anaona dalili mbaya upande wake hasa kuhusu mambo mawili au matatu.
Mosi, ni kuhusu hatima ya Bernard Membe, jambo lile si jepesi kisiasa.
Pili, ni kuhusu Makamu Mwenyekiti wake kuwekewa viuatilifu wakati wa vikao vyao vya ndani.
Sasa kulikuwa na haja kubwa sana kuwaleta pamoja viongozi wastaafu ili walau apate kuungwa mkono na watu maarufu ndani ya chama. Hii ni rushwa of its own kind.
Zawadi zozote mwaka wa uchaguzi kutoka kwa wanasiasa ni RUSHWA. Wale tausi ni rushwa!
Rushwa ni adui wa haki! Hii zamani ilikuwa ni ahadi ya Mwana TANU lakini kwa bahati mbaya haikurithiwa na wana CCM.
Juzi tumeona tausi lukuki wakitolewa kwa Marais wastaafu kama zawadi. Kwangu mimi ile ni rushwa tena first class. Nitafafanua.
Kwangu mimi ile ni rushwa kwasababu siku chache zijazo vikao vya maamzi makubwa ndani ya chama cha mapinduzi, CCM vitaanza. Jamaa akisoma alama za nyakati anaona dalili mbaya upande wake hasa kuhusu mambo mawili au matatu.
Mosi, ni kuhusu hatima ya Bernard Membe, jambo lile si jepesi kisiasa.
Pili, ni kuhusu Makamu Mwenyekiti wake kuwekewa viuatilifu wakati wa vikao vyao vya ndani.
Sasa kulikuwa na haja kubwa sana kuwaleta pamoja viongozi wastaafu ili walau apate kuungwa mkono na watu maarufu ndani ya chama. Hii ni rushwa of its own kind.
Zawadi zozote mwaka wa uchaguzi kutoka kwa wanasiasa ni RUSHWA. Wale tausi ni rushwa!