Naionya China, isijaribu

Japan nakubali. Ila India big no
 
Kweli mkuu, vita vya Ukraine vimei cost na kuipa hasara kubwa Russia. Hapo bado hatujazungumzia vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa wa watemi hawa wa dunia ya kwanza. Miaka 3 ijayo Russia itakuwa nyuma hata ya Saudia Arabia kijeshi na kiuchumi.
 
Nahisi anapiga mkwara tu, hawezi kuingia mazima kama mwenzake mrusi. Vita ya urusi imewazindua wengi ambao walifikiri vita ni kitu cha urahisi rahisi tu kama vile kutafuna big jii na kutema.
 
Tujikumbushe kwanza Uchina kama sikosei karibia zaidi ya mara tatu ilijaribu kuivamia Taiwan. Hata pia kwa Taiwan kutaka kufanya mpango wa kurudisha utawala wake Uchina kupitia mpango wa Project National Glory.
Mfano upo mgogoro wa mwaka 1954 ambao ulikuwa mkubwa kiasi kwamba Marekani ilitoa onyo la kutumia mabomu ya Nuclear kama utawala wa Mao Zedong utajaribu kuivamia Taiwan hali iliyomfanya Uchina atulie kwa muda kujitathmini upya. Pitia Taiwan strait crisis 1, 2 na 3.

Hivyo kijana mpango wa Uchina kuivamia Taiwan upo pale pale either through diplomatic process or through armed means, kinachomkwamisha Uchina ni uwepo wa Super Power wa Dunia pale Taiwan ambapo kuwepo kwa Taiwan kunamfanya Marekani aweze kum contain Uchina katika eneo la Pacific ya mbali akisaidiwa na Korea Kusini na Japan.
Uzuri ulijitokeza pale Uchina alipoweza kujitahidi kumtengeneza Communist Ally North Korea la sivyo angekuwa amezingirwa pakubwa sana (Wataalamu wanaelewa hapa madhara ya kuzingwa na adui, ndivyo alivyofanya Urusi baada kuona Ukraine inataka kujiunga NATO).
Katika kila namna Uchina itajaribu kila njia kuichukua Taiwan ila uwepo wa US pale ni nightmare kwa Taifa hilo kwa sababu mbalimbali kama vile uchumi na hali ya usalama maeneo ya Far East itakayo mwarhiri yeye vilevile. Wasalam.
 
U
Unafikir hawajui mkuu. Wanajua vizur,ila nchi ikishaongozwa na MTU mmoja inakuaga vigumu kusikiliza washaur,ndio maana marekani hawakurupuk mambo yao yanaamuliwa na vikao
 
Kabisa mkuu, nchi za kidikteta mara nyingi maamuzi yao huwa ni ya mtu mmoja alie mbele ya mstari. Hata kama kuna athari mbele yao wao wataenda tu ili mradi watekeleze matakwa ya dikteta wao.
U

Unafikir hawajui mkuu. Wanajua vizur,ila nchi ikishaongozwa na MTU mmoja inakuaga vigumu kusikiliza washaur,ndio maana marekani hawakurupuk mambo yao yanaamuliwa na vikao
 
Watu hawaelewi bwashee ,kwanza ukiwa vitani ni ngumu wawekezaji kuwekeza kwako kuhofia usalama,pia vita inaharibu diplomatic relationship, vita inatafuna bajet ya nchi,vita vinamaliza wanajeshi muhimu,vita vinaua biashara,yaan nikuambie tuu Russia anasababisha hasara kwa pande zote mbili,,ila navyoona Russia mda si mwing ataomba wayamalize mezan maana kama walimdindia kumwachia yule demu mcheza basketball kwa njia ya SWAP Jana naona Russia wamekubali yaishe.ngoja tuone maana sisikii tena Putin akileta mbwembwe
 
Na mchina alivyokwaopua Hong Kong ndio hivyo hivyo kama case ya Russia kukwapua Crimea , sasa muache ajichanganye kuingia Taiwan hapo ndio atajua maharage sio mboga
 
Hahaha Putin kanywea kama kidonge kinapowekwa ndan ya glas ya maji.
Sasa hivi anamtumia sana waziri wake wa mambo ya nje katika mambo yake.
 
Na mchina alivyokwaopua Hong Kong ndio hivyo hivyo kama case ya Russia kukwapua Crimea , sasa muache ajichanganye kuingia Taiwan hapo ndio atajua maharage sio mboga
China akipima kuivamia Taiwan ataambulia aibu ya karne. Madege yake na vifaru vya jeshi havitamsaidia kushinda vita.
 
Yaani wabongo banaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, unakaa nchi ya ulimwengu wa tatu, kwenye dampo la dunia, unajitia kuwashauri viongozi na serikali ya Russia na China yenye agents hatari wanayoijua hii dunia?
Umekula ugali wako na muhogo umeshiba unakuja kudhani una ijua kesho ya Russia kuliko FSB? Raisi tu wa Russia ni former KGB, serikali ya Ukraine ina agents wengi tu wana leak data...

Unaijua China kuliko MSS? Chinese wana puppets wengi tu serikali ya Taiwan, tunajua machache sana...

Russia wanajua walifanyalo, walishajiandaa, kila kitu kipo calculated...

Kama umeshiba ugali better ukae chini ufuatilie bifu ya Harmonize na Diamond na udaku wa insta, huwezi ijua China au Russia kama agents wao ambao hawalali, wana risk afya zao na maisha yao, wamesomea ukachero na wanaishi ukachero na wanakula kikachero hata mapenzi ni kikachero, wakipumua ni ukachero... Ogopa sana hio...

Kwamba Russia imeingia mtegoniπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, Huyo ni mbongo, hivi vile vichwa vyote vya wale wazee pale Moscow vyenye mvi, makachero wabobezi toka USSR hawakujua plans za US?πŸ˜‚πŸ˜‚

Inaskitisha sana kwa kweli..
 
Shida iliyopo US wanategemea bidhaa za china, kuanzia chupi hadi mitambo,, sababu viwanda vilihamia china kukwepa gharama za uzalishaji marekani, [emoji16][emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…