Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Zeni2017

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2017
Posts
1,247
Reaction score
534
Nilikuwa mdogo sana lakini naikumbuka kama jana!

Viwanda vya nguo kochokocho Mwatex, Urafiki, nk. Bora, chuma, mbolea, SIDO nk.

Shule ilikuwa na maana. Ukipasi la saba wewe umetimia hakuna kuhongahonga. Ukiwa kilimani (chuo kikuu) unaranda. Unangojea pijo kupanda.

Hakukuwa na TV lakini RTD ilikuwa burudani tosha kina mzee Jongo, Kipara, Mangushi, Pwagu na Pwaguzi. Usisahau wale watangazajj wa mpira kina Jongo hasa mbili kasorobo na ule mwimbo wa kipindi cha michezo.

Taarifa ya habari na ngoma 10 za mzee Morisi ikifuatiwa na mazungumzo baada ya habari. Habari za siku hizi wala hazinichengui.

Simba na Yanga ilikuwa ngoma nzito. Kibadenj na Sunday Manara. Miji ilizizima. Na hakukuwa na huu ujinga eti mchezaji kachukua hela za Simba na Yanga. Kulikuwa na kina Chogo chemba na Kapela, Yanga Yanga kweli Simba Simba kweli.

Reli ya kati hata kama usafiri ulikuwa mgumu lakini ulikuwa ni rahisi na wa uhakika hasa kwa wanafunzi.

Sikukuu Idi na Krismas utajua tu kuwa leo mjini watu wana furaha. Kila mtoto na nguo mpya. Kidongo chekundu kulinoga.

Kwa wala rushwa na wahujumu Nyerere aliwabamba na pesa za moto na wengi waliishia jela. Kwa wafanyakazi na biashara halali maisha waliyamudu vizuri.

Zamani magorofani Ilala pale kila baba alikuwa na gari. Kulikuwa na datsun, volswagen kobe na kombi, ford cortina na escort. Kulikuwa na land cruiser, landrover na range rover, morris na renault. Mikebe ya benzi za zamani. Pijo ndio usiseme. Teksi zote ni 404. Washua walikuwa na 204, 304, 404 na 504 kwa mabishoo wa mji. Halafu 404 na datsun zilikuwa na pick up zake.

Lile gari la Nyerere sijui lilikuwa Rolls Royce lile. Na pale ndani ya Makumbusho (Museum) kulikuwa na Rolls Royce sijui wajanja washaliuza.

Nani anakumbuka yale maziwa ya pakti ya pembe tatu. Kama sikosei yaliitwa KCC.

Kwa wasio na magari. UDA ilinguruma kila dakika tano. Hii nchi ilikuwa sambamba na Ulaya kwenye miaka ya sabini. Mitaa ilikuwa misafi na nyumba za mpangilio. Tizama nyumba za kota Ilala au za CDA Dodoma.

Namlaani sana aliyeuza lile gorofa la Ilala na kulifanya hoteli ya binafsi. Wengine tulikulia pale. Si afadhali wangehamisha ile shule ya Boma pale gorofani wakachukua eneo la Boma kufanya hiyo hoteli yao. Ubinafsi kitu kibaya sana.

LG Life is Good was then!

Sijui tulipotea stepu wapi!
 
Zama zimebadilika mkuu hiyo ilikuwa yako yetu hii mbona bado iko poa
Kuna barabara za kufika tuendako
Mawasiliano ya sim
Shule huru(binafsi)
Sawa viwanda vimepungua ila bidhaa zipo angalau kutokana na soko huria
Nk

Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app
 
Ile vurugu ya kariakoo na wamachinga mitaani haikuwepo. Dar ilikuwa na nidhamu kama Ulaya kila mtu na shughuli ya kueleweka. Vijiwe kulikuwa hakuna. Jiji likuwa safi.

Kinachoendelea sasa hivi ni kudandia maendeleo ya nchi zilizoendelea bila ya kuwa na misingi ya maendeleo waliyoweka wenzetu.
 
Wanadamu sio manyani mkuu lazima tubadilike kifikra
 
8684398ada7ea9f4e5f62f7d77ac0290.jpg


Tizama Dar ilivyokuwa safi.
 
Maisha ya zamani yalikuwa matamu sana


Ni kwa sababu ulikuwa hauna majukumu.....ulishawahi kukaa foleni wewe kusubiri unga, sukari, mafuta ya taa, mchele kitumbo, sabuni mbuni, dawa ya mbu? Hii ilikuwa karibia ya mwishoni wa miaka ya 70 wakati wa vita ya Uganda na baada yake. Miaka ile ilikuwa balaa asikuambie mtu.
 
Ni kwa sababu ulikuwa hauna majukumu.....ulishawahi kukaa foleni wewe kusubiri unga, sukari, mafuta ya taa, mchele kitumbo, sabuni mbuni, dawa ya mbu? Hii ilikuwa karibia ya mwishoni wa miaka ya 70 wakati wa vita ya Uganda na baada yake. Miaka ile ilikuwa balaa asikuambie mtu.

Kwani Marekani baada ya vita vya Iraq si iliingia kwenye recession?
 
Ni kwa sababu ulikuwa hauna majukumu.....ulishawahi kukaa foleni wewe kusubiri unga, sukari, mafuta ya taa, mchele kitumbo, sabuni mbuni, dawa ya mbu? Hii ilikuwa karibia ya mwishoni wa miaka ya 70 wakati wa vita ya Uganda na baada yake. Miaka ile ilikuwa balaa asikuambie mtu.
Haya ya miaka ya themanini mkuu siyo sabini anayoisema.
 
Walosomeshwa kwa pesa ya walipa kodi ndo walisaidia kuuza nchi....na bado wapo wanazidi kuuza nchi.

Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom