Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Akizungumza katika mkutano mkuu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, March 04, 2025, Ruvuma. Naibu waziri wa Habari, sanaa na Michezo na utamaduni Hamis Mwinjuma (Mwana FA) amevitaka vyombo vya habari kuripoti kwa usawa kwa vyama vyote kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Aidha amevitaka vyombo vya habari kuacha kuripoti taarifa zinazohamasisha kususia uchaguzi, kwa kuwa wananchi wamemuelewa Rais Samia Suluhu Hassan.
"Turipoti bila kuhamasisha kususia uchaguzi ama fujo kwenye uchaguzi tusiyaweke rehani maisha ya Watanzania, Watanzia wamemuelewa Rais Samia" - Naibu Waziri wa Habari sanaa, michezo na utamaduni
Aidha amevitaka vyombo vya habari kuacha kuripoti taarifa zinazohamasisha kususia uchaguzi, kwa kuwa wananchi wamemuelewa Rais Samia Suluhu Hassan.
"Turipoti bila kuhamasisha kususia uchaguzi ama fujo kwenye uchaguzi tusiyaweke rehani maisha ya Watanzania, Watanzia wamemuelewa Rais Samia" - Naibu Waziri wa Habari sanaa, michezo na utamaduni