Ni kuku wa aina gani wanakuwa vyema na kuvumilia magonjwa kati ya Sasso, Kroiler na Israeli?
Kama kuna aina nyingine naomba mnijulishe ili nianze rasmi ufugaji wa kuku.
Wa kienyeji wanalipa zaidi,ukiweza kutunza Vifaranga walau kwa muda flani wabaki ndani uwatunze kama kuku wa kisasa ,chakula na joto uku mama yake unamtimua akagegdwe atage tena
Inategemea na uhitaji wako/lengo la wewe kufuga, je ni kwa ajili ya:
*nyama
*mayai
*nyama na mayai
Black astro ni kuku wazuri lakini kwa ajili ya mayai kwenye nyama hawako poa
Kwa jinsi sasso walivyopatikana (evolution yao) ni wazuri katika utagaji wa mayai.
Kuroiler wao ni wazuri katika kutengeneza nyama japokuwa wote (sasso na Kuroiler) wanataga na kutengeneza nyama.
Unaweza kuwafuga kienyeji, Kuroiler na sasso na baada ya miezi mitano wataanza kutaga, kwa nyama itakuchukua wiki 10-12 kuanza kuwauza hapo watakuwa na kg Kuanzia 1.4 na kuendelea
Lakini kitu walichonacho kwa pamoja ni kutokuwa na uwezo wa kuatamia mayai unaweza kuta katika (sasso / Kuroiler) 10 ni wawili wenye uwezo wa kuatamia.
Magonjwa kuku wa kienyeji ni wavumilivu lakini kama umeamua kufuga ukifuata taratibu zote za kiafya Magonjwa hayatakuwa na sehemu kwa kuku wako, labda yale ya mlipuko.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.