Habari za leo wakuu?
Jamani mimi natarajia kuanza kilimo kwa ufugaji wa ng'ombe wa maziwa, nguruwe pamoja na mbuzi wa kisasa (mbuzi wa maziwa). Naomba msaada wa ushauri na maelekezo kwa wazoefu kuhusu upatikanaji wake bei, masoko pamoja na masuala mengineyo yanayohusiana na ufugaji huu.
Kama kuna mtu ana contacts pale SUA, nitashukuru maana nimesikia wanauza aina mbalimbali za mifugo ya kisasa kwa ajili ya kilimo.
Msaada tafadhali
BB
Mkuu, Shaloom
Hongera kwa wazo/mawazo mazuri
Kwauzoefu naomba nikushauri hivi
1-Kama huna mtaji wa kutosha huwezi ukaanza moja kwa moja na ufugaji wa mbuzi,ngombe na nguruwe kwa pamoja ukatoboa unless uniambia utafanya hivyo lakini isiwe kilimo biashara. Chagua kitu kimoja tafuta elimu then anza nacho.
2-Unatakiwa utambue sehemu unayotaka kufugia hali yake ya hewa ikoje..mbua zinapatikana za kutosha? ni malisho ya namna gani yanastawi,upatikanaji wa wafanyakazi,,,upatikanaji wa huduma za ugani....usalama....na mengineyo.
3-Kwa ufugaji wowote utakaofanya anza kwanza kulima/kuweka stock ya chakula.kama ni mbuzi/ngombe/nguruwe hakikisha una chakula cha kutosha cha kuwalisha angalau mizezi mitatu.....USHAURI WANGU....Ili ufanikiwe ktk ufugaji hakikisha unachakula cha uhakika na sio chakula tu majani na virutubisho vinavyotakikana kwa kila myama
4-Wekeza kwenye MBEGU mfano hakuna haja ya kufuga ngombe au mbuzi/Nguruwe wa kienyeji ambao utawalisha chakula kingi na wakupe matokeo madogo...Nguruwe Mtafute Malafyale Pig farms( kabla hujamtafuta NUNUA vitabu vyao viwili hakikisha umevisoma ukavielwa then watafute kwa ushauri zaidi na mbegu) Kwa Ngombe kama utafuga wa maziwa ( wekeza kwenye mbegu...Yapoa mashaaamba makubwa Iringa mfano ASAS, KWAPHILIPIS,KIBEBE FARMS, na mengneo ununue begu bora za ngombe andaaa TSH4,000,000/=Milioni NNE kwa ngombe moja mwenye MIMBA...Tambua na mazingira yana matters saana..Pia kama mfuko wako unaruhusu...WAPO NGOMBE WANAITWA FLECKVIEH asili yao ujerumani ni wazuri saana kwa nyama na maziwa. Kwa huu ukanda wa africa mashariki watafute...
Fleckvieh Genetics East Africa.....wanauza mashahawa kwa ajili ya kupandikiza ngombe....kama mfuko wako unaruhusu zaidi..watafute BUYERN GENETICS wakuuzie embriyo kabisa. kwa TZ kuna wazunngu wanafugia kilombero wanahizi breed
5- Kwa MBUZI..pia wekeza kwenye mbegu, tafuta madume ya BOER na SAVANAH ya cross na hawambuzi wa maziwa.mfanoa ALPNE, NORWEGIAN...machotara utakayopata yatakupa matoeo mazuri saana...Pure boar na savanah kumpata hapa tanzania ni ngumu saana,,,mpaka uagize SOUTH AFRICA au Uganda..kwa DAR watafute SHAMBAANI GOAT FARMS wanao pure boer goat na kalahari red ila hawauzi watakupa ushauri
6--Malisho ni muhimu saana ni bora ukaandaa shama maalumu kwa ajili ya kulima majani yako peke yako kwa ajili yakulishia mifugo...hapa ukimtembelea MSTAAFU KIKWETE PALE MSOGA UTAJIFUNZA MENGI....KUMBUKA ukiwa na chakula cha kutosha itakusaidia usitetereke kipindi cha ukama...nakumbuka mwaka juzi wafugaji wengi wa chalinze walienda nunua majani DODOMA kutokana na ukame...KWA NGOMBE NA MBUZI wa maziwa,,, unaweza lima mahindi yale yaNJANO then ukatengeneza SILAGE,, yapo majani mengine ambayo unaweza lima mfano ALFAFA mbegu unaweza agiza S&w SEED COMPANY(US) unaweza lima CHLORIS GAYANA mazuri saana kwa ajili ya mbuzi hata ngombe
7- Yapo mengi siwezi andika yote hapa...mfano kuna swala la MAGONJWA/CHANJO/MASOKO/WAFNAYAKAZI/WIZI nk
HITIMISHO ili ufanikiwe tafuta elimu ya kutosha kuhusu unachotaka kufuga/tafuta mtaji wa kutosha/litambue soko lako..then anza kufuga..
Karibu saana kwenye ufugaji