Nahitaji mwalimu wa Kiingereza kutoka Kenya

Nahitaji mwalimu wa Kiingereza kutoka Kenya

My story

Member
Joined
Jun 9, 2019
Posts
23
Reaction score
3
Habari wanaJF,

Leo acha nifunguke ukweli katika maisha yangu nilipenda sana kusoma ila kutokana na mambo yaliyojitokeza mwaka 2006 nikawa nimeacha shule na nilikomea darasa la sita. Kwahiyo, kuanzia kipindi hicho nikaamua kutafuta pesa maana ndoto za kuendelea na shule zilifutika kutokana na sababu ambazo sitapenda kuzieleza hapa.

Nimejitahidi sana kujifunza lugha hii ya Malkia kwa kiwango fulani.

Ila kutokana na ubusy wa kazi zangu nimeshindwa kuendelea kuwa English kozi.

Kwahyo natafuta mwalimu wa hii Lugha nitakayekuwa naongea nae tu muda wote kwa muda wa miezi mitatu najua kuwa nitakuwa nimeiva.

Nimependekeza Kenya sababu wao hii lugha hujifunza tangu shule za awali kwahiyo nina imani kuwa itakuwa rahisi zaidi kuelewa.

Kwa muda huo ataishi kwangu na huduma zote zitakuwa juu yangu.

Pia, nitamlipa mshahara tutakaokuwa tumelelewana. Ila ningependa umri wake awe chini ya 25 sababu sipendi kumwajiri ambaye tuko sawa kiumri au kanizidi.

NB: mshahara si tatizo.
 
Habari?

Aisee pole kwa yaliyokusibu huko kipindi cha mwaka 2006 lakini hongera kwa kushikilia msimamo na lengo lako la kutaka kujifunza lugha ya Kiingereza. Kujifunza lugha ni muhimu na kuna faida nyingi. Kwa mtazamo wangu na uzoefu wangu wa kimaisha naomba nichangie uzi wako kama ifuatavyo:

Kwanza, naomba utambue kuwa siyo kila mtu anaweza kufundisha ukaweza kumudu kujifunza comfortably. Uhusiano kati ya mwalimu na mwanafunzi unahitaji muunganiko fulani ili mwanafunzi awe huru kwa mwalimu na kwa mwalimu iwe rahisi kumsoma na kumuelewa mwanafunzi wake, hiki kitu huitwa "chemistry". Kwa maelezo yako nilivyoelewa unachotafuta hapa ni mkufunzi binfasi, (personal trainer). Personal trainer kwa umri usizidi miaka 25 napata mashaka kidogo kama atakuwa ana ukomavu wa kutosha kufundisha ama hata kuwa na saikolojia ya nafasi unayohitaji kumpa. Ama labda unachotafuta ni kijana tu ndani ya umri huo uwe unawasaliana naye kwa Kiingereza.

Pili, unapojifunza lugha inafaa mwalimu awe na matamshi yasiyo na lafudhi (pronounciation without accent). Kwa ninavyowahamu Wakenya wengi matamshi yao (hata ya Kiswahili) yana lafudhi kali (strong Kenyan accent). Ujio wa walimu wengi kutoka Kenya miaka kadhaa nyuma kwenye shule zetu za English Medium kulisababisha matamshi ya wadogo zetu kuharibika sana kuwa walifundishwa masomo kwa lugha ya Kiingereza yakiwa na lafudhi kali ya Kikenya. Hivyo samahani kwa hili ila SIKUSHAURI utafute mwalimu mwenye asili ya huko. Kama kuna Mkenya anasoma hoja yangu naomba nisamehe pia. Kiukweli kwenye upande wa kazi Wakenya ni wachapakazi wazuri sana.

Tatu, wapo vijana hapahapa wana Kiingereza kizuri tu na wanaweza kufanya hiyo kazi, na pia kama utapenda uwe unafanya mawasiliano ya hapa na pale kwa lugha ya Kiingereza fasaha.

Karibu sana mimi nipo. Feel free, we can communicate anytime.

Regards
 
Habari?

Aisee pole kwa yaliyokusibu huko kipindi cha mwaka 2006 lakini hongera kwa kushikilia msimamo na lengo lako la kutaka kujifunza lugha ya kiingereza. Kujifunza lugha ni muhimu na kuna faida nyingi. Kwa mtazamo wangu na uzoefu wangu wa kimaisha naomba nichangie uzi wako kama ifuatavyo:


Kwanza, naomba utambue kuwa sio kila mtu anaweza kufundisha ukaweza kumudu kujifunza comfortably. Uhusiano kati ya mwalimu na mwanafunzi unahitaji muunganiko fulani ili mwanafunzi awe huru kwa mwalimu na kwa mwalimu iwe rahisi kumsoma na kumuelewa mwanafunzi wake, hiki kitu huitwa "chemistry". Kwa maelezo yako nilivyoelewa unachotafuta hapa ni mkufunzi binfasi, (personal trainer). Personal trainer kwa umri usizidi miaka 25 napata mashaka kidogo kama atakuwa ana ukomavu wa kutosha kufundisha ama hata kuwa na saikolojia ya nafasi unayohitaji kumpa. Ama labda unachotafuta ni kijana tu ndani ya umri huo uwe unawasaliana nae kwa Kiingereza.


Pili, unapojifunza lugha inafaa mwalimu awe na matamshi yasiyo na lafudhi (pronounciation without accent). Kwa ninavyowahamu wakenya wengi matamshi yao (hata ya kiswahili) yana lafudhi kali (strong Kenyan accent). Ujio wa walimu wengi kutoka Kenya miaka kadhaa nyuma kwenye shule zetu za English Medium kulisababisha matamshi ya wadogo zetu kuharibika sana kuwa walifundishwa masomo kwa lugha ya Kiingereza yakiwa na lafudhi kali ya kiKenya. Hivyo samahani kwa hili ila SIKUSHAURI utafute mwalimu mwenye asili ya huko. Kama kuna mKenya anasoma hoja yangu naomba nisamehe pia. Kiukweli kwenye upande wa kazi waKenya ni wachapakazi wazuri sana.

Tatu, wapo vijana hapahapa wana Kiingereza kizuri tu na wanaweza kufanya hiyo kazi, na pia kama utapenda uwe unafanya mawasiliano ya hapa na pale kwa lugha ya kiingereza fasaha karibu sana mimi nipo feel free we can communicate anytime.

Regards
Asante sana mkuu, umenipa mwanga.

Na umeongea jambo moja muhimu sana ambalo pia nililizingatia, nalo ni la uchapakazi. Najua kuwa WaTz wapo wengi ambao wanaweza kufanya hii kazi ila changamoto ni uchapakazi wa ndugu zangu WaTz ndo nilioutilia mashaka.
 
Tuko pamoja mkuu.

Kila la kheri nakutakia maendeleo mema kwenye mafunzo yako ya Kiingereza.
 
Kama Ras Simba amekushindwa, au amekosa vigezo endelea.
We soma vitabu tu na kuangalia BBC
 
Kwanza kabisa Wakenya wanazungumza kiingereza kilichoathiriwa na lugha mama zao..primary nilisoma English medium ambayo 90% ya walimu walikua ni kutoka Kenya i.e Wakikuyu, Wakamba etc mapungufu yao ni katika utamshi i.e Thie Mboy- This Boy This Ngirl- This Girl utapotea mkuu wewe kama hela unazo nenda British Council unasoma kwa wiki mara 2 au ikishidikana English course centre zipo nyingi sana mkuu
 
Habari wanaJF,

Leo acha nifunguke ukweli katika maisha yangu nilipenda sana kusoma ila kutokana na mambo yaliyojitokeza mwaka 2006 nikawa nimeacha shule na nilikomea darasa la sita. Kwahiyo, kuanzia kipindi hicho nikaamua kutafuta pesa maana ndoto za kuendelea na shule zilifutika kutokana na sababu ambazo sitapenda kuzieleza hapa.

Nimejitahidi sana kujifunza lugha hii ya Malkia kwa kiwango fulani.

Ila kutokana na ubusy wa kazi zangu nimeshindwa kuendelea kuwa English kozi.

Kwahyo natafuta mwalimu wa hii Lugha nitakayekuwa naongea nae tu muda wote kwa muda wa miezi mitatu najua kuwa nitakuwa nimeiva.

Nimependekeza Kenya sababu wao hii lugha hujifunza tangu shule za awali kwahiyo nina imani kuwa itakuwa rahisi zaidi kuelewa.

Kwa muda huo ataishi kwangu na huduma zote zitakuwa juu yangu.

Pia, nitamlipa mshahara tutakaokuwa tumelelewana. Ila ningependa umri wake awe chini ya 25 sababu sipendi kumwajiri ambaye tuko sawa kiumri au kanizidi.

NB: mshahara si tatizo.
Mimi imezaliwa kule eldoreti kaunt ya kisumu ipo vizur sana kwenye kizungu pigia mimi +254765880800
 
Back
Top Bottom