Nahitaji msaada wa kifedha, nimekwama

Nahitaji msaada wa kifedha, nimekwama

Mara Huna Hata Kitanda, Mara Nitaweka Rehani Vitu Vyangu. Una Vitu Gani Sasa? Naona Wewe Ni Msanii Tu. Pia Nakushauri Nenda Pride Au Finca, Wao Wana Mikopo Ya Vikundi, Na Dhamana Yake Weka Hivyo Vitu Vyako Vya Ndani
mkuu ndio maana nikasema nitaweka rehani vitu vyangu ila ntakaa navyo kwa maana ya kwamba ndivyo ninavyovitumia katika biashara hii ya juice! vitu nilivyomaanisha ni freezer,brender,juice dispenser na hata baiskeli niliyotengeneza! nafikir umenielewa mkuu!!!
kuhusu pride na finca nilishaenda huko ila wanataka uwe na leseni,uzoefu mda mrefu na kazi uwe ushaanza inaendelea pia wanataka dhamana!
kuhusu vikundi ni kuanzia watu watano,ila kupata watu wenye mawazo,uchungu na wasio ogopa mikopo kama mimi imekuwa ngumu kwa sababu inatakiwa wote muwe mnakaa sehemu moja kama mtaa na biashara ziwe karibu!! ila mkopo ninaohitaji mimi ni wa haraka mkuu ingekuwa ni baada ya miezi kadhaa ningelijua nifanye nini
 
Nitafutie BANK inayo nunua MADENI ukiipata Niambie nikauze MADENI yangu then nitakukopesha.
 
mimi ninafanya kazi kampuni ya ujenzi ngoja niangalie kwa matechnician wetu kesho kuna kazi gani site nikuambie uende huko maana kwa siku ni elf 10 hadi 15 nadhani
kuna kujenga ,zege ,kuna barabara kazi mbalimbali nk
nitakupa mrejesho
upo tayari kwenda hata mikoani sio?
. .samahani kama nitakua nakosea mimi niko moro kama kuna uwezekano niunganishe . mana me natafuta kaz yoyote ambayo nitaingiza hata kipato kidogo kwa siku
 
HAUNA HELA,ALAF UNA SIMU YA KUINGIA JAMII FORUM,ALAF UNAJIITA HAMIS,MBONA UNATUDHALILISHA WAJINA,TAFUTA KAZI,KUOMBA NI KUJIDHARIRISHA MDOGO WANGU,
 
HAUNA HELA,ALAF UNA SIMU YA KUINGIA JAMII FORUM,ALAF UNAJIITA HAMIS,MBONA UNATUDHALILISHA WAJINA,TAFUTA KAZI,KUOMBA NI KUJIDHARIRISHA MDOGO WANGU,
samahani kama nakuzalilisha mkuu ila natamani kama ungeliweza kujua hali iliyopo!!
mkuu usifikir labda sijawaza kitu kama hicho! nishawaza sana tu hata nishawaza kuuza hivi vifaa nilivyonavyo ili nipate cash! ila at the end ni kwamba nikishauza baadae nikiingia ndani nitavihitaji tena make ni vitu vya lazima kuwa navyo ili ufanye kazi!
simu hata nikiuza haitamaliza tatizo maana ni ya hela ndogo sana tu! hata hivo kuna shughuli natakiwa nije nianze kuifanya ambapo simu tena smartphone niblazima niwe nayo sababu ya camera, nishawaza kuuza vitu vingi ila naona ntakuwa najidanganya mwenyewe!
kufanya kazi sijashindwa mkuu, hata hivo mpaka kujipanga kupata hivi vifaa nayo ni kazi pia! na ndo maana nikasema kuwa kama hii hela ingekuwa inahitajika baada ya miezi kadhaa ningetafuta taratibu bila kuomba ila kwa sababu ni hitaji la haraka ndo maana nikaomba na tena nimeomba kukopeshwa!!!!!
mkuu mi sio mjinga kuja kuomba hapa! ni mitihani inakuwa mingi tu
 
Refa kauzu, uwanja wenyewe mkavu. Kilichobaki kucheza rafu!

Harakati za mtu mweusi zina changamoto nyingi sana kwakweli. Wengi wetu vijana tupo on the same shoes. Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi inshaalah.

Bongo nyosso, Bongo balaa. Kaza jombaa.

-Kaveli-
 
powa wajina usiwaze sana,ndo ukubwa huo,si unajua wanaume tumeumbwa matesooo matesooo kuhangaikaaa,
 
Refa kauzu, uwanja wenyewe mkavu. Kilichobaki kucheza rafu!

Harakati za mtu mweusi zina changamoto nyingi sana kwakweli. Wengi wetu vijana tupo on the same shoes. Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi inshaalah.

Bongo nyosso, Bongo balaa. Kaza jombaa.

-Kaveli-
nashukuru kijana mwenzangu,mambo magumu
 
Miss natafuta kaisha ufunga huu uzi labda mleta mada aje afungue uzi mwingine wa mrejesho hongera miss natafuta kwa mguso uliouonyesha.
mkuu nashukuru kwa wazo lako japo bado sijaonana na Miss Natafuta ,pia kanambia kuna kazi ila bado nitakuwa sijatatua tatizo lote kama hela ya kumalizia mradi wangu na kodi tu!!! ambavyo vyote vinahitaji laki sita (600,000), hii ni hela ambayo inahitajika haraka sana maana mda unakaribia kuisha!!! ila dada Miss natafuta kasema kunitafutia sehemu ya kibarua cha kulipia kwa siku angalau siku zisogee nipate ya matumizi ya mambo ya kawaida!!! nafikiri umenielewa Mkuu!!
kwa hiyo bado nahitaji mtu atakayeweza kunikopesha hiyo laki sita ili nitatue hili tatizo la haraka sana!!
 
mkuu nashukuru kwa wazo lako japo bado sijaonana na Miss Natafuta ,pia kanambia kuna kazi ila bado nitakuwa sijatatua tatizo lote kama hela ya kumalizia mradi wangu na kodi tu!!! ambavyo vyote vinahitaji laki sita (600,000), hii ni hela ambayo inahitajika haraka sana maana mda unakaribia kuisha!!! ila dada Miss natafuta kasema kunitafutia sehemu ya kibarua cha kulipia kwa siku angalau siku zisogee nipate ya matumizi ya mambo ya kawaida!!! nafikiri umenielewa Mkuu!!
kwa hiyo bado nahitaji mtu atakayeweza kunikopesha hiyo laki sita ili nitatue hili tatizo la haraka sana!!
Ni kweli ndugu yangu lakini kuna wakati sio kila jambo tunalo lipanga huja hivyo hapana ndio maana kuna neno kuakhirisha jambo au wahenga hunena maji yakizidi unga ugali haupikiki una koroga uji siku inapita.
Laki sita sio maji mafupi kwa usawa huu tulionao sisemei wengine ila kuipata kwa haraka haraka ni mtihani mkubwa endelea kupigana ila kwa maoni yangu ungejaribu kujikita kwenye mipango mingine kwanza hilo la project yako ungeliweka pending kwanza.
 
Habari za humu ndani?

samahani kwa nitayemuudhi labda kwa kuweka wazi sana maisha yangu, ila waswahili husema mficha uchi hazai na mficha maradhi kifo humuumbua! Najua humu ndani kuna watu wakubwa,wenye nyazifa tofauti,matajiri wenye uwezo tofauti,wafanya biashara, watu wenye fani tofauti n.k .

Naomba mnisikilize nakuja mbele yenu ninaomba msaada wenu na natumahi kuwa ipo siku ambayo haina tarehe wala saa nitarudisha fadhira kwa atakayenitoa katika shimo hili.

Mimi ninakaa Dar es salaam, katika kipindi cha kusoma kwangu nimejitahidi kukusanya hela kiasi japo kwa shida sana sana ili zije zinisaidie baadae! nilivomaliza ikabidi sasa nianze kutumia hizo hela katika kujitegemea na kutafuta maisha kiujumla! nikawaza nifanye biashara gani ambayo ni risk calculated business! nikaona afadhari biashara ya juice kwa kuzingatia hali ya jiji hili la Dar!

Basi kiasi fulani cha hela nikanunua freezer, brender na juice dispenser pamoja na nikatengeneza baiskeli maalumu itakohusika na usambazaji wa juice! kwa kuwa ndo kipindi cha joto kinaanza sasa nikawa natakiwa nianze kazi rasmi!

MTIHANI SASA

hizo hela nilizojitahidi kuzikusanya kwa shida sana sasa zimeisha kutokana na kwamba nimenunulia hivyo vifaa na pia kwa matumizi binafsi ukizingatia hamna mtu ninae mtegemea anipe hela ya matumizi!

Mzazi wangu nashindwa kumuomba maana yeye sasa hivi ana mitihani saa nyingine nikimsikiliza japo kwenye simu nataman hata kulia!! Sasa kwa sasa sina hata hela ya kula, nimekuwa mtu wa kuomba omba ili mradi tu nipate ya kula, ndani sina kitanda wala godoro nimelalia chini kwenye sakafu mpaka sasa najiuliza kwa nini mimi??

Kodi inakaribia kuisha nina karibia mwezi mmoja hivi kodi kuisha pia ninahitaji hela ya kulipia kwa mwezi kama umeme,maji na usafi n.k !! tangia nianze kusoma sijawahi kupata raha maana kila siku imekuwa ni mitihani tu!! nimemaliza chuo bado ni mitihani tu na naona inazidi!!

Nimesoma chuo bila mkopo na kushinda njaa ni kitu ambacho ni utaratibu wa kila siku ila kwa sasa mpaka inafikia hatua sijui kesho yake nitakula nini!!! Mtu unaweza kujiuliza kwamba kwa nini nisitafute kazi??? kazi zinataka ujuane na watu na pia kazi siwezi kuipata sasa hivi na nilipwe sasa hivi ukizingatia sasa hivi sina hata cheti!

Pia kuhusu kufanya kazi hata za kutwa nipate hela ya kula imekuwa ngumu kutokana na kwamba kila siku nimekuwa mtu wa kuzunguka kutafuta jinsi ya kutatua matatizo haya! kwa hiyo mpaka nikaona siwezi kupata mda wa kufanya kazi hata itakayonipatia elfu tano kwa siku!!

Nimehangaika sana kutafuta mtaji wa kuendeleza hii biashara yangu ila nimekitana na mitihani mingine zaidi maana sina nyumba wala ardhi wala leseni ili kuweka kama dhamana pia hata watu wanaotoa kwa riba nao wana masharti magumu sana ukizingatia sina kitu cha thamani zaidi kuweka kama bond!! Nimetafuta kwa ndugu,jamaa na marafiki ila kila mtu ananiambia hana hana kabisa mpaka ninabaki nikiwa sina jinsi ya kufanya nikaona nije hapa ili kuona kama kuna mtu ataweza kunisaidia katika hili!!

Mimi binafsi nimesomea biashara na ninapenda biashara! napenda sana ujasiriamali na nina ndoto kubwa sana za kutoka kimaisha na kuwa successful person hapo baadae!! Nina amini katika kupambana zaidi na nina penda kuchakalika huku na huku kufanya biashara! Pia nina uzoefu na kazi na hotel, mambo ya juice n.k

NINACHOHITAJI

Naomba mtu ambae anatamani na ana uwezo wa kunisaidia anisaidie maana nipo katika kipindi kigumu zaidi katika maisha! ninaomba mtu anikopeshe laki sita tu ili niweze kulipia kodi pamoja na kumalizia mradi wangu! kiasi nimeamua kulipia kodi kwa sababu vifaa vya kutumika katika uzalishaji ninavyo kama freezer, brender na juice dispenser ila ni marekebisho kidogo tu yanahitajika kuongezewa kwenye juice dispenser na hiyo baiskeli maalum niliyotengeneza!!! Kwa hiyo niko serious na hela hizi!!!

Ninaomba hata kama mtu akitaka kunikopesha kwa riba na tukaandikiana niko tiyari na akitaka niweke bondi vitu vyangu ntaomba vitu niendelee kuwa navyo maana ndivyo nitakavyokuwa natumia katika uzarishaji!!! Ila hata kama mtu atataka kujitolea kama msaada tu napenyewe nitashukuru sana maana na Mungu nae atamuongezea zaidi!

Usiwe na wasiwasi labda hela nitairudisha vipi ni kwamba nikipata hicho kiasi nitarekebisha juice dispenser yangu na nitaiweka sehemu penye watu wengi nina imani nitauza tu na ukizingatia juice ina faida tu nzuri na pia kwa hapa Dar es salaam itaenda vizuri. Pia kwa kutumia hiyo baiskeli nitamuweka kijana ambaye atasambaza mjini ili niwe na uhakika hela inarudi haraka sana! hata hivyo kwa kutumia freezer yangu naweza kuongeza biashara nyingine kama maziwa mtindi , ice cream,maji n.k! nima imani hela nitaweza kuirudisha!

Binafsi nilitamani milioni moja ili angalau nipate hata hela ya kununulia godoro au kitanda cha kawaida sana maana inaumiza sana kulala chini kwa mda mrefu! lakini kwa yeyote mwenye uwezo nitashukuru sana akinisaidia hiyo laki sita au akiweza hata milioni moja tu!

MATEGEMEO YANGU

Kama nikibahatika kwa siku nikatengeneza 20,000 haya yakiwa ni makadirio ya chini zaidi ina maana kwa mwezi nitapata laki sita! na pia kumbuka faida inaweza kuongezeka zaidi hata kufikia 40,000 na zaidi! kwa maana hiyo nitaweza kurejesha mkopo huo baada ya mda furani!

Naomba mtu mwenye uwezo aniamini maana naelewa hii ni pesa pia naelewa hichi ni kipindi kigumu sana pesa haipatikani kirahisi! lakin hata hivyo ntaomba mtu huyo aniamini sana maana nina uchungu sana na maisha !!!! pia mimi sio mtu wa starehe sinywi pombe,sivuti sigara,naishi mwenywe na sina mke wala mtoto! naomba msaada wenu tafadhari.

Atakayehitaji aniandikie sms DM ili tuweze kuwasiliana zaidi!
With all the due respect nathubutu kusema wewe ni Muongo! Na pia haupaswi kuaminiwa....nimepitia moja ya thread zako uliyowahi kuileta hapa....na humo ulituambia kwamba haukufanikiwa kumaliza chuo,uliishia mwaka wa pili kwa sababu ulizozitaja wewe! Lakini leo unaleta story kwamba chuo ulimaliza lakini bado haujapata Cheti.! Kwa Uongo huo tu nimejiridhisha kuwa haupaswi Kupewa dhamana! Naamini unajua vizuri naongelea nini
 
Huyu Kijana anaitaji Msaada. BAK nakukabidhi kwa huyu Kijana mkopeshee au MPE iyo hela anayouraji.Mungu atakulipa..Please tusipende kuwa Negative kwa kila jambo..Kuna Watu wanapitia Shida ninyi Acheni.Na Maisha ya Dar Hope mlioanzia Dar mnajua Ni Shida. Wizaea ya Vijana Kuna fungu la kuwawezesha vijana ila kupataaa. Nu URASIMU sana.All the best Young brother
 
mkuu umeelewka ila kwa sie watu wa humu tushakutana na utapeli wa kila aina,unayoyaongea binafsi umeniteka lkn sijui kwa nini nimekuwa mgumu kumuamini binadamu kwa sasa,sina sababu ya kutokukuamini lakini naomba niseme sikuamini kabisa,pamoja na kuwa mchanganuo wako umenishika na kuguswa,not bad try ur lucky,may be this is ur day,wishing u the bestest on ur hustler!

Unge MPM kumwambia Haya nafikiri ingekuwa vyema! Umekuwa negative na pengine angekuwa mtu mwingine hapa wa kumsaidia lakini Kwa ujumbe wako huu akakata tamaa.
 
Mleta mada inafika wakati unakubali matokeo tu. Ridhika na utakachopata iyo elfu 15 kwa siku kwa kubeba zege siyo mbaya. Ukitaka vitu vikubwa chini ya uwezo wako utazidi kukwama. Maisha ya ujanjaujanja hayasaidii kabisa.

Laki sita siyo mchezo kwa wabongo sasa hivi na ukata wa Magu. Hakuna atakayekukopesha. Halaf ni hulka yangu kutomuamini mtu anayeomba msaada kwa kujielezaa saaanaa.


USHAURI

Fanya kazi Bro kazi haimuui mtu na Ridhika na utakachopata hata kama kidogo utaish kwa aman.
 
Back
Top Bottom