Nahisi simpendi mke wangu

Duh ! Pole sana kaka mara nyingi huwa msoji lakini hii story imenivuta kuchangia. Kama ungebadilisha maelezo kidogo tu ningeamini wewe ni kaka yangu coz na anamatatizo kama haya kila anachofanya mwanamke anampinga ila wao wamefunga ndoa wana watoto watatu kama wewe lakini wote wa kile pole sana. Najua kuna baadhi ya watu ni ngumu kuamini lakini mimi nimeshuhudia kwa kaka yangu Kweli sometimes std 7 ni majanga, nakumbuka kaka angu alipata safari ya kikazi ila kwakua ni mbali aliruhusiwa kwenda na familia ticket zilikatwa ila cku ya safari mke kakataa alafu ni usafiri wa ndege ilibidi ampigie mama cmu kumuombea ili mke akubali kwenda akifanywa kuombwa kwenda kufika huko ni majanga wafanyakazi wa kike wakimsemesha ni kosa. All in all pole sana najua jinsi gani wanawake wa hivyo walivyo gundu na kuondoka hawataki atakusumbua sana ila mwisho wa cku wewe ndo mwenye maamuzi .
 

Kimsingi nimezungumza shida ya moyo wangu, kama ana shida ya moyo wake atazungumza kwenye jukwaa lake. Mimi na yeye tumeshakaa vikao vingi na mara nyingi huwa naishia kujuta kwa nini nimeanzisha mada. Kwa mfano, kuna kipindi nilitoka safari nikamkuta nje nikamsalimia nikaingia ndani, yeye alibaki nje. Nilitua vitu vyangu na kasha nikakaa chumbani. Baadae nilimpigia simu aje chumbani (ili nimuonyeshe kuwa nimemmiss) alipokuja nikaanza kumtania na kumchezea, baada ya muda akaniambia nimsubiri anakuja. Alitoka nje akaenda kukaa na housegirl, nilikaa chumbani kumsubiria mpaka nikapatwa na hasira nikaamua kuondoka. Nilimpita nje akiwa anapiga stori na housegirl wetu. Usiku niliporudi nikataka kikao naye, badala ya kuongea alikuwa anaangua kilio tuu, tukakaa siku mbili bila kulala. Badala ya mazungumzo ya kutafuta suluhu tunaishia kugombana.
N'way, una uhuru wa kuniona mkorofi kwa kuwa hunijui, hilo ni lako na huenda una experience na watu wa namna hiyo.
 

Kwaiyo wewe kwako unaona ni sawa dada zako kuwa close au kuchat na x wako wakati una mke? huo ni upuuzi na ndio chanzo cha matatizo alafu mnaleta JF kuomba msaada mke wangu haelewani na dada zangu wakati ulikuwa unachekelea upuuzi walokuwa wanafanya, mapenzi ni jambo la hisia na la kuliheshimu sio kulichezeachezea kama karata, vp wewe mkeo akiendelea kuchati na x boyfriend wake utaona vema tu sababu hujui walijuana vp? unapojibu hoja jaribu kutafuta umakini wa na uelewa na ujaribu kuiweka mgongoni kwako then utafaham uhalisia wake, likikukuta utajua starehe yake
 

Sikia ndugu, kwa sehemu kama hii unapoleta jambo lako, tegemea yote, kwahiyo usiumizwe na wachache wenye maoni tofauti, kuna vitu vingine mpaka vimkute mtu yeye kama yeye au mtu wa karibu yake ambako anaweza kushuhudia ndo aamini kwamba ni kweli yapo na yanatokea, mfano mtu anakulaum eti miaka 10 hujamuoa labda ndo sababu inamfanya awe hivyo, hivi kwa tabia hizo kweli mtu unaweza hata kushawishika kufungua ndoa?na isitoshe ulishajaribu akagoma mwenyewe, anyway binafsi naamini unachosema na hata kama wewe utakuwa na mapungufu lakini anayoyafanya mkeo ni extreme na hayana excuse ya aina yoyote, huyo kama hana mapepo basi anatabia ya asili ambayo ni mbaya, unajua kuna watu wengine wanatabia za ajabu na mbaya zaidi wao wanakuwa hawajijui na wanayotenda wanaona sawa tu na huwa ni ngumu kuwabadilisha na wengi mpaka hufikia uzee wako hivyo hivyo, sasa basi kwa kuwa wewe na yeye hakuna ndoa achana nae tu, gawaneni mlivyonavyo kila mtu aanze maisha mapya bila hivyo kama hata kuua kwa kudhamiria basi anaweza kuja kukusababishia maradhi yatakayokupeleka kaburini mapema sana, hebu jiulize mfano leo hii umepata stroke nazani unajua mgonjwa wa stroke anavyokuwa sasa unategemea atakuuguza huyo? ndo kwanza atabeba kila kitu akukimbie ndani ya nyumba akuache ufe peke yako au anaweza kukutilia sumu ufe haraka ili ajiepushe na kazi ya kukuuguza
 
sina tatizo la uelewa kama unavyodhani
maswali niliyokuuliza hujajibu hata moja
hujui ndoa ni nini
hata sheria ya nchi yako hujui inasemaje kuhusiana na ndoa
Una ufahau mdogo sana na mambo ya kanisa
aina za ndoa kisheria huzijui unang'ang'ana tu na taratibu zako(umeacha sheria ya Mugu ambayo ni NENO lake)
na Mungu hujui anasema nini juu ya mke na mme
Rafiki pia hujui maana ya kuzini

hujui hujui hizi nying nilizoandika rafik nahsi zitakuumiza!!! kwanza nisamehe pili kama ni vinginevyo binafsi tutaanzia pale uliposhauri lakini iwe kwa urafiki.
asante sana
 
Yaaani mkuu hilo ni zigo haswaa , maamuzi ni yako kulitua au kuendelea kukuchosha......

hutakaa uwe na amani au furaha maishani mwako ukimwendekeza huyo mwanamke..........

Almanusra na mimi yanikute hayo , japo mimi nilistuka katikati ya safari nikasepa.

huyo mwanamke utadhani umemcopy na kumpaste yuleee wa kwangu......... duh!!!!!!
 
Imeandikwa"Linda moyo wako kuliko vyote!alafu tambua mwanaume ni mfano wa Mungu,PIGA chini songa mbele mkuu..
 
Pole sana mpendwa sio bure wapo wanaomzuzua hembu mpe likizo kwanza huenda atajifunza na kuithamini ndoa yake hao wanampenda coz yupo anayegharamia wao wanajisevia tu kiulaini.
 

Ndugu mbona majina yanafanana
 
Mkw wako ana maneno sana, sasa hapo kazi unayo, huyo ndio tabia yk hawez kubadilika, pole sana
 
To,have foolish mom is not ure fault, but to have foolish wife is ure fault.
 

uko sahihi kabisa.
wanawake ni wavumilivu sana. ukiona kadilika au anareact ujue wewe nawe una vituko vyako vikubwa tu,huwezi vitaja hapa uko unamfanyia na amevichoka.
 
Kuna a saying that goes " Sometimes after marriage, a husband & wife became like two sides of a coin, they cant face each other but still stay together", Mkuu Goboshi ,pole sana kwa yaliyokukuta, ushauri wangu kama ndo zile ndoa zetu za kanisani, piga goti usali kwa maana nothing is impossible to the Almighty God, but if otherwise achana na huyo mdada maana ana-elements za kichawi!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…